Aliyekutwa katika tairi la ndege Uholanzi ni Mkenya

Maafisa wa polisi wa Uholanzi wamethibitisha kwamba mtu aliyekutwa katika tairi la ndege katika uwanja wa ndege wa Schipholni raia wa Kenya mwenye umri wa miaka 22.

Anapanga kuwasilisha ombi la kuchukua hifadhi nchini Uholanzi.

Mtu huyo alipatikana akiwa hai na kuwa na uwezo wa kuzungumza.Kwasasa anapokea matibabu katika hospitali moja.

Alikutwa katika tairi la ndege ya Cargolux baada ya ndege hiyo kusafiri kutoka Johhanesburg hadi nchini Uholanzi kupitia Nairobi Kenya.

Msemaji wa jeshi la polisi nchini Uholanzi aliasema inatarajiwa kwamba ataomba hifadhinchini Uholanzi , lakini kwasasa hali yake ya kiafya ndio muhimu.

Sio kawaida kwa stowaway katika safari za mwendo ,mrefu kukutwa wakiwa hai, kutokana na baridi kali na upungufu wa hewa ya oksijeni angani.

Maafisa wa polisi wa Uholanzi wanachunguza iwapo alijificha katika tairi hilo akiwa nchini Afrika kusini au Kenya.

Katika kipindi cha miaka mitano , watu saba waligunduliwa katika ndege hizo za Uholanzi na ni wawili pekee waliokutwa wakiwa hai.
Wa-Dutch watakuwa wamesikitika sana kwa tukio hili. "Be careful", huwa wanapenda sana kutumia neno hli. Sasa mtu alikuwa kenye tairi la ndege, na hizi ndege za masafa marefu huwa zinapaa futi 30,000 juu (au zaidi) ambako nadhani ubaridi wa anga lake ukijaribu kutoa mkono nje kwa sekunde moja tu mkono unaganda!
Watakuwa wamemuonea huruma sana
 
Kwenye matairi alijifichaje mkuu?.

1643107201582.png
 

Where do stowaways hide on planes?​



Where do stowaways hide on planes?Close

A suspected stowaway who is believed to have fallen from the landing gear of a flight bound for Heathrow Airport has been found dead in a Clapham, London, garden.
A neighbour says the body - believed to be that of a man - landed just a metre away from someone sunbathing on Sunday afternoon.
Police think the he'd hidden on a Kenya Airways flight from Nairobi.
After a similar case in 2013, in which Jose Matada died, the BBC's Rob Walker investigated the area that some stowaways hide in on passenger jets.


 
Hao wanaitwa mabaharia hata bongo wapo wanaojificha chini ya axle za nyuma za mabus yale yenye dabo diff toka mikoani waje dar jiji la bashite kama bahati sio yao kwenye bumps huwa wanabamizwa kama bahati ni yao wanatoboa hadi mbezi wanajificha hadi saba.

Wengine wanadandia tenk au contena juu usiku maadamu wafike dar.
Hii kuweka roho rahani ni kazi kweli.
 
Ahaaaa dah kweli watu wanajua ku risk maisha. Ahaaa utasikia airport kuna full security 24hrs😂😂😂 nyooolo zao sasa huyo aliingiaje bila kuonekana?
Hua ni mikwala tu maana huyo si wa kwanza kufanya hivyo ni mara kwa mara.
 
Back
Top Bottom