Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,552
Jamani mtalii wetu mtukuka yuko wapi? mbona kaachia ngazi kwenye daladala?
Imepita muda sijamsikia akishika mchuma au kuzamia mtemba kutembeza ungo kukusanya unga, kauzu na mchunga!
Je yanayowakabili Baniani ni machungu mno mpaka Kibuge ameacha kukaa nje ya Jamatini akisubiri kiporo cha Cheuro, Pera maziwa na Kuku wa Tanduri na Tika?
Mara ya mwisho nilisikia alikuwa aongoze msafara wa Wagogo (FMES kumradhi usinishikie marimba!) kwenda Jamatini kudai unga wa dengu, choroko na pilipili, kisa kule nyumbani kwa kina Baniani, wameanza kulishana dengu na maziwa lala!
Miezi thenasahara mara tatu ukiongeza nne, imemalizika, Kibuge bado kang'ang'ania usukuani wa mabua, akidai anajua njia ya kufika mtoni, lakini kila tukimuuliza tutafika lini anasema tumuache aendelee kuendesha mkweche tusimuingilie kazi.
Mkweche uko hoi bin taabani, viraka kila kona, mafuta ya breki yanavuja watu washayapigia hesabu eti yanatibu Utangotango, abiria wanapiga kelele Mkweche waenda chopi, utingo anasema tunapiga domo, tuende na wakati tushangilie mwendo kasi, tusihofu kuvuja kwa mafuta na kuungua kwa gasketi!
Huko juu ya Mkweche ni gombania goli, utingo wako wengi, kila mtu akivutia abiria wake na kujinadi kuwa anajua kubwabwaja hovyo, tairi lina viraka, fundi gari wanadai moto chini!
Kibuge kakaa kimya, anakenua meno ka mahindi ya Krismasi, kafutuka na ile gogozi yake, anakwangua gia ambalo linasaga chuma kwa kukosa girisi, watu wanalia tema mate, kusanya banjo ulainishe vyuma, anapayuka "babako analo?"
Sasa mimi nilifikiri Mkweche ni wetu sote, kumbe una watu wake maalum, wenye kujidai kuwa wao ndio wenye mali! Lakini hawachelewi kuchangisha nauli za ziada eti kusaidia Mkweche uende kwenye msitu mzuri watu wakajisaidie.
Mimi sijali hayo, nalia na ule ungo, Kibuge anatudanganya kila siku akienda kukusanya ufuta na giligilani! Tunamwambia hatuhitaji Sambusa na Kababu, tuna mbaazi na samaki nchanga wenye protini, yeye anadai, lazima tupate pera maziwa, la sivyo tutakufa njaa!
Akienda Jamatini, hakosi kujikomba komba na kutoa misifa kibao, kazi kuomba kula pozi na MaBaniani wa mitaani na si wale wenye maana ambao watamsukuma akapande mbaazi na kuziuza kwao.
Nasikia kuna Banyamulenge mmoja, kaamua kuwa yeye na ungo, basi hakuna urafiki na wala hataki tena kupewa viporo na chupi mtumba! Banyamulenge anasema lazima aanze kuwalisha Wagogo, Wanyaturu, Wazaramo na Warangi chakula na kuwavalisha nguo!
Najiuliza tena Kibuge vipi anapigwa teki na Banyamulenge? Vipi tena mwenzetu hataki Pera maziwa au kuomba Mshiko kwa Baniani eti hana ukoma anaweza jitegemea huku ni mtoto mdogo tuu?
Lakini nasikia, Kibuge yeye damu damu na Gabacholi! Hata yule Gabacholi anayejitapa kuwa mikuku na miembe yote ni yake ni mshikaji wake ingawa Baniani washamshitukia Gabacholi kuwa ni alosto!
Sisikitiki Kibuge kupunguza safari kukatisha mitaa na masafa, nasikitika atakachowaambia watoto wake na abiria mwaka huu, maana Baniani dengu zimekauka na wamekuwa wakali!
Mpeni Kibuge pole zangu, mwaambieni tumeshakubali kachoka, usukani wa Mkweche aachie wenye uwezo wauchukue!
Imepita muda sijamsikia akishika mchuma au kuzamia mtemba kutembeza ungo kukusanya unga, kauzu na mchunga!
Je yanayowakabili Baniani ni machungu mno mpaka Kibuge ameacha kukaa nje ya Jamatini akisubiri kiporo cha Cheuro, Pera maziwa na Kuku wa Tanduri na Tika?
Mara ya mwisho nilisikia alikuwa aongoze msafara wa Wagogo (FMES kumradhi usinishikie marimba!) kwenda Jamatini kudai unga wa dengu, choroko na pilipili, kisa kule nyumbani kwa kina Baniani, wameanza kulishana dengu na maziwa lala!
Miezi thenasahara mara tatu ukiongeza nne, imemalizika, Kibuge bado kang'ang'ania usukuani wa mabua, akidai anajua njia ya kufika mtoni, lakini kila tukimuuliza tutafika lini anasema tumuache aendelee kuendesha mkweche tusimuingilie kazi.
Mkweche uko hoi bin taabani, viraka kila kona, mafuta ya breki yanavuja watu washayapigia hesabu eti yanatibu Utangotango, abiria wanapiga kelele Mkweche waenda chopi, utingo anasema tunapiga domo, tuende na wakati tushangilie mwendo kasi, tusihofu kuvuja kwa mafuta na kuungua kwa gasketi!
Huko juu ya Mkweche ni gombania goli, utingo wako wengi, kila mtu akivutia abiria wake na kujinadi kuwa anajua kubwabwaja hovyo, tairi lina viraka, fundi gari wanadai moto chini!
Kibuge kakaa kimya, anakenua meno ka mahindi ya Krismasi, kafutuka na ile gogozi yake, anakwangua gia ambalo linasaga chuma kwa kukosa girisi, watu wanalia tema mate, kusanya banjo ulainishe vyuma, anapayuka "babako analo?"
Sasa mimi nilifikiri Mkweche ni wetu sote, kumbe una watu wake maalum, wenye kujidai kuwa wao ndio wenye mali! Lakini hawachelewi kuchangisha nauli za ziada eti kusaidia Mkweche uende kwenye msitu mzuri watu wakajisaidie.
Mimi sijali hayo, nalia na ule ungo, Kibuge anatudanganya kila siku akienda kukusanya ufuta na giligilani! Tunamwambia hatuhitaji Sambusa na Kababu, tuna mbaazi na samaki nchanga wenye protini, yeye anadai, lazima tupate pera maziwa, la sivyo tutakufa njaa!
Akienda Jamatini, hakosi kujikomba komba na kutoa misifa kibao, kazi kuomba kula pozi na MaBaniani wa mitaani na si wale wenye maana ambao watamsukuma akapande mbaazi na kuziuza kwao.
Nasikia kuna Banyamulenge mmoja, kaamua kuwa yeye na ungo, basi hakuna urafiki na wala hataki tena kupewa viporo na chupi mtumba! Banyamulenge anasema lazima aanze kuwalisha Wagogo, Wanyaturu, Wazaramo na Warangi chakula na kuwavalisha nguo!
Najiuliza tena Kibuge vipi anapigwa teki na Banyamulenge? Vipi tena mwenzetu hataki Pera maziwa au kuomba Mshiko kwa Baniani eti hana ukoma anaweza jitegemea huku ni mtoto mdogo tuu?
Lakini nasikia, Kibuge yeye damu damu na Gabacholi! Hata yule Gabacholi anayejitapa kuwa mikuku na miembe yote ni yake ni mshikaji wake ingawa Baniani washamshitukia Gabacholi kuwa ni alosto!
Sisikitiki Kibuge kupunguza safari kukatisha mitaa na masafa, nasikitika atakachowaambia watoto wake na abiria mwaka huu, maana Baniani dengu zimekauka na wamekuwa wakali!
Mpeni Kibuge pole zangu, mwaambieni tumeshakubali kachoka, usukani wa Mkweche aachie wenye uwezo wauchukue!