barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,739
- 32,917
Imetokea ktk Wilaya ya Same,katika Jimbo la Same Magharibi katika kijiji cha Makanya,bibi kizee mwenye umri wa miaka 90(Jina linahifadhiwa) amebakwa na watu wasiojulikana mpaka kuvunjwa kiuno.
Akiongea kwa taabu na huku akiwa na maumivu makubwa,bibi huyo anasema alibakwa na mtu asiyemtambua usiku akiwa nyumbani kwake.Bibi huyo anaishi peke yake bila wajukuu wala watoto amepata majeraha na michubuko sehemu za siri huku akivunjika kiuno kwa adha ya kubakwa.
Ametibiwa ktk hospitali ya wilaya ya Same na baadae kupata msaada toka kwa Misheni ya kanisa katoliki Jimbo la Same,wakiongea kwa uchungu kina Mama wa eneo hilo wameomba polisi kufanya uchunguzi ili kumpata muhusika na kumfikisha ktk vyombo vya sheria kwani ni kitendo cha kinyama kwa bibi muhusika na wanawake kwa ujumla.
Bibi huyo anaendelea na matibabu ya kiuno na nyonga aliyoteguka baada ya kuingiliwa kwa nguvu.
Akiongea kwa taabu na huku akiwa na maumivu makubwa,bibi huyo anasema alibakwa na mtu asiyemtambua usiku akiwa nyumbani kwake.Bibi huyo anaishi peke yake bila wajukuu wala watoto amepata majeraha na michubuko sehemu za siri huku akivunjika kiuno kwa adha ya kubakwa.
Ametibiwa ktk hospitali ya wilaya ya Same na baadae kupata msaada toka kwa Misheni ya kanisa katoliki Jimbo la Same,wakiongea kwa uchungu kina Mama wa eneo hilo wameomba polisi kufanya uchunguzi ili kumpata muhusika na kumfikisha ktk vyombo vya sheria kwani ni kitendo cha kinyama kwa bibi muhusika na wanawake kwa ujumla.
Bibi huyo anaendelea na matibabu ya kiuno na nyonga aliyoteguka baada ya kuingiliwa kwa nguvu.