chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 20,725
- 31,305
Hakika kuna jambo Gwajima alikuwa analipanga. Alikuwa anajikosha kujifanya nini sijui, kipindi cha uchaguzi dola inakuwa makini kwa asilimia 1000,000, kama unataka kufadhili magenge ya uhalifu utajulikana tu
==================
"Usiku huo huo majira ya saa tano, kanisa lilivamiwa na magari ya polisi (defenders) likazingirwa, waumini waliokuwa mkesha wa maombi walipigwa, kutolewa nje ya kanisa kwa nguvu bila maelezo na kuwakamata waumini 96, wakiwemo wanawake, wazee na vijana wasio na hatia yoyote zaidi ya kumuomba Mungu wao" - Askofu Mwanamapinduzi
"Makanisa yote 2,112 ya GCTC (Ufufuo na Uzima) yamefungwa nchi nzima. Waumini zaidi ya milioni 6 wamenyimwa haki ya kuabudu. Maaskofu, wachungaji, na wafanyakazi wa kanisa wamepoteza ajira, huduma na wito wa kazi ya Mungu. Akaunti zote za kifedha za kanisa zimefungiwa (frozen) bila kufuta utaratibu wa kisheria" - Askofu Mwanamapinduzi
"Uongozi wa kanisa ulichukua hatua za kisheria kwa kuwasilisha barua ya rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, lakini Waziri alikana barua ile kwa kusema haijasainiwa wala haijatoka kwa Msajili wa Vyama vya Kiraia. Hata hivyo, vyombo vya dola viliendelea kutekeleza amri hiyo ya kufunga makanisa yote ya Ufufuo na Uzima nchini na kuweka ulinzi mkali huku wakizuia mtu yeyote asiingie kwenye makanisa hayo isipokuwa Askari Polisi pake yake" - Askofu Mwanamapinduzi
==================
"Usiku huo huo majira ya saa tano, kanisa lilivamiwa na magari ya polisi (defenders) likazingirwa, waumini waliokuwa mkesha wa maombi walipigwa, kutolewa nje ya kanisa kwa nguvu bila maelezo na kuwakamata waumini 96, wakiwemo wanawake, wazee na vijana wasio na hatia yoyote zaidi ya kumuomba Mungu wao" - Askofu Mwanamapinduzi
"Makanisa yote 2,112 ya GCTC (Ufufuo na Uzima) yamefungwa nchi nzima. Waumini zaidi ya milioni 6 wamenyimwa haki ya kuabudu. Maaskofu, wachungaji, na wafanyakazi wa kanisa wamepoteza ajira, huduma na wito wa kazi ya Mungu. Akaunti zote za kifedha za kanisa zimefungiwa (frozen) bila kufuta utaratibu wa kisheria" - Askofu Mwanamapinduzi
"Uongozi wa kanisa ulichukua hatua za kisheria kwa kuwasilisha barua ya rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, lakini Waziri alikana barua ile kwa kusema haijasainiwa wala haijatoka kwa Msajili wa Vyama vya Kiraia. Hata hivyo, vyombo vya dola viliendelea kutekeleza amri hiyo ya kufunga makanisa yote ya Ufufuo na Uzima nchini na kuweka ulinzi mkali huku wakizuia mtu yeyote asiingie kwenye makanisa hayo isipokuwa Askari Polisi pake yake" - Askofu Mwanamapinduzi