Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Wana JF,
Mtabaini kwamba Omutwale nimekuwa Passive member hapa JF. Lakini katika siku hizi mbili uvumilivu wa kubaki msomaji na kugonga thanx umeshindikana. Najifunza kuandika.(Nisamehe nikiku-bore) baada ya kusikia kauli za-kina Mama Simba na Mkuchika wakimbeza Mzee Mzalendo, Bwana Reginard Mengi. Kauli hizi mbili zikifuatiwa na nyongeza ya mtazamo wa M/Kiti wa chama kinachoendelea kupoteza dira, Prof. Ibrahim Lipumba pamoja na tamko lililotolewa jana na vijana wa uvccm toka Tabora vilinifedhehesha na kuninyongonyesha saaana. Wapendwa wana neno stahili kwa hali iliyonipata linaitwa Roho kuugua
Roho yangu iliugua kutokana na mambo makuu mawili:
Moja, kuona serikali kupitia Mawaziri wake imeamua kubainisha wazi upande wake katika vita hii dhidi ya ufisadi na mafisadi papa. Kinyume na matarajio na fikra za walio wengi, sasa ni wazi serikali inapigana vita toka kona/upande wa ufisadi na mafisadi papa ikishambulia wenye nia njema na nchii hii (yetu sote) waliojitoa muanga hadharani kupingana na ufisadi na mafisadi papa.
Pili, Roho yangu iliugua kutokana na kuchanganyikiwa kwa wadanganyika na kuibuka kwa wananchi-maslahi waliojitokeza kuwatetea mapapa waliotajwa. Miongoni mwao ni waliojiita wazee wa yanga wakimtetea manji na wale vijana toka Tabora wakimtetea Rostam.
La pili liliniumiza zaidi maana serikali inaweza kuwa mbovu wananchi wenye umoja na uelewa wakairekebisha, lakini jamii/wananchi waliowabovu na wasio na umoja hawawezi kuirekebisha serikali mbovu. Hii ilinisukuma kutaka kujua uelewa wa wananchi na msimamo wa walio wengi juu ya masuala ya ufisadi na mafisadi papa. Napenda niwashirikishe wana JF, kwa mara nyingine tena, algebra za CCM na Serikali yetu kwa ujumla zimeenda alijojo. Kauli zilizotolewa na Mawaziri ziliwakadiria wadanganyika kuwa bado wako 1947! lakini nilchobani watanganyika wako oktoba 2010, mwaka mmoja mbele ya CCM na Serikali yetu wakingoja kwa hasira na machungu uchaguzi mkuu.
Kwa mnaotazama ITV 95% ya wanaotoa maoni juu ya Orodha ya Mafisadi papa wanamuunga mkono Mzee Mengi kwa kauli yake. Nataka nikuthibitishie, siyo kama REDET bali kama mtafiti huru wa masuala ya kisiasa na kiuchumi, hizi takwimu ni sahihi na hazina hata chembe ya walakini. Huzuni yangu ilinipelekea kutembelea vijiwe vya kahawa mbalimbali Dar (Buguruni Sokoni, Kariakoo, Gerezani, Gongo la Mboto, Tabata, Temeke na Mbagala) na hapa Bukoba (Kashai, Hamugembe, Rwamishenye, Sokoni, Uswahilini na Kastamu) hasikudanganye mtu, watanganyika hawafanywi tena wadanganyika. Wanaelewa wabunge-maslahi wanaotaka walipwe12M, wanafahamu mafisadi papa, wanajua hata ushemeji wa rais wao kwa Rostam! Hutawaambia nini wakuelewe kwa hoja za kizandiki kama za kina Jackkson Manyenyere? Kuthibitisha ninachokieleza juu ya uelewa wa wananchi na msimamo wao ni rahisi sana; Mwombe Mama Sophia, Mkuchika au mtetezi yoyote wa mafisadi akatolee kauli za kuwabeza wanaopingana na ufisadi na mafisadi papa, kwenye majukwaa ya wazi ya wananchi na si kwenye semina za ndani apate maajibu.
Kwa wanaoona alama ukutani na kusoma nyakati vizuri, wanajua kiu ya wananchi kwa sasa ni kupingana na ufisadi na mafisadi papa. Kasi inazidi kupamba moto kama moto wa nyikani. Waliolifahamu hili, hotuba za mei mosi hazikuwapa shida kuzianda. Toka Mbeya, nenda Iringa, Morogoro, Dar mpaka Musoma Risala zote za Vyama vya wafanyakazi ziliunga mkono vita dhidi ya ufisadi na kuhoji juu ya watendaji wakuu serikali wanaowapinga Wazalendo wanaowataja wazi mafisadi. Hotuba nazo kama ile ya Lukuvi-Dar ilijikita kuhamasisha wafanyaazi kujitokeza wazi kupinga ufisadi na mafisadi papa. Hili ni kundi moja tu ila lenye nguvu ambalo limepata jukwaa la mei mosi na kulitumia kufikisha ujumbe wake juu ya vita ya ufisadi. Kumbuka yako makundi mengine mengi tu ndani ya jamii ambayo hayajapata jukwaa rasmi kueleza mtazamo na maoni yake juu ya vita hii. Hawa jukwaa lao ni uchaguzi mkuu 2010 au wakibahatika ni pale wanapotembelewa na kiongozi wa juu na kumwona jukwaani.
Nirejee kwenye mada, awali nimesema CCM na Serikalai yetu wamekosea kwa mara nyingine tena.Mara ya kwanza ilikuwa ni pale Mpiganaji Mzalendo Dr. Slaa alipotoa Orodha ya Mafisadi pale Mwembeyanga. CCM ikambeza, akaitwa mwongo, wakaandaa mkakati wa kuzunguka nchi nzima kuelezea uzuri wa bajeti. Yaliyojiri sote ni mashahidi. Wananchi walibuni na kutekeleza mpango mahsusi wa kuwazomea wabunge, wakuu wa wilaya, mawaziri, W/Mkuu lowassa na kumpopoa Rais kama nja yao pekee na mbadala ya kupingana na hali ya ufisadi huku wakiendeleza utulivu kungoja hukumu kwenye boksi la kura 2010. safari hii Mzee Mengi naye ana Orodha ya Mafisadi kumi ila kataja Mafisadi Papa Watano. Kama kawaida serikali tayari imembeza; Mengi kachemsha, Mengi mwehu, tutamshughulikia! Mapapa wamekwisha mpa notisi za kumtaka asalimu amri kwa kumwomba radhi na baadhi wamemfungulia kesi mahakamani na kudai fidia.
Binafsi, sioni jipya si kutoka upande wa watetezi wa ufisadi yaani serikali wala mafisadi papa wenyewe. Kama ni kubeza hata Orodha ya Dr. Slaa waliibeza, kama ni mahakamani na kutaka kuombwa msamaha mafisadi waliotajwa walitishia. La ajabu hadi hivi naandika sijasikia Dr. Slaa akiomba msamaha, kusomewa kesi au kulipa faini. Zaidi nimeshuhudi demokrasia ya upeo wa karne ndani ya Tanganyika wananchi wakiwazomea na kuwapopoa viongozi wao wa juu kabisa serikalini. Nimeshuhudia serikali ikidumu katika kashfa zaidi ya miaka mitatu kwa kashfa ambazo mwanzo wake uliitwa uongo. Nimewaona na kuwasikia Wabunge Dandia-Treni-Kwa-Mbele wakigombana kutwaa umaarufu kwa hoja za kupinga ufisadi ambazo mwazo wake waliupinga kufa na kupona. KUBWA, nimejifunza wepesi wa viongozi kusahau na kutojifunza kupitia matukio ya aina ileile yaliyotokea si muda mrefu uliopita. Mfano:
Richmond Dowans
Orodha ya Mafisadi Mafisadi Papa
Zabuni ya Umeme wa Dharura Zabuni ya Vitambulisho
Tafadhali ongeza matukio yaliyotokea siku zilizopita na kusababisha kashfa na yanaelekea kutokea au yametokea tena.
