Ajira isikufanye kuwa Mtumwa...

Mtoa mada twende taratibu, hivi unaujua Ile msemo wa mtumikie kafiri???

Vijana wa siku hizi wanasema kