Mwanamageuko
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 8,596
- 5,584
Nilipata kuandika hapa nini kitatokea chadema na vyama vingine vya upinzani mwaka 2010. Naandika tena hii leo hii sio ramli wala unajimu ni kuzisoma alama za nyakati zinasemaje?
Ziko njia mbili pekee nizionazo, yako mambo matatu yaweza kutokea:
Njia:
1. Mabadiliko ya kweli ikiwa ukawa itaingia madarakani, japo kutakuwepo changamoto za awali (kipindi cha mpito) hakitazidi miezi sita kwani mh. Lowassa anawafahamu watendaji wazuri waliopo katika serikali ya sasa ambao akiunganisha nguvu atajenga serikali imara yenye uwezo wa kutekeleza ilani ya ukawa.
Wananchi wengi watakuwa na matumaini na hamasa kubwa ya kurudisha uzalendo na ari ya kutumikia nchi. Idadi ya watanzania wenye mitaji na ujuzi watavutiwa kurudi nyumbani kuwekeza wakiwa na amani kuliko urasimu waliokutana nao awali walipojaribu kufanya hivyo. Sitozungumzia uwekezaji uliopo kwa sasa. Na mambo yakienda kombo wataweza kujieleza mapema na wananchi wataelewa, punde mambo yatakaa sawa na nchi itapata maendeleo ya haraka kuliko wakati wowote ndani ya miaka minne hadi mitano ya kwanza.
2. Ni serikali ya Magufuli!!! Kama inavyolazimishwa kuitwa, hii ni serikali ya CCM ambayo wananchi wameshakata nayo tamaa. Inawezekana mh. Magufuli akaanza kwa kasi kama alivyoanza mzee ruksa au zaidi, kasi yake itazuiwa kwa nguvu na mashinikizo makubwa toka kwa wanasiasa wakongwe kiasi kwamba atakata tamaa na kukosa uvumilivu, hapa mvurugano mkubwa wa wenye chama na wanachama wa CCM utajitokeza wazi na kukipasua rasmi lakini pia bila kuiacha salama serikali yao.
Upande wa pili wananchi walioweka matumaini kwa serikali ya magufuli watakata tamaa na kuanza kupinga waziwazi huku wakibeba mabango ya kudai ahadi alizotoa. Mambo haya yatamchanganya na sitoshangaa akitumia mkono wa chuma kutuliza hali ya mambo kama si kutawala. Vilio na kulaani vitaenea toka mashariki mpaka magharibi, kaskazini na kusini. Hali ya mambo itazorota na wafanyabiashara watakata tamaa.
Kati ya hizo njia mbili watanzania wana hiyari ya kuchagua moja inayowafaa.
Matokeo matatu.
1. Ikiwa uchaguzi utafanyika kwa haki, mshindi wa ngazi yoyoye iwayo akapata haki yake na matokeo yakawa halali amani itakuwa maradufu ya awali na dalili za maendeleo na ukuaji demokrasia itakuwa dhahiri.
2. Ikiwa wizi au ujanja wowote uwao kwa mgombea yeyote awaye ili kushinda uchaguzi basi mengi yatajitokeza ikiwamo kutokuwajibika na hujuma zinginezo hali itakayopelekea mshindi husika kudharaulika na kutoaminika tena.
3. Iwapo mshindi yeyote au chama chochote watakapojitambua kuwa hii nchi ni ya watanzania na kila mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi ama utawala na wakashirikiana basi pia litakuwa jambo la kheri na tanzania itang'ara na kupaa kutoka tulipo kwenda kwenye mafanikio,kinyume na hapo... Ni giza giza tupu.
Kwa ufupi ni hayo ndugu zangu. Tunaitazama tanzania, wapi tulikuwa, wapi tupo, wapi tunapelekwa. Wako watu wamejenga chuki kwa mtindo wa kutengeneza tatizo ili watafute ufumbuzi baada ya uchaguzi je wanao uhakika gani na hayo masuluhisho hao kufaulu?
Ninasubiri kuona, kazi yangu ni kukumbusha na kuonya basi.
Mungu ibariki Tanzania.
Ziko njia mbili pekee nizionazo, yako mambo matatu yaweza kutokea:
Njia:
1. Mabadiliko ya kweli ikiwa ukawa itaingia madarakani, japo kutakuwepo changamoto za awali (kipindi cha mpito) hakitazidi miezi sita kwani mh. Lowassa anawafahamu watendaji wazuri waliopo katika serikali ya sasa ambao akiunganisha nguvu atajenga serikali imara yenye uwezo wa kutekeleza ilani ya ukawa.
Wananchi wengi watakuwa na matumaini na hamasa kubwa ya kurudisha uzalendo na ari ya kutumikia nchi. Idadi ya watanzania wenye mitaji na ujuzi watavutiwa kurudi nyumbani kuwekeza wakiwa na amani kuliko urasimu waliokutana nao awali walipojaribu kufanya hivyo. Sitozungumzia uwekezaji uliopo kwa sasa. Na mambo yakienda kombo wataweza kujieleza mapema na wananchi wataelewa, punde mambo yatakaa sawa na nchi itapata maendeleo ya haraka kuliko wakati wowote ndani ya miaka minne hadi mitano ya kwanza.
2. Ni serikali ya Magufuli!!! Kama inavyolazimishwa kuitwa, hii ni serikali ya CCM ambayo wananchi wameshakata nayo tamaa. Inawezekana mh. Magufuli akaanza kwa kasi kama alivyoanza mzee ruksa au zaidi, kasi yake itazuiwa kwa nguvu na mashinikizo makubwa toka kwa wanasiasa wakongwe kiasi kwamba atakata tamaa na kukosa uvumilivu, hapa mvurugano mkubwa wa wenye chama na wanachama wa CCM utajitokeza wazi na kukipasua rasmi lakini pia bila kuiacha salama serikali yao.
Upande wa pili wananchi walioweka matumaini kwa serikali ya magufuli watakata tamaa na kuanza kupinga waziwazi huku wakibeba mabango ya kudai ahadi alizotoa. Mambo haya yatamchanganya na sitoshangaa akitumia mkono wa chuma kutuliza hali ya mambo kama si kutawala. Vilio na kulaani vitaenea toka mashariki mpaka magharibi, kaskazini na kusini. Hali ya mambo itazorota na wafanyabiashara watakata tamaa.
Kati ya hizo njia mbili watanzania wana hiyari ya kuchagua moja inayowafaa.
Matokeo matatu.
1. Ikiwa uchaguzi utafanyika kwa haki, mshindi wa ngazi yoyoye iwayo akapata haki yake na matokeo yakawa halali amani itakuwa maradufu ya awali na dalili za maendeleo na ukuaji demokrasia itakuwa dhahiri.
2. Ikiwa wizi au ujanja wowote uwao kwa mgombea yeyote awaye ili kushinda uchaguzi basi mengi yatajitokeza ikiwamo kutokuwajibika na hujuma zinginezo hali itakayopelekea mshindi husika kudharaulika na kutoaminika tena.
3. Iwapo mshindi yeyote au chama chochote watakapojitambua kuwa hii nchi ni ya watanzania na kila mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi ama utawala na wakashirikiana basi pia litakuwa jambo la kheri na tanzania itang'ara na kupaa kutoka tulipo kwenda kwenye mafanikio,kinyume na hapo... Ni giza giza tupu.
Kwa ufupi ni hayo ndugu zangu. Tunaitazama tanzania, wapi tulikuwa, wapi tupo, wapi tunapelekwa. Wako watu wamejenga chuki kwa mtindo wa kutengeneza tatizo ili watafute ufumbuzi baada ya uchaguzi je wanao uhakika gani na hayo masuluhisho hao kufaulu?
Ninasubiri kuona, kazi yangu ni kukumbusha na kuonya basi.
Mungu ibariki Tanzania.
