Akili iliyotumika kumsifu Kikwete ndio akili hiyo hiyo inayotumika tumuone Magufuli ni malaika

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,089
144,537
Watanzania wenzangu, akili na fikra zilizotumika kutetea utawala wa Raisi Kikwete kwa karibu kila jambo na kupinga mawazo ya upinzani ya kumkosoa Kikwete ndio hiyo hiyo inayotutaka leo hii tuamini Magufuli ni malaika asiefanya makosa na kumkosoa ni dhambi kubwa kama sio wivu.

Ni hawa hawa walitetea safari za nje ya nchi za wakati wa Kikwete lakini ni hawa hawa leo hii wanaungana na Magufuli kuziponda safari hizi!Watu wa ajabu sana hawa!

Ni hawa hawa walitetea na kusifu mabilioni ya shilingi kutumika kwenye sherehe za uhuru na ni watu wale wale leo hii wameungana na Magufuli kuzipinga sherehe hizi kwamba zinatumia fedha nyingi!Unafiki gani huu!

Ni watu hawa hawa walitetea bajeti kubwa ya chai na vitafunwa kutengwa kwa ajili ya Ikulu na maofisi mengine ya umma lakini ni watu hawa hawa leo hii wanaungana na kumsifia Magufuli kwa kubana matumizi!Binadamu hawa sijui unaweza kuwapata wapi zaidi ya nchi hii!

Ni akili hii hii iliyoshabikia kuwa elimu bure haiwzekani lakini ni akili hiyo hiyo leo hii inaamini elimu bure inawezekana!Zero kabisa!

Ni akili hii hii inayotuambia tunaweza kujitegemea bila misaada lakini ni akili hiyo hiyo inapigia chapuo misaada ya fedha kutoka kwa wachina! Very pathetic!

Yako mengi sana kuhusu hawa wenzetu ambao nadhani sample ya brain yao inahitajika kupelekwa maabara kwa uchunguzi kuoma kama wana afya ya kili inayokubalika.

Tuwaepuka hawa bendera fuata upepo.
 
Wee jamaa una wivu sana, watu wakisifu wewe unakosa nini?? Wewe ponda, alafu mbona wa kuponda wapo hata humu? Acha wengine waponde wengine wasifu, hatuwezi wote tukapanda basi moja!
Kubali matokeo.
 
ni ha
Watanzania wenzangu, akili na fikra zilizotumika kutetea utawala wa Raisi Kikwete kwa karibu kila jambo na kupinga mawazo ya upinzani ya kumkosoa Kikwete ndio hiyo hiyo inayotutaka leo hii tuamini Magufuli ni malaika asiefanya makosa na kumkosoa ni dhambi kubwa kama sio wivu.

Ni hawa hawa walitetea safari za nje ya nchi za wakati wa Kikwete lakini ni hawa hawa leo hii wanaungana na Magufuli kuziponda safari hizi!Watu wa ajabu sana hawa!

Ni hawa hawa walitetea na kusifu mabilioni ya shilingi kutumika kwenye sherehe za uhuru na ni watu wale wale leo hii wameungana na Magufuli kuzipinga sherehe hizi kwamba zinatumia fedha nyingi!Unafiki gani huu!

Ni watu hawa hawa walitetea bajeti kubwa ya chai na vitafunwa kutengwa kwa ajili ya Ikulu na maofisi mengine ya umma lakini ni watu hawa hawa leo hii wanaungana na kumsifia Magufuli kwa kubana matumizi!Binadamu hawa sijui unaweza kuwapata wapi zaidi ya nchi hii!

Ni akili hii hii iliyoshabikia kuwa elimu bure haiwzekani lakini ni akili hiyo hiyo leo hii inaamini elimu bure inawezekana!Zero kabisa!

Yako mengi sana kuhusu hawa wenzetu ambao nadhani sample ya brain yao inahitajika kupelekwa maabara kwa uchunguzi kuoma kama wana afya ya kili inayokubalika.

