Akiwa na rafiki zake lazima tugombane

Akiwa na rafiki zake lazima tugombane

kuna uwezekano hata mkioana mtakuwa mnagombana hivyohivyo maana inaonekana mchumba wako hajui kutofautisha urafik na mahusiano. Hajui kuwa mahusiano na mume/mchumba ni zaidi ya hayo ya marafiki. Usishangae akiwa na hao unakuwa huna thaman ukipiga simu anaona kero na wanakaa kukujadili na ha6arafiki
 
kilambalambila... Usishangae akiwa na hao unakuwa huna thaman ukipiga simu anaona kero na wanakaa kukujadili na ha6arafiki...unachosema hata mm huwa nahisi hivo..sasa nifanyeje
 
Last edited by a moderator:
Mmmhh huenda rafiki zake walimponda 'mmhh huyo shem sura mbaya ka fenesi kifupii loh'
akaona awe anakudis akiwa nao
hapana chezeiya girls!!!!
upo?
 
Kwenye hili nahitaji msaada wa mawazo ndugu zangu..

Niko kwenye mahusiano na dada mmoja,tunaishi Iringa-Kihesa. Tupo pamoja muda mrefu kidogo, tunapendana, kwa ujumla maisha yetu ya mapenzi ni mazuri hadi kufikiria kufunga ndoa mwakan.

Lakin tatizo lake ni mashoga zake ambao wengine wanaishi dar, wengine mwanza.. hawa rafiki zake huwa wanakuja iringa kila baada ya miezi miwili..hawa rafiki zake wakija iringa wanafikia kwao(kwa mpenzi wangu ) maana wanatambulika na wazazi wake..hawa rafiki zake wanapokuja ni lazima tugombane mm na mpenzi wangu maana anapunguza kabisa attention kwangu. Mara utasikia wamekwenda Ruaha national park bila kuniambia mm..na sio kawaida yake kwenda...sehemu bila kuniambia...mara nikimpigia simu ananijibu vibaya kwa dharau au sometimes hapokei simu kabisa..akipokea anasema amechoka anataka kulala..ili mradi tu tugombane..she s real soundin weird.

Rafiki zake wanaweza kukaa wiki mbili iringa..na pindi wanapoondoka mambo yanakuwa kawaida..tunaishi vizuri..tunaheshimiana..tunapendana...

Nahitaji ushauri nifanye nn

Nimefikiria kipuuzi tu, nikapata sababu lukuki kama ifuatavyo

  • Hajui kutofautisha nafasi ya mpenzi na marafiki wa kawaida au
  • Inawezekana hajawaambia hao rafiki zake kuwa ana mchumba/mpenzi ambaye ni wewe na hayuko tayari kufanya hivyo sasa au
  • Ana mwingine ambaye anatambulika na hao rafiki zake na wewe upo kama mtu wa kuzugia tu
  • Au yuko na wewe kwa kampani tu, hafikiri kama utakuwa mume huko baadaye
  • Au hajiamini anaona aibu kukutambulisha au kuwa karibu na wewe akiwa na rafiki zake
Nakushauri kaa naye chini na mueleze wazi kusikitishwa na hizo tabia na umtake ajirekebishe kama atakuwa mkorofi basi mojawapo la hayo niyoyataja hapo juu yanaweza kuwa ni kweli!

Kila la kheri,

HP
 
Kifupi wewe ni chaguo la pili chaguo lake la kwanza ni marafiki
 
Wewe unamchukulia serious yeye anakuchukulia kiaina tu kwa wepesi na rafiki zake hawakukubali na yeye akili kashikiwa!!!!

Yaani unatumika hapo kumuondoa upweke tu akiwa hana watu wanafanana!!!!

Utaachwa pindi tu atakapopata mtu anayeendana naye sawia!!
 
Wakiondoka na wewe mchunie ujidai hauna habari nae, ukiona hana time ya kukutafuta wala hali hiyo haimshtui basi tingishia mazima hakuna mapenzi hapo.
 
Hao marafiki wanapokuja ameshawahi kukutambulisha kwao au umeshwahi kuonana nao? Pili unajua sisi wadada bwana tukionyeshwa upendo hasa ule wa dhati huwa tunajisahau sana na mara nyingi huwa tunakaa sawa pale mambo yanapoanza kwenda kombo, sasa basi kwa kuwa umesema una mpango wa kumuoa hakikisha hilo jambo unaliondoa kabisa ili lisije leta balaa zaidi mtakapokuwa mmeoana, mueleze na umuonyeshe msimamo kwamba hupendezwi na tabia zake rafiki zake wanapokuja na umwambie kwamba abadilike la sivyo yatakushinda, ukiona habadilik basi rafiki zake wakija na wewe kaa kimya usimtafute kwa aina yoyote unless yeye ndo akutafute mpaka hao rafiki zake watakapoondoka, na akilalamika mwambie kwamba ulishamuonya abadilike lakini unaona habadiliki kwahyo na wewe umeamua kufanya maamuzi yako, ukiona na hapo bado habdiliki basi sikushauri kumuoa manake ndoa yenu itaharibiwa na hao marafiki zake na utajuta kumoa
 
Nimefikiria kipuuzi tu, nikapata sababu lukuki kama ifuatavyo

  • Hajui kutofautisha nafasi ya mpenzi na marafiki wa kawaida au
  • Inawezekana hajawaambia hao rafiki zake kuwa ana mchumba/mpenzi ambaye ni wewe na hayuko tayari kufanya hivyo sasa au
  • Ana mwingine ambaye anatambulika na hao rafiki zake na wewe upo kama mtu wa kuzugia tu
  • Au yuko na wewe kwa kampani tu, hafikiri kama utakuwa mume huko baadaye
  • Au hajiamini anaona aibu kukutambulisha au kuwa karibu na wewe akiwa na rafiki zake
Nakushauri kaa naye chini na mueleze wazi kusikitishwa na hizo tabia na umtake ajirekebishe kama atakuwa mkorofi basi mojawapo la hayo niyoyataja hapo juu yanaweza kuwa ni kweli!

Kila la kheri,

HP
binamu upuuzi uliofikiria ni sahihi kabisa maana hata jamaa huyu jamaa yaweza hajajitambua.....
 
hapana chezea wasichana kuna siri ndani yake

henda ana mpenzi mwingine na hao mashosti wake wanamjua kwa hiyo wewe htambulikani ndo mana anakupotezea

au hawez kutofautisha urafiki na mahusiano....
 
E BWANA WEWE,HIVI KILE KILABU CHA IDUNDA HAPO KIHESA BADO KIPO? NA KWA SEMTEMA BADO KUNA UWAMBULE?:A S wink::A S wink::A S wink:
 
hapana chezea wasichana kuna siri ndani yake

henda ana mpenzi mwingine na hao mashosti wake wanamjua kwa hiyo wewe htambulikani ndo mana anakupotezea

au hawez kutofautisha urafiki na mahusiano....

kuna ukweli hapa
 
Mmmhh huenda rafiki zake walimponda 'mmhh huyo shem sura mbaya ka fenesi kifupii loh'
akaona awe anakudis akiwa nao
hapana chezeiya girls!!!!
upo?

Lol... umenikumbusha shosti fulani alikua anamuonea aibu bf wake kwetu. Anamponda na sie tunakandamizia.
Sahivi ndie mumewe halali.
Yalitushuka
 
hapana chezea wasichana kuna siri ndani yake

henda ana mpenzi mwingine na hao mashosti wake wanamjua kwa hiyo wewe htambulikani ndo mana anakupotezea

au hawez kutofautisha urafiki na mahusiano....

Na huenda hana hata huyo mwingine.
Hajiamini tu na usichana unamsumbua
 
Nimefikiria kipuuzi tu, nikapata sababu lukuki kama ifuatavyo

  • Hajui kutofautisha nafasi ya mpenzi na marafiki wa kawaida au
  • Inawezekana hajawaambia hao rafiki zake kuwa ana mchumba/mpenzi ambaye ni wewe na hayuko tayari kufanya hivyo sasa au
  • Ana mwingine ambaye anatambulika na hao rafiki zake na wewe upo kama mtu wa kuzugia tu
  • Au yuko na wewe kwa kampani tu, hafikiri kama utakuwa mume huko baadaye
  • Au hajiamini anaona aibu kukutambulisha au kuwa karibu na wewe akiwa na rafiki zake
Nakushauri kaa naye chini na mueleze wazi kusikitishwa na hizo tabia na umtake ajirekebishe kama atakuwa mkorofi basi mojawapo la hayo niyoyataja hapo juu yanaweza kuwa ni kweli!

Kila la kheri,

HP

Maneno yako yana busara na ukweli ndani yake mkuu

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom