Aliyebambikiwa kesi ya mauji Tanzania ni Mussa Sadiki wa Tabora tu au kuna wengine wengi? Tujadili...

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,526
13,014
Bwana Mussa Sadiki alibambikiwa kesi ya mauaji huko Tabora! kwa mujibu wa DPP, aliandika barua ya wazi kwa Mkuu wa nchi kupitia gazeti la Majira uk 6.halijatajwa tarehe wala toleo.

Barua ikamfikia mwenye nchi na akaisoma kwa kuwa ilikuwemo gazetini ingeenda kwa posta nina uhakika isingefika.
Rais kwa kuguswa na suala lile aliagiza DPP afanye uchunguzi na afuatilie suala lile kwa undani wake, alifanya hivyo na kugundua kuwa sio kweli. Leo bwana Mussa Sadiki na mwenzake wapo nje.

Kkwa mujibu wa bwana Mussa Sadiki, kituo cha polisi Tabora mjini ni mahala pabaya kwani watu hubambikiwa kesi za mauaji na kuozea ndani.

Kwa mujibu wa DPP uchunguzi unaendlea na askari kadhaa wameshachukuliwa hatua za kinidhamu japo hajazitaja.

Nilijiuliza maswali baada ya kusikia habari ile kupitia Uhai radio fm.

1. Je, ni watu wangapi wapo magerezani kwa makosa ya kubambikiwa kama ya mauaji, ulawiti, ubakaji na uhujumu uchumi?

2. Je, ni wangapi wanaweza kufikisha maoni na malalamiko yao kwa Rais kupitia Magazeti?

3.Je, ni kituo cha Central Tabora tu au hata kwingineko watu hubambikiwa kesi?

4. Rais anawasaidiaje wale wengine ambao hawawezi kumfikia kama alivyomfika bwana Mussa Sadiki?

5. Je, sio kweli sasa kwamba wakati umefika wa kuunda tume ya kijaji kupitia magereza na mahabusu zote ili kujua nani na nani wapo huko mahabusu tangu lini na kwa sababu zipi?

Tujadili
 
Tatizo letu siku zote badala ya ku deal na mfumo unayosababisha hayo tu deal na tukio!! Na watu wanapongeza, wakati chimbuko la haya ni mfumo ambao ni wa ovyo!! Mambo ya kumbambikiwa kesi ni mengi mno karibia kila sehemu, na watu wanafungwa sana tu, sasa badala ya kuangalia au kuweka mfumo ambao utasaidia kuondoa uhuni huo, tunakimbilia tukio na kuona kuwa haki imetendeka?!!! Hapo kuna shida toka zamani watu walishasema kuwa polisi wawe wakamataji tu, halafu pawe na wapelelezi ambao sio polisi kabisa, iwe ni idara nyingine kabisa. Sasa leo polisi ndio mkamataji, ndio apeleleze hiyo case kuna nini hapo?
 
Naunga mkono hoja zifuatazo.

Mosi, Iundwe TUME YA KIJAJI IPITIE MAHABUSU NA MAGEREZA YOTE ICHUNGUZE WATU WALIOBAMBIKIWA KESI KWA KUANZIA NA HUKO TABORA.

Pili, POLIS wabaki kuwa wakamataji tu, Wapelelezi iundwe idara nyingine kabisa inayojitegemea.
 
Tatizo letu siku zote badala ya ku deal na mfumo unayosababisha hayo tu deal na tukio!! Na watu wanapongeza, wakati chimbuko la haya ni mfumo ambao ni wa ovyo!! Mambo ya kumbambikiwa kesi ni mengi mno karibia kila sehemu, na watu wanafungwa sana tu, sasa badala ya kuangalia au kuweka mfumo ambao utasaidia kuondoa uhuni huo, tunakimbilia tukio na kuona kuwa haki imetendeka?!!! Hapo kuna shida toka zamani watu walishasema kuwa polisi wawe wakamataji tu, halafu pawe na wapelelezi ambao sio polisi kabisa, iwe ni idara nyingine kabisa. Sasa leo polisi ndio mkamataji, ndio apeleleze hiyo case kuna nini hapo?
Umeongea vyema sana .. kama kila kituo kidogo kingekuwa kina fungwa camera .. halafu system ya kuzi operate camera hiyo ingekuwa ipo chini ya wizara husika hayo mambo yote yange toweka yasingelikuwepo .....

Ila ngojeeni kwanza tujenge airport chato ... maybe tukimaliza hii project tutaifanya hiyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwingine Mimi hapa, demu wangu alinibambikia kesi kuwa Nina mchepuko.....wakati haikuwa kweli
 
Polisi wapunguziwe kazi ya kupeleleza na mimi naunga mkono iundwe idara nyingine. Iwe na wenye taaluma ya sheria tena iwe ya upelelezi ya makosa ya jinai mauaji ugaidi rushwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bwana Mussa Sadiki alibambikiwa kesi ya mauaji huko Tabora! kwa mujibu wa DPP, aliandika barua ya wazi kwa Mkuu wa nchi kupitia gazeti la Majira uk 6.halijatajwa tarehe wala toleo.

Barua ikamfikia mwenye nchi na akaisoma kwa kuwa ilikuwemo gazetini ingeenda kwa posta nina uhakika isingefika.
Rais kwa kuguswa na suala lile aliagiza DPP afanye uchunguzi na afuatilie suala lile kwa undani wake, alifanya hivyo na kugundua kuwa sio kweli. Leo bwana Mussa Sadiki na mwenzake wapo nje.

Kkwa mujibu wa bwana Mussa Sadiki, kituo cha polisi Tabora mjini ni mahala pabaya kwani watu hubambikiwa kesi za mauaji na kuozea ndani.

Kwa mujibu wa DPP uchunguzi unaendlea na askari kadhaa wameshachukuliwa hatua za kinidhamu japo hajazitaja.

Nilijiuliza maswali baada ya kusikia habari ile kupitia Uhai radio fm.

1. Je, ni watu wangapi wapo magerezani kwa makosa ya kubambikiwa kama ya mauaji, ulawiti, ubakaji na uhujumu uchumi?

2. Je, ni wangapi wanaweza kufikisha maoni na malalamiko yao kwa Rais kupitia Magazeti?

3.Je, ni kituo cha Central Tabora tu au hata kwingineko watu hubambikiwa kesi?

4. Rais anawasaidiaje wale wengine ambao hawawezi kumfikia kama alivyomfika bwana Mussa Sadiki?

5. Je, sio kweli sasa kwamba wakati umefika wa kuunda tume ya kijaji kupitia magereza na mahabusu zote ili kujua nani na nani wapo huko mahabusu tangu lini na kwa sababu zipi?

Tujadili
Tatizo la kubambikiwa kesi ni kubwa sana kuliko watu wanavyofikiria. Na hii yote ni katika kutafuta rushwa au kukukomoa mhusika
 
Kuna shida pahala ngoja kwa leo nikae kimya
YESU aliyajua haya na aliwaasa kwa kuwaambia
"Msidhurumu
Msishitaki kwa uongo
Rizikeni (toshekeni) na mishahara yenu "
Shida ipo hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi wapunguziwe kazi ya kupeleleza na mimi naunga mkono iundwe idara nyingine. Iwe na wenye taaluma ya sheria tena iwe ya upelelezi ya makosa ya jinai mauaji ugaidi rushwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mkuu hili sekeseke ni la kikamataji ama ni la kipelelezi pekee?

Nionavyo mimi iundwe kamisheni ya kumonita malalamiko ya mahabusu na wafungwa Tz nzima.

Makosa ya makusudi na ya kinyama yanayofanywa na watendaji kuonea watu yana mnyororo mrefu.

Kuna hao polisi kubambika kesi na kubambikia makosa kwa njia ya upelelezi. Kuna mahakimu kwa makusudi wanaopotosha tafsiri za kisheria na kupelekea kutia adhabu isiyostahili ama ya kiuonevu kwa watu.

Kuna waandika mashitaka wana uwezo wa makusudi wa kuvuruga uandikaji wa mashitaka kwa minajili ya kuwapendelea waharifu ama kuwakandamiza watu na mifano mbalimbali ipo.

Iundwe tume mahsusi sasa ya kufuatilia malalamiko ya watu kisha wabaini ukweli na kisha wale wote waliobambikia watu kwa kuwakamata bila makosa, kuandikia mashitaka na kutoa ushahidi wa uongo na mahakimu waliopotosha hukumu, wote hao washuhulikiwe ipasavyo bila ya kuangalia sura zao maana ni mashetani wakubwa waliotufikisha tulipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom