Akaunti ya Twitter ya Rais wa Marekani Donald Trump yafungwa kwa muda

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
63cb241f6bfae80b6070f9c9400af44d.jpg
45e9d35cd051afab940b7d9f97a09946.jpg
Akaunti ya mtandao wa Twitter ya Rais wa Marekani Donald Trump ilifungwa kwa muda siku ya Alhamisi lakini, ikarudishwa baadaye, Kampuni hiyo imesema.

Twitter imesema kuwa akaunti hiyo kwa jina @realdonaldtrump iliondolewa na mfanyakazi mmoja na baadaye kueleza kuwa ilikuwa siku yake ya mwisho ya kazi.

Akaunti hiyo iliondolewa kwa muda wa dakika 11 na sasa kampuni ya Twitter inachunguza.

Bwana Trump ambaye ni mtumizi wa mtandao wa Twitter wa mara kwa mara akiwa na wafuasi milioni 41. 7 hajatoa tamko lolote kuhusu suala hilo.

Siku ya Alhamisi jioni wale waliotembelea akaunti ya Rais Trump waliona ujumbe uliosoma "pole ukurasa huu hauko kwa sasa"

Baada ya akaunti kurejeshwa ujumbe wa kwanza wa Bwana Trump ulikuwa kuhusu ule mpango wa Republican wa kupunguza kodi.

Hata hivyo POTUS ambayo ndio akaunti rasmi ya Rais Trump haukuathiriwa.

Twitter wamesema kuwa inachunguza tatizo hilo na kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa kisa kama hicho hakitokei tena.

Kampuni hiyo ilisema katika ujumbe wake kwamba wamebaini katika uchunguzi wao kwamba kisa hicho kilifanywa na mfanyakazi anayewahudumia wateja ambaye alifanya hivyo katika siku yake ya mwisho ya kazi.
 
Back
Top Bottom