Tulia!! Iko hivi: Kama hujafika kwenye ukomo wa ngazi yako, na mwajiri wako ameridhia upate nyongeza ya mwaka kwa maana ya kuwa ameridhika na utendaji wako kwa mujibu ya tathmini yake ya mwaka, hapo ni haki yako kupata nyongeza ya mwaka. Ila kama umefika kwenye ukomo wa ngazi yako, huwezi kupata nyongeza ya mwaka. Kitakachokuvusha hapo ni promosheni! Kwa mfano kwenye ngazi ya TGS D ukomo wake ni TGS D12 Tsh. 930,000/=. Aliye kwenye TGS D12 hawezi kupata nyongeza ya mwaka ya sh 15,000/=. Huyu atasubiri hapo atakapopata promosheni na kupandishwa daraja hadi TGS E1 sh 1,000,000/= kwa mwezi.
Kwa kifupi, kupata nyongeza ya mwaka siyo automatic! Ni mpaka vigezo vitimie!! vigezo vyenyewe ni mwajiri wako aridhie kwa mujibu wa utendaji wako wa kazi na pia uwe hujafika kwenye ukomo wa ngazi yako ya mshahara.
MUHIMU: Kama mwajiri asiporidhia kukuongeza nyongeza ya mwaka sheria inamtaka ni LAZIMA akujulishe hivyo kwa barua rasmi, akiainisha sababu za kutokupata kwako nyongeza ya mwaka. Kama hujawahi kujulishwa hilo na nyongeza ya mwaka usipewe, hapo una HAKI ya kuidai!!