Mtabaini kwamba Omutwale nimekuwa Passive member hapa JF. Lakini katika siku hizi mbili uvumilivu wa kubaki msomaji na kugonga thanx umeshindikana. Najifunza kuandika.(Nisamehe nikiku-bore) baada ya kusikia kauli za-kina Mama Simba na Mkuchika wakimbeza Mzee Mzalendo, Bwana Reginard Mengi. Kauli hizi mbili zikifuatiwa na nyongeza ya mtazamo wa M/Kiti wa chama kinachoendelea kupoteza dira, Prof. Ibrahim Lipumba pamoja na tamko lililotolewa jana na vijana wa uvccm toka Tabora vilinifedhehesha na kuninyongonyesha saaana. Wapendwa wana neno stahili kwa hali iliyonipata linaitwa Roho kuugua
Roho yangu iliugua kutokana na mambo makuu mawili:
Moja, kuona serikali kupitia Mawaziri wake imeamua kubainisha wazi upande wake katika vita hii dhidi ya ufisadi na mafisadi papa. Kinyume na matarajio na fikra za walio wengi, sasa ni wazi serikali inapigana vita toka kona/upande wa ufisadi na mafisadi papa ikishambulia wenye nia njema na nchii hii (yetu sote) waliojitoa muanga hadharani kupingana na ufisadi na mafisadi papa.
Pili, Roho yangu iliugua kutokana na kuchanganyikiwa kwa wadanganyika na kuibuka kwa wananchi-maslahi waliojitokeza kuwatetea mapapa waliotajwa. Miongoni mwao ni waliojiita wazee wa yanga wakimtetea manji na wale vijana toka Tabora wakimtetea Rostam.
La pili liliniumiza zaidi maana serikali inaweza kuwa mbovu wananchi wenye umoja na uelewa wakairekebisha, lakini jamii/wananchi waliowabovu na wasio na umoja hawawezi kuirekebisha serikali mbovu. Hii ilinisukuma kutaka kujua uelewa wa wananchi na msimamo wa walio wengi juu ya masuala ya ufisadi na mafisadi papa. Napenda niwashirikishe wana JF, kwa mara nyingine tena, algebra za CCM na Serikali yetu kwa ujumla zimeenda alijojo. Kauli zilizotolewa na Mawaziri ziliwakadiria wadanganyika kuwa bado wako 1947! lakini nilchobani watanganyika wako oktoba 2010, mwaka mmoja mbele ya CCM na Serikali yetu wakingoja kwa hasira na machungu uchaguzi mkuu.
Kwa mnaotazama ITV 95% ya wanaotoa maoni juu ya Orodha ya Mafisadi papa wanamuunga mkono Mzee Mengi kwa kauli yake. Nataka nikuthibitishie, siyo kama REDET bali kama mtafiti huru wa masuala ya kisiasa na kiuchumi, hizi takwimu ni sahihi na hazina hata chembe ya walakini. Huzuni yangu ilinipelekea kutembelea vijiwe vya kahawa mbalimbali Dar (Buguruni Sokoni, Kariakoo, Gerezani, Gongo la Mboto, Tabata, Temeke na Mbagala) na hapa Bukoba (Kashai, Hamugembe, Rwamishenye, Sokoni, Uswahilini na Kastamu) hasikudanganye mtu, watanganyika hawafanywi tena wadanganyika. Wanaelewa wabunge-maslahi wanaotaka walipwe12M, wanafahamu mafisadi papa, wanajua hata ushemeji wa rais wao kwa Rostam! Hutawaambia nini wakuelewe kwa hoja za kizandiki kama za kina Jackkson Manyenyere? Kuthibitisha ninachokieleza juu ya uelewa wa wananchi na msimamo wao ni rahisi sana; Mwombe Mama Sophia, Mkuchika au mtetezi yoyote wa mafisadi akatolee kauli za kuwabeza wanaopingana na ufisadi na mafisadi papa, kwenye majukwaa ya wazi ya wananchi na si kwenye semina za ndani apate maajibu.
