Aliniacha miaka mitano sasa ananilaumu nifanyaje?

Aliniacha miaka mitano sasa ananilaumu nifanyaje?

CHEO73VWgAAetpl.jpg
 
ni kweli kwanza sasa hivi niko kazini ninajitegemea, simtegemei kwa lolote ila anataka anitawale nikae nanyenyekea mtu hewa ambaye hakuwahi kuliona hata tumbo langu hadi mtoto mwenyewe miaka minne sasa,
believe in your self you are beautfull na una future nzuri tu pendeza vizuri kaa vizuri usiwe mtu wa majuto jiweke vizuri kula vizuri kaa na mwanao vizuri
uwe na muenekano mzuri tu usijiachie na kikubwa FUNGUA MOYO WAKO KWA MTU MWINGINE
achana na huyo jamaa kama unataka kuishi kwa amani
kama unataka usi enjoy maisha mpaka unaingia kaburini ENDELEA KUMFIMFIKIRIIA JAMA
 
hili nalo lisikusumbue apite vileee mbali na ww.. dear tengeneza maisha yako andaa msingi usiotetereka huyo mtoto anakuangalia wewe.. ko asikupe stress zisizo na mwelekeo coz usipo angalia atakudundika mtoto wa pili afu apotee tena baada ya miaka mitanoo ndo atajitokeza tena..
all in all kaa macho yan ucpepese ata kidogo utadanganywa tena
 
ni kweli kwanza sasa hivi niko kazini ninajitegemea, simtegemei kwa lolote ila anataka anitawale nikae nanyenyekea mtu hewa ambaye hakuwahi kuliona hata tumbo langu hadi mtoto mwenyewe miaka minne sasa,

Mi ningekatisha mpaka Mawasiliano na ndugu zake.
 
Nakushauri ufanyie kazi ushauri wake kuwa tumia akili ujiongeze.
 
Habari ndugu zangu wa jf. naamini hapa huwa napata ushauri usio na hila.
Mimi ni mwanamke niko single, niliachana na mwanaume huyu baada ya kumweleza kuwa nimepima nikakuta nina ujauzito wa mwez mmoja, aligomba sana na mimi pamoja na kwamba kweli nilikuwa nimemwamini na kufungua moyo kumpenda, sikuona sababu ya kujipa shida niliwataarifu wazazi wangu wakanitia moyo nikalea ujauzito miezi vote tisa (bila yeye kutamani hata kuliona hilo tumbo maana niliamua kuondoka DSM kurudi mkoani baada ya yeye kugoma).

hata baada ya kujifungua hakuja kuniona alituma ndugu same kumwona mtoto na akasistiza kwamba hawakuja kuchumbia ni kumwona mtoto tu. haikunipa shida. Alinitumia matumizi ya mtoto hadi mtoto alipotimiza mwaka mmoja akastop kwa sababu kwamba amepata majukum ya kishule, nikamwelewa haikunisumbua. Lakini mda mfupi baadaye akaniambia amepata mtoto kwa mama mwingine, japo sikutaka kuhoji logic ya yeye kunipa taarifa hiyo, haikunisumbua pia. ndugu same tunawasiliana vizuri japo yeye hadi leo hii mtoto anaelekea mwaka wa nne sijamwona na mwanzoni mwa mwaka aliniambia mda wote huu tuliokaa mbali basi niwe na akili ya kujiongeza, haikunisumbua pia.

Kinachonifanya niombe mawazo yenu ndugu zangu ni hiki; hivi karibuni amekuwa na mawasiliano ya karibu kila siku na mimi kwamba anahitaji aje tuonane akauliza kama nimewahi kuwa na mahusiano humu katikati nikamjibu NDIYO, kwani muda wenyewe ulikuwa mrefu sikuona juhudi same zozote kwangu na mimi ni binadamu. japo kwa kweli sikuwa nimefikiria kuolewa na mwanaume mwingine zaidi yake hadi leo hii. Kilichotokea hapo nimetukanwa nimeonekana Malaya mimi na kwamba hana tena hamu ya kuniona japo alitaka tupange habari za ndoa. nimejiuliza kosa langu ni lipi sikuona, nimewaza labda anatafta sababu za kujustfy maamuzi yake ya kutokuwa na mimi au ni vipi.... mawazo yenu plz hata kama nimekosea niambiwe.[/QUOTE

Embu muulize kasahau nini kwako?
 
ni kweli kwanza sasa hivi niko kazini ninajitegemea, simtegemei kwa lolote ila anataka anitawale nikae nanyenyekea mtu hewa ambaye hakuwahi kuliona hata tumbo langu hadi mtoto mwenyewe miaka minne sasa,

Binti yangu, achana na huyo ndorobo! Wa kwako bado anakuja, meanwhile mmeo awe kazi yako.
 
Khaaaa
Kakuacha miaka 5
Karudi from nowherw nawe unakubali mazungumzo ya namna hiyo????

Mbona wanawake hamjithamini?????

Yaani huyo mwanaume kama ana swichi anawasha na kuzima atakavyo???

Khaaaaa
 
Mhhhhhh pole mpendwa.mume wako yuko anakuja usijali.n usilazimishe na usitumie moyo kuamua wakati mwingine.tumia akili lv n uruhusu kumpokea mwanaume mwingine.na ushauri wangu wa maana zaidi ni KUSALI TU.hiyo njia itakuletea mume yaani ubavu wako ambae atabeba tatizo lako kama lake
 
Achana na huyo mtoa mbegu .. siyo mume huyo ni mbegu donor

wanawake kwanini mnakuwa hvi? kuna jamaa alisemaga kuwa alimsemea mkewe kwamba anatumia vyeti fake, mkamuombea msamaha sana yule dada lakn leo humu michango yenu karibia wote mnataka amuache jamaa, hii sio sawa
 
Kwa uvumilivu huo kama ni kweli, njoo kwangu tu.
 
Mi mwezi tu usiponitafuta ndo nafuta namba yako
 
Cheka na kima. ,utakuja kufungua thread ya mimba ya pili
 
Jamii forum mtu kuwa n.a. I'd Saba na akazitungia uzi na kuujibia ni saw a.Funguo moja vitasa kumi
 
Thats why i warn people each and every single day that mary a single mother for your own peril unless otherwise the father of the kid is dead.
 
Back
Top Bottom