Mkunde Original
JF-Expert Member
- Jul 20, 2013
- 807
- 647
Habari zenu wandugu,
Mawazo na michango yenu inahitajika kunusuru hii familia.
Ni familia ya mume mke na watoto 5, watoto 3 wako sekondari shule za bweni na wawili ndo wako shule ya msingi wanakaa nyumbani na wazazi wao.
Hii familia kwa miaka 3 mfululizo wamekuwa kwenye changamoto mbalimbali kiasi kwamba wote baba na mama kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitamani kuachana ila kigezo cha watoto ndo huwa kinakuwa zuio.
Changamoto imeongezeka baada ya utawala mpya kuingia madarakani mume au baba mwenye nyumba alitumbuliwa na mheshimiwa na hadi sasa yuko benchi tuu. Tangu huyo baba atumbuliwe amekuwa kero kwenye familia yake. Mwezi mmoja wa kwanza baada ya kutumbuliwa alikuwa anashinda nyumbani asubuhi hadi asubuhi nyingine, yaani alikuwa baba wa nyumbani na akajikuta anakuwa karibu na housegirl matokeo yake kuanza mahusiano na wadada wa kazi. Aibu hii mkewe aliigundua maana wadada walionesha mabafiliko kuna walioonesha jeuri na kiburi na kuna walioaga kuacha kazi gafla maana si waschana wote wanakubali kuwa na mahusiano na baba mwenye nyumba. Hivyo hilo limefanya mke kuwa na kero ya kubadili waschana wa kazi kila leo kama mjuavyo si rahisi kupata waschana wa kazi waweza kaa miezi 3 hadi 4 ukiwa unatafuta bila kupata.
Mke akiongea hii kero na mumewe mume akaona abadili muelekeo na kuanzia hapo akaanza asubuhi mke akijiandaa kwenda kazini na watoto shule yule baba mwenye nyumba anajiandaa nae anatoka. Anakoenda haijulikani basi ya miezi kadhaa mke akagundua kumbe huwa anaenda baa muda wa asubuhi atakula na kunywa maji hadi mchana akihama baa moja kwenda ingine na pale pombe zinaporuhusiwa kuanza kuuzwa basi huzifakamia utasema kuambiwa zinaongeza nguvu za kiume. Anarudi nyumbani akiwa njwii hajitambui anarudishwa na bodaboda hana hata kumi....
Amekuwa akitumia akiba yake kufanya huo ulevi na sasa amekuwa mlevi wa kupindukia. Mke ameshamshauri mara kadhaa aache kufanya hivyo maana hakubadilishi au kumpunguzia msongo wa mawazo alionao badala yake amekuwa mkali kwa mke na watoto. Mke anaona uvumilivu unamshinda maana kila siku afadhali ya jana. Mbali ya hapo bwana mume amekuwa akishusha kipondo kila arudipo amelewa na hapo kuna siku anarudi ananukia marashi ya kike siku ingine shati zina alama za rangi ya mdomo na foundation.... mke anafua tuu.... Kweli jamani na hii avumilie. .... magonjwa je?
Nyie mwaonaje maana hii familia naifahamu na huyu mama huwa tunaongea sana. Sijamshauri cha kufanya nimekuwa nikimpa pole tuu ila ninakoelekea nahisi ntamwambia aachanena mumewe maana huko si kuvumiliana kwa shida na raha khaa.
Kusema ukweli hata mie ndoa yangu ina misukosuko ila si kama ya huyu mama. Na yangu ingekuwa kama ya huyu wallah ningeachika tangu juzi.
Nyie mnashaurije?
Mawazo na michango yenu inahitajika kunusuru hii familia.
Ni familia ya mume mke na watoto 5, watoto 3 wako sekondari shule za bweni na wawili ndo wako shule ya msingi wanakaa nyumbani na wazazi wao.
Hii familia kwa miaka 3 mfululizo wamekuwa kwenye changamoto mbalimbali kiasi kwamba wote baba na mama kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitamani kuachana ila kigezo cha watoto ndo huwa kinakuwa zuio.
Changamoto imeongezeka baada ya utawala mpya kuingia madarakani mume au baba mwenye nyumba alitumbuliwa na mheshimiwa na hadi sasa yuko benchi tuu. Tangu huyo baba atumbuliwe amekuwa kero kwenye familia yake. Mwezi mmoja wa kwanza baada ya kutumbuliwa alikuwa anashinda nyumbani asubuhi hadi asubuhi nyingine, yaani alikuwa baba wa nyumbani na akajikuta anakuwa karibu na housegirl matokeo yake kuanza mahusiano na wadada wa kazi. Aibu hii mkewe aliigundua maana wadada walionesha mabafiliko kuna walioonesha jeuri na kiburi na kuna walioaga kuacha kazi gafla maana si waschana wote wanakubali kuwa na mahusiano na baba mwenye nyumba. Hivyo hilo limefanya mke kuwa na kero ya kubadili waschana wa kazi kila leo kama mjuavyo si rahisi kupata waschana wa kazi waweza kaa miezi 3 hadi 4 ukiwa unatafuta bila kupata.
Mke akiongea hii kero na mumewe mume akaona abadili muelekeo na kuanzia hapo akaanza asubuhi mke akijiandaa kwenda kazini na watoto shule yule baba mwenye nyumba anajiandaa nae anatoka. Anakoenda haijulikani basi ya miezi kadhaa mke akagundua kumbe huwa anaenda baa muda wa asubuhi atakula na kunywa maji hadi mchana akihama baa moja kwenda ingine na pale pombe zinaporuhusiwa kuanza kuuzwa basi huzifakamia utasema kuambiwa zinaongeza nguvu za kiume. Anarudi nyumbani akiwa njwii hajitambui anarudishwa na bodaboda hana hata kumi....
Amekuwa akitumia akiba yake kufanya huo ulevi na sasa amekuwa mlevi wa kupindukia. Mke ameshamshauri mara kadhaa aache kufanya hivyo maana hakubadilishi au kumpunguzia msongo wa mawazo alionao badala yake amekuwa mkali kwa mke na watoto. Mke anaona uvumilivu unamshinda maana kila siku afadhali ya jana. Mbali ya hapo bwana mume amekuwa akishusha kipondo kila arudipo amelewa na hapo kuna siku anarudi ananukia marashi ya kike siku ingine shati zina alama za rangi ya mdomo na foundation.... mke anafua tuu.... Kweli jamani na hii avumilie. .... magonjwa je?
Nyie mwaonaje maana hii familia naifahamu na huyu mama huwa tunaongea sana. Sijamshauri cha kufanya nimekuwa nikimpa pole tuu ila ninakoelekea nahisi ntamwambia aachanena mumewe maana huko si kuvumiliana kwa shida na raha khaa.
Kusema ukweli hata mie ndoa yangu ina misukosuko ila si kama ya huyu mama. Na yangu ingekuwa kama ya huyu wallah ningeachika tangu juzi.
Nyie mnashaurije?