Akina dada ndoa sio rahisi kama mnavofikiria

Akina dada ndoa sio rahisi kama mnavofikiria

Shida na raha

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
3,773
Reaction score
3,474
Najisika kuwa na nguvu ya kuwapa dada zangu ukweli ili uweze kuwavusha inawezekana ...umeomba sana lakini nguvu ya kufanya maamuzi haipo ndani yako pasipo... Kuwa na nguvu ya kuamua..

Umepata Bwana, Umempenda Kweli kweli na Umemlalamikia Sana Eti Kwanini Hakupeleki Kwa Wazazi Wake Kukutambulisha, Jamaa Akagoma Sana mwishowe akaona isiwe Kesi Akakupeleka

Wewe badala hata utake hiyo advantage umefika tu Siku ya Kwanza Umeshinda Unachati, Siku ya Pili Umeshinda Unachati Tena ndio unajisifia kwenye groups upo ukweni Kumbe Wao Wanakutazama Tu na kukupimia Wala Hawakwambii Kitu.

Siku ya Tatu Wanakwambia Leo Ni Zamu Yako Kupika, Unaingia Jikoni unaona Kila Kitu Kigeni
Vya Huku Unaweka Kule, Vya kule Unaweka Huku (Yaani Hujui Kupika Chochote)

Sufuria Unashika Kama Umeshika Power Bank, Unapika Na Lipstick, Mdomo Mwekunduuu Utafikiri Mtoto wa Jini Katoka Kufundishwa Kunyonya Damu tena huku Umevaa Saa, Umevaa Culture Zimejaa Nusu Ya Mkono, Umevaa Mini Skirt Kama Wafanyakazi Wa shirika la Emirates

Msosi wa Wakwe Huwezi Kupika.... , Ukiambiwa Hufai Kuolewa Unavuta Mdomo Utafikiri Umenyimwa USB Cable Ubust Smartphone Yako
Unaanza Kulalamika Wakwe Hawakupendi, Unalalamika Weee, Unashindwa Kuelewa Kuwa Wewe Ndio Tatizo.....unaanza kuweka dp whatsap za kuwananga mawifi...

Usitake Kuolewa Ukidhani Mumeo Atakula Chips na Wewe Utakuwa Utakula Pizza Kila Siku, Jifunze Hata Kuchemsha Chai Basi
Jifunze hata kupasha mihogo
Au Unadhani Google Wataleta App ambayo Unaweka USB Kwenye Simu yako alafu unaielekezea kwenye sahani Inaproduce msosi.

JIPANGE DADA Usidhani Ndoa Ni Kama Kupiga selfie,.. uwe na usiku wenye maamuzi ukinuna pasuka kama chupa.
 
Sawa tumekusikia,tumekuelewa!
 
Hahahah nimependa hapo "mdomo mwekundu utafikiri mtoto wa jini anafundishwa kunyonya damu"

Hakika na waelewe
 
Duh aisee lakin mimi mke wangu mbitiyaza anajua kupika
 
Mambo ya Ngoswe, muachie Ngoswe mwenyewe.

Ama sivyounaweza kuambiwa unawanyanyapaa kwa mfumodume.
 
Hivi kuna wanawake wanaitwa

Bi..... Na sio bibi
Kama wapo ujue sio single mother(s)
 
Kwahiyo ukijua kupika ukweni ndo unapata sifa ya kuolewa?
 
Ndoa ingekuwa kupika pika kama unavyoelezea basi ingenua rahisi sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom