Mzizi wa Mbuyu
JF-Expert Member
- May 15, 2009
- 7,320
- 6,806
Ni miaka kumi na mbili sasa, lkn nalikumbuka tukio hili kama limetokea leo hii...
Nilikuwa nimetoka kazini muda wa saa nne hivi asubuhi naendesha gari ya ofisi kueklekea airport ya JK Nyerere, ghafla nikasikia kishindo kikubwa nyuma ya gari. Nikajua nimepata matatizo ya tairi ya gari hivyo nikaisogeza gari pembeni kabisa kushoto mwa barabara..ili kuweza kuyapisha magari mengine yaliyokuwa yana pita kwa kasi mno ktk barabara hiyo ya Nyerere upande wa kutokea Tazara..
Nilijishika kiunoni kwa mikono miwili ikiwa ni dalili za kukata tamaa, baada ya kushuka chini ya gari na kugundua tairi ya nyuma kushoto imepasuka vibaya sana...na kwa muundo wa gari hiyo Toyota Hilux pick up inabidi kuanza kukorokochoa chini ya gari kwa nyuma ambako kulikuwa kumejaa matope kiasi hata tairi ya akiba ikawa inaonekana ni tope pia.
Nilipokuwa katika hali hiyo, ndipo ghafla nikamwona ghafla mtu wa makamo hivi mbele yangu mwnye miaka kama 45 hadi hamsini hivi. Alikuwa na mwili mkubwa na kifua kipana hivi, ingawa sura yake ilikuwa kama imekauka kauka hivi kwa mazoezi au sijui nii bwana lakini ndivyo alivyokuwa kwa mtazamo wangu.
Yule mtu akaniangalia huku akitabasamu hivi...akaniambia "pole bwana?' nikajibu 'ah" huku nikiwa kama nina huzunika hivi...
Ngoja nifupishe kisa hiki nisije wakwaza watu humu.....
Jamaa yule akaamua kunisaidia kuitoa ile tairi ya akiba na kuifunga badala ya ile iliyo pasuka....lakini wakati wa shuguli nzima tukawa tunaongea stori za hapa na pale jamaa akiwa yeye ni msemaji zaidi maana mimi nilikuwa naogopa jamaa atanidai pesa kubwa mnop baada ya kazi ile, na alikuwa mkubwa kwangu kwa wakati huo mie nilikuwa na miaka 26 na ushee hivi.
Jamaa akanieleza mambo mengi, Majina yake na kuwa yeye ni dereva maroli ya mizigo yaendayo nje ya nchi...na mkewe ni mwalimu anafundisha shule fulani(akanitajia na shule!) Maeneo ya Kigogo na yeye anaishi hukohuko kigogo n.k...
Sasa twende kwenye tikio....
Baada ya jamaa kumaliza nikatoa shilingi 3 ,000 jamaa akakataa, ni kaongeza buku jamaa akasema hata 20,000 hapokei anajua matatizo ya magari amenisaidia tu....nikamshukuru mno yule bwana , sanasan! akasema usijali bwana mdogo wakati mwingine na wewe mtu akipata matatizo msaidie tu bila kumdai malipo.... ndiyo ubinaadamu...!!
Akawa anasema hivyo huku anatroti kuvuka barabara.....akavuka kipande kinachokwenda uwanja wa ndege.....
nikawa nimesimaa namwangalia....na kumshangaa jinsi alivyo na roho nzuri...akageuka, akanipungia mkono na kuingia kipande kinachotoka uwanja wa ndege...
Tukio hili lilitokea kwa kama dakika tu...ndugu yangu laki ntajitahidi kukujulisha hivyo hivyo..
Ghafla alipokuwa amepiga hatua kama mbili tu kutaka kuvuka..gari ikaja kwa spidi kubwa!! jamaa aagh! sijui nisemeje jamaa akagongwa kwa kishindo cha jabu kabisa na kurushwa juu!! alipotua ktkt ya lami gari ingine kama fuso hivi ikaja kwa nyuma ikampanda! na kupitiliza japo iliyumba mno lkn hatimaye ikaendelea na safari....
Hapo nipo nilipopata fahamu, nikakimbia kwenda upande ule ili kuzuia magari yasiendelee kuja....sijui kama niliweza kwani ni kama nilichanganyikiwa hivi kwa nilikuwa nalia na macho yangu yame jaa machozi...
Nilipoona gari gari haziji tena nikatimua mbio kwenda kumpa msaada yule jamaa pale alipo angukia na kupitikwa na gari nyingine...nilichokiona hapo..!! kilikuwa kitu amabacho siomei tena kuja kukiona na wewe usiombe! utumbo, moyo, maini mfupa wa kichwa umekwanguliwa na kuwa mweupeee! Huku pembeni yake damu ikitoka kwa spidi ya ajabu kabisa! kifua kilikuwa kinamwaga damu nyiingi kweli jamani binadamu anadamu nyingi!!
Gari iliyomgonga mara ya kwanza pia ilifanikiwa kukimbia ingawa nakumbuka niiona ikienda nje kasa ya barabara karibu na mtaro hivi...lakini nilipozinduka kutaka kuifuatilia ndiyo ikawa inaingia main road na kutokomea kwa spidi! hata namaba sikuweza kuisoma kwani macho yangi yalijaa machozi!!
Nimalizie hivi, maiti ya jamaa yule ilipelekwa hsp kwa gari yangu....mimi ndiye niyeenda kumtaarifu mkewe jamaa si aliniambia anafanya kazi wapi! lkn sikwenda 1kwa1 nikaenda kwanza kwa mwalimu mkuu nikamweleza kuusu ile ajali lakini sikusema jinsi jamaa alivyonisaidia ....taratibu zikafuatwa...mambo yakaendelea..
Mwisho kabisa nikwamba mie siku hiyo kazi haikufanyika tena, niliporudi kazi jioni ofisi zilikuwa zimefungwa na nilikuwa nimetoa taarifa kuwa nimefiwa na mjomba wangu nimepitia huko bahati nzuri bosi alinielewa..na kesho yake sikwenda kazini..nikaenda msibani Kigogo.
Nilipofika watu walikuwa wengi sana na mie nika kwa mmoja kati ya marafiki wa marehemu lkn bado sikumwabia mtu kisa cha yule bwana kunisaidi Askari mmoja alinionya tulipokuwa hosipitali nisiseme eti kwatu wanaweza kuielewa vibaya, nili tii ushauri wake. Nikajipenyeza hadi ..ndani..ndni kabisa walipokuwa kinamama nikafanikiwa kumkuta mke wa marehemu amaezungukwa na kinamama..nikaenda kumpa mkono niliokuwa nimefutika Shilingi50,000 akazipokea...
Basi bwana,nilipotoka nje nikawa sina cha kufanya tena nikawa naondoka eneo hilo..lakini moyo wangu ukiwa na majonzi makuu, sikuwa na gari siku hiyo.. hivyo nikawa nasikia sauti za nymbo ya kuomboleza nikama zikawa zinanisindikiza, kila ninapopiga hatua nikwa nasikia zinafifia ...PALAPANDAAAA..ITALIAAPALAPANDA!..PALAPANDAAAA..ITALIAAPALAPANDA!.....
...................................................................................................................
Kisa hiki ni cha kweli kabisa kilicho wahi kunikuta wadau wenzagu, Nauliza ulikuwa mkosi, balaa, nuksi au kitu gani???!!!!
Nilikuwa nimetoka kazini muda wa saa nne hivi asubuhi naendesha gari ya ofisi kueklekea airport ya JK Nyerere, ghafla nikasikia kishindo kikubwa nyuma ya gari. Nikajua nimepata matatizo ya tairi ya gari hivyo nikaisogeza gari pembeni kabisa kushoto mwa barabara..ili kuweza kuyapisha magari mengine yaliyokuwa yana pita kwa kasi mno ktk barabara hiyo ya Nyerere upande wa kutokea Tazara..
Nilijishika kiunoni kwa mikono miwili ikiwa ni dalili za kukata tamaa, baada ya kushuka chini ya gari na kugundua tairi ya nyuma kushoto imepasuka vibaya sana...na kwa muundo wa gari hiyo Toyota Hilux pick up inabidi kuanza kukorokochoa chini ya gari kwa nyuma ambako kulikuwa kumejaa matope kiasi hata tairi ya akiba ikawa inaonekana ni tope pia.
Nilipokuwa katika hali hiyo, ndipo ghafla nikamwona ghafla mtu wa makamo hivi mbele yangu mwnye miaka kama 45 hadi hamsini hivi. Alikuwa na mwili mkubwa na kifua kipana hivi, ingawa sura yake ilikuwa kama imekauka kauka hivi kwa mazoezi au sijui nii bwana lakini ndivyo alivyokuwa kwa mtazamo wangu.
Yule mtu akaniangalia huku akitabasamu hivi...akaniambia "pole bwana?' nikajibu 'ah" huku nikiwa kama nina huzunika hivi...
Ngoja nifupishe kisa hiki nisije wakwaza watu humu.....
Jamaa yule akaamua kunisaidia kuitoa ile tairi ya akiba na kuifunga badala ya ile iliyo pasuka....lakini wakati wa shuguli nzima tukawa tunaongea stori za hapa na pale jamaa akiwa yeye ni msemaji zaidi maana mimi nilikuwa naogopa jamaa atanidai pesa kubwa mnop baada ya kazi ile, na alikuwa mkubwa kwangu kwa wakati huo mie nilikuwa na miaka 26 na ushee hivi.
Jamaa akanieleza mambo mengi, Majina yake na kuwa yeye ni dereva maroli ya mizigo yaendayo nje ya nchi...na mkewe ni mwalimu anafundisha shule fulani(akanitajia na shule!) Maeneo ya Kigogo na yeye anaishi hukohuko kigogo n.k...