Tuwaepuka hawa bendera fuata upepo.
ni hawa hawa walioimba nchi nzima kuwa ndg. Lowassa ni fisadi mkubwa na ni hawahawa leo wanaimba kuwa Lowassa ni malaika...jamani wanafiki hawa na wababaishaji.
 
Unaenda rwanda na magari alafu ndege inatoka dar inakufuata na unafika uwanja wa ndege na kukuta serikali yote inakusubiri ili kukupokea
na bado ukawaambia watanzania unabana matumizi na wakakushangilia
nchi ni ya ajabu kweli'
 
Unaenda rwanda na magari alafu ndege inatoka dar inakufuata na unafika uwanja wa ndege na kukuta serikali yote inakusubiri ili kukupokea
na bado ukawaambia watanzania unabana matumizi na wakakushangilia
nchi ni ya ajabu kweli'
halafu bado anataka tuendelee kuamini kuwa yeye mbana matumizi?
 
Unaenda rwanda na magari alafu ndege inatoka dar inakufuata na unafika uwanja wa ndege na kukuta serikali yote inakusubiri ili kukupokea
na bado ukawaambia watanzania unabana matumizi na wakakushangilia
nchi ni ya ajabu kweli'

Huyo ndo rais wako, wee endelea kuponda na kuona mabaya kwako, ila kapunguza gharama, kama shule ilikupiga chenga, huwezi ona!
Emdelea kulefusha lips zako.
 
kusifu sio kuamini. unaweza ukasifia kitu kutokana na stuationj ilivyo hasa ktk kutafta rizki.
 
watasema na ninyi mlimsafisha lowasa na mkamsifu...kwa akili zenu mlituambia ni fisadi
 
Nakumbuka enzi hizo kikwete alikua akisafiri vilio vinakuja, mpaka ikaandaliwa thread maalum ya kuhesabu safari zake, akaja Magu, sasa wanasema huyu naye hasafiri sijui ataendesha vipi nchi bila kusafiri na kujionea wenzake wanavyofanya, tena akawa anatumia gari ili asfiri kupitia barabara wakawa wanasema ni hatari sana awe anatumia ndege, ni hao hao ambao kila jambo sio jema kwao, tumeshazoea akili zao ziko katika kupinga kila kitu hata hili nililoliandika hapa ambalo kwa asilimia kubwa ni ukweli, watakuja kulipinga.
 
Yaani hapo umenena ukweli mtupu. Watanznia wengi ni watu wa kufuata upepo.Wengi wanaojua ni wanafiki na wale wengine ambao upeo wao una mushkeli huwa hawajui hata wanachosifia.
 
Unaenda rwanda na magari alafu ndege inatoka dar inakufuata na unafika uwanja wa ndege na kukuta serikali yote inakusubiri ili kukupokea
na bado ukawaambia watanzania unabana matumizi na wakakushangilia
nchi ni ya ajabu kweli'
Kweli kabisa nchii hii ni ya ajabu sana unazunguka nchi nzima kuhubiri ufisadi wa lowassa afu baadae unakuja sema jamaa ni msafi kama sanda na bado watu wakakushangilia hakika nchii hii ya ajabu
 
Aacha ukorofi ukiambiwa ukiambiwa Leo umeweka chunvi nyingi halaf kesho haujaweka kabsa sasa wewe tukueleweje yaani usibiwe chunvi hakuna ?
Nakumbuka enzi hizo kikwete alikua akisafiri vilio vinakuja, mpaka ikaandaliwa thread maalum ya kuhesabu safari zake, akaja Magu, sasa wanasema huyu naye hasafiri sijui ataendesha vipi nchi bila kusafiri na kujionea wenzake wanavyofanya, tena akawa anatumia gari ili asfiri kupitia barabara wakawa wanasema ni hatari sana awe anatumia ndege, ni hao hao ambao kila jambo sio jema kwao, tumeshazoea akili zao ziko katika kupinga kila kitu hata hili nililoliandika hapa ambalo kwa asilimia kubwa ni ukweli, watakuja kulipinga.
 
Back
Top Bottom