Ajira polisi zatangazwa

Ajira polisi zatangazwa

Mfichua siri

Senior Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
135
Reaction score
62
Wadau wa hili jukwaa mimi ni kijana niliye maliza kidato cha sita hivi karibuni na matokeo yangu yametoka hayana hata wiki moja, ndoto zangu ni kuwa Polisi hasa (trafic), katika kufuatilia ni namna gani nianze mchakato wa kuingia katika kulitumikia Taifa langu katika eneo hili nimepata hili Tangazo hapa chini, kwenye Red pananichanganya sana wanaonyesha ....Wataajiri vijana waliomaliza kidato cha nne mwaka2012 na kidato cha sita 2013 ambao ndo sisi, lakini inaonyesha tayari wanao orodha ya ya watu wa kuwaita kwenye Usaili ilihali wahusika ndo kwanza matokeo yetu yametoka na hawaonyeshi kama wanatutaka tuombe kazi.

Sasa swali langu ni je hizi kazi zilishatangazwa? na hawa form six wa mwaka 2013 wamewapata wapi? maana huwezi ukasema umemaliza kidato fulani wakati matokeo hayajatoka bado, naombeni msaada nataka kujua kama deadline ya kuomba bado na kama bado ni namna gani naweza kuomba hizi kazi na kuwaonyesha kwamba mimi nimemaliza kidato cha sita mwaka2013 maana hata transcripts bado hazijatoka, nimejaribu kwenda Polisi makao makuu juhudi za kuonana na wahusika zimegonga mwamba naombeni msaada plz.

Jeshi la Polisi Tanzania katika mwaka wa fedha 2013/2014 litaajiri vijana kutoka katika makundi yafuatayo: waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012, kidato cha sita mwaka 2013, JKT/JKU mwaka 2013 na vyuo vya elimu ya juu mwaka 2013.Taratibu zinakamilishwa ili waliomaliza kidato cha nne na sita na waliojaza fomu za maombi kabla ya kumaliza mitihani yao ya mwisho waitwe kwenye usaili. Usaili wa vijana wa JKT umekamilika mapema mwezi Aprili, 2013.

 
Kinachokusumbua ni roho ya Rushwa tu ndugu yangu.

Watake radhi Jeshi la Polisi na Serikali kwa ujumla, hata kama kuna Trafic amewahi kuthibitishwa kwamba ni mla rushwa haimaanishi kwamba wote ni wala rushwa
 
Maombi au fomu zinaletwa kwa wakuu wa shule alafu mnajaza kabla ya kumaliza,pale katika fomu utaacha anuani na namba ya simu
 
Cjajua utaratbu wasasa ila huwa wanaohitaj izo kaz huwa wanafanya maombi wakiwa shule

Hii haijakaa vizuri hata kidogo, ukiwa shule unaomba kwa elimu ipi? ilihali hujamaliza, naomba Mungu isiwe hivyo maana hizi marks zangu zitaniweka sana mtaani nimepiga E ya Commerce E ya Economics masomo yaliyobakia baraza halikuona sababu inayowazuia kunipa F
 
Wakati wenzio wanajaza zle form wewe ulikua wapi?
 
Hii haijakaa vizuri hata kidogo, ukiwa shule unaomba kwa elimu ipi? ilihali hujamaliza, naomba Mungu isiwe hivyo maana hizi marks zangu zitaniweka sana mtaani nimepiga E ya Commerce E ya Economics masomo yaliyobakia baraza halikuona sababu inayowazuia kunipa F

kwa elimu ipi! kwani ulipokuwa ukijaza fomu kwakuchagua hayao masomo uliyosoma kidato cha sita ulikuwa unachagua kwa kutumia kigezo cha elimu ipi? maana vilevile ulichagua ilihali matokeo yalikuwa bado. wewe sema kwamba hukuwa na wazo la kuwa trafic ila limekuja baada ya kupata hofu ya kukaa mtaani, sababu kama ungekuwa na nia hiyo ungejaza wakati ukiwa shuleni.
 
Kijana anajifanya mgumu kuelewa statement ndogo ila "UTAELEWA TU" wakati wenzako wakienda kweny interview kipawa ndo utajua walijaza form wakiwa shule. Ikiwa waliopo chuo wanajaza form na kumwachia dean of student azipeleke kwa Mwema itashndkana vp mkuu wa shule kubaki na form za vijana waliomaliza form six. ? Una macho unashndwa tizama soma lebo
 
Mbona wakuu wa mashule mengi waliwatangazi wanafunzi waliokuwa wanataka kujaza form za polisi. Na utaratibu huu umeanzishwa mwaka 2012. OVER
 
Mkuu jibu lipo hapa, ''Taratibu zinakamilishwa ili waliomaliza kidato cha nne na sita na waliojaza fomu za maombi kabla ya kumaliza mitihani yao ya mwisho waitwe kwenye usaili'' @Mfichua siri fomu ulijaza kabla ya kufanya mtihani wa mwisho.
 
http://www.policeforce.go.tz/index.php/career



TANGAZO LA AJIRA
Jeshi la Polisi Tanzania katika mwaka wa fedha 2013/2014 litaajiri vijana kutoka katika makundi yafuatayo: waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012, kidato cha sita mwaka 2013, JKT/JKU mwaka 2013 na vyuo vya elimu ya juu mwaka 2013.Taratibu zinakamilishwa ili waliomaliza kidato cha nne na sita na waliojaza fomu za maombi kabla ya kumaliza mitihani yao ya mwisho waitwe kwenye usaili. Usaili wa vijana wa JKT umekamilika mapema mwezi Aprili, 2013.Tangazo hili linawaalika vijana walioko kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini watakaohitimu masomo hivi karibuni na wanaopenda kujiunga na Jeshi la Polisi.Fomu za waombaji baada ya kujazwa kikamilifu ziletwe na mkuu wa chuo kabla ya tarehe 30/6/2013 kwa:Inspekta Jenerali wa Polisi,Makao Makuu ya Polisi,S.L.P. 9141,DAR ES SALAAM.Fani zinazotakiwa ni; Shahada za Menejimenti ya Rasilimali watu, Utawala, Uchumi, Usimamizi wa Sheria na Utekelezaji(BaLE), Ualimu, Sosholojia, Saikolojia na Ushauri Nasihi(Educational Psychology and Councelling),Takwimu, Lugha(Kiswahili/Kiingereza/Kifaransa/Kireno/Kiarabu), Usimamizi wa Programu za Maendeleo ya Jamii, Uhusiano wa Kimataifa, Uhandisi Mitambo(Mechanical Engineering), Uhandisi Kompyuta(Net Work, System Analyst, Data Base, Electronic & Telecommunications), Uandishi wa Habari, Mawasiliano ya Umma, Upangaji na Uendeshaji miradi, Jinsia na Watoto. Pia stashahada katika Usimamizi wa programu za maendeleo ya Jamii, Utunzaji kumbukumbu na Ukutubi.Sifa za Muombaji:
  • Awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Awe na umri usiozidi miaka 28.
  • Awe na tabia njema.
  • Awe hajawahi kushtakiwa kwa kosa la jinai.
  • Awe na afya njema.
  • Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
  • Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Asiwe na alama za kuchora mwilini(Tatuu).
  • Awe hajawahi kutumia madawa ya kulevya na
  • Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya Polisi.
Imetolewa na:Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,Makao Makuu ya Polisi,S.L.P. 9141,DAR ES SALAAM.


--
Kimambo, ON.
 
Back
Top Bottom