Kwa wanaoona alama ukutani na kusoma nyakati vizuri, wanajua kiu ya wananchi kwa sasa ni kupingana na ufisadi na mafisadi papa. Kasi inazidi kupamba moto kama moto wa nyikani. Waliolifahamu hili, hotuba za mei mosi hazikuwapa shida kuzianda. Toka Mbeya, nenda Iringa, Morogoro, Dar mpaka Musoma Risala zote za Vyama vya wafanyakazi ziliunga mkono vita dhidi ya ufisadi na kuhoji juu ya watendaji wakuu serikali wanaowapinga Wazalendo wanaowataja wazi mafisadi. Hotuba nazo kama ile ya Lukuvi-Dar ilijikita kuhamasisha wafanyaazi kujitokeza wazi kupinga ufisadi na mafisadi papa. Hili ni kundi moja tu ila lenye nguvu ambalo limepata jukwaa la mei mosi na kulitumia kufikisha ujumbe wake juu ya vita ya ufisadi. Kumbuka yako makundi mengine mengi tu ndani ya jamii ambayo hayajapata jukwaa rasmi kueleza mtazamo na maoni yake juu ya vita hii. Hawa jukwaa lao ni uchaguzi mkuu 2010 au wakibahatika ni pale wanapotembelewa na kiongozi wa juu na kumwona jukwaani.
Nirejee kwenye mada, awali nimesema CCM na Serikalai yetu wamekosea kwa mara nyingine tena.Mara ya kwanza ilikuwa ni pale Mpiganaji Mzalendo Dr. Slaa alipotoa Orodha ya Mafisadi pale Mwembeyanga. CCM ikambeza, akaitwa mwongo, wakaandaa mkakati wa kuzunguka nchi nzima kuelezea uzuri wa bajeti. Yaliyojiri sote ni mashahidi. Wananchi walibuni na kutekeleza mpango mahsusi wa kuwazomea wabunge, wakuu wa wilaya, mawaziri, W/Mkuu lowassa na kumpopoa Rais kama nja yao pekee na mbadala ya kupingana na hali ya ufisadi huku wakiendeleza utulivu kungoja hukumu kwenye boksi la kura 2010. safari hii Mzee Mengi naye ana Orodha ya Mafisadi kumi ila kataja Mafisadi Papa Watano. Kama kawaida serikali tayari imembeza; Mengi kachemsha, Mengi mwehu, tutamshughulikia! Mapapa wamekwisha mpa notisi za kumtaka asalimu amri kwa kumwomba radhi na baadhi wamemfungulia kesi mahakamani na kudai fidia.
Binafsi, sioni jipya si kutoka upande wa watetezi wa ufisadi yaani serikali wala mafisadi papa wenyewe. Kama ni kubeza hata Orodha ya Dr. Slaa waliibeza, kama ni mahakamani na kutaka kuombwa msamaha mafisadi waliotajwa walitishia. La ajabu hadi hivi naandika sijasikia Dr. Slaa akiomba msamaha, kusomewa kesi au kulipa faini. Zaidi nimeshuhudi demokrasia ya upeo wa karne ndani ya Tanganyika wananchi wakiwazomea na kuwapopoa viongozi wao wa juu kabisa serikalini. Nimeshuhudia serikali ikidumu katika kashfa zaidi ya miaka mitatu kwa kashfa ambazo mwanzo wake uliitwa uongo. Nimewaona na kuwasikia Wabunge Dandia-Treni-Kwa-Mbele wakigombana kutwaa umaarufu kwa hoja za kupinga ufisadi ambazo mwazo wake waliupinga kufa na kupona. KUBWA, nimejifunza wepesi wa viongozi kusahau na kutojifunza kupitia matukio ya aina ileile yaliyotokea si muda mrefu uliopita. Mfano:
Richmond Dowans
Orodha ya Mafisadi Mafisadi Papa
Zabuni ya Umeme wa Dharura Zabuni ya Vitambulisho
Tafadhali ongeza matukio yaliyotokea siku zilizopita na kusababisha kashfa na yanaelekea kutokea au yametokea tena.