Sasa twende kwenye tikio....
Baada ya jamaa kumaliza nikatoa shilingi 3 ,000 jamaa akakataa, ni kaongeza buku jamaa akasema hata 20,000 hapokei anajua matatizo ya magari amenisaidia tu....nikamshukuru mno yule bwana , sanasan! akasema usijali bwana mdogo wakati mwingine na wewe mtu akipata matatizo msaidie tu bila kumdai malipo.... ndiyo ubinaadamu...!!
Akawa anasema hivyo huku anatroti kuvuka barabara.....akavuka kipande kinachokwenda uwanja wa ndege.....
nikawa nimesimaa namwangalia....na kumshangaa jinsi alivyo na roho nzuri...akageuka, akanipungia mkono na kuingia kipande kinachotoka uwanja wa ndege...
Tukio hili lilitokea kwa kama dakika tu...ndugu yangu laki ntajitahidi kukujulisha hivyo hivyo..
Ghafla alipokuwa amepiga hatua kama mbili tu kutaka kuvuka..gari ikaja kwa spidi kubwa!! jamaa aagh! sijui nisemeje jamaa akagongwa kwa kishindo cha jabu kabisa na kurushwa juu!! alipotua ktkt ya lami gari ingine kama fuso hivi ikaja kwa nyuma ikampanda! na kupitiliza japo iliyumba mno lkn hatimaye ikaendelea na safari....
Hapo nipo nilipopata fahamu, nikakimbia kwenda upande ule ili kuzuia magari yasiendelee kuja....sijui kama niliweza kwani ni kama nilichanganyikiwa hivi kwa nilikuwa nalia na macho yangu yame jaa machozi...
Nilipoona gari gari haziji tena nikatimua mbio kwenda kumpa msaada yule jamaa pale alipo angukia na kupitikwa na gari nyingine...nilichokiona hapo..!! kilikuwa kitu amabacho siomei tena kuja kukiona na wewe usiombe! utumbo, moyo, maini mfupa wa kichwa umekwanguliwa na kuwa mweupeee! Huku pembeni yake damu ikitoka kwa spidi ya ajabu kabisa! kifua kilikuwa kinamwaga damu nyiingi kweli jamani binadamu anadamu nyingi!!
Gari iliyomgonga mara ya kwanza pia ilifanikiwa kukimbia ingawa nakumbuka niiona ikienda nje kasa ya barabara karibu na mtaro hivi...lakini nilipozinduka kutaka kuifuatilia ndiyo ikawa inaingia main road na kutokomea kwa spidi! hata namaba sikuweza kuisoma kwani macho yangi yalijaa machozi!!
Nimalizie hivi, maiti ya jamaa yule ilipelekwa hsp kwa gari yangu....mimi ndiye niyeenda kumtaarifu mkewe jamaa si aliniambia anafanya kazi wapi! lkn sikwenda 1kwa1 nikaenda kwanza kwa mwalimu mkuu nikamweleza kuusu ile ajali lakini sikusema jinsi jamaa alivyonisaidia ....taratibu zikafuatwa...mambo yakaendelea..
Mwisho kabisa nikwamba mie siku hiyo kazi haikufanyika tena, niliporudi kazi jioni ofisi zilikuwa zimefungwa na nilikuwa nimetoa taarifa kuwa nimefiwa na mjomba wangu nimepitia huko bahati nzuri bosi alinielewa..na kesho yake sikwenda kazini..nikaenda msibani Kigogo.
Nilipofika watu walikuwa wengi sana na mie nika kwa mmoja kati ya marafiki wa marehemu lkn bado sikumwabia mtu kisa cha yule bwana kunisaidi Askari mmoja alinionya tulipokuwa hosipitali nisiseme eti kwatu wanaweza kuielewa vibaya, nili tii ushauri wake. Nikajipenyeza hadi ..ndani..ndni kabisa walipokuwa kinamama nikafanikiwa kumkuta mke wa marehemu amaezungukwa na kinamama..nikaenda kumpa mkono niliokuwa nimefutika Shilingi50,000 akazipokea...
Basi bwana,nilipotoka nje nikawa sina cha kufanya tena nikawa naondoka eneo hilo..lakini moyo wangu ukiwa na majonzi makuu, sikuwa na gari siku hiyo.. hivyo nikawa nasikia sauti za nymbo ya kuomboleza nikama zikawa zinanisindikiza, kila ninapopiga hatua nikwa nasikia zinafifia ...PALAPANDAAAA..ITALIAAPALAPANDA!..PALAPANDAAAA..ITALIAAPALAPANDA!.....
...................................................................................................................
Kisa hiki ni cha kweli kabisa kilicho wahi kunikuta wadau wenzagu, Nauliza ulikuwa mkosi, balaa, nuksi au kitu gani???!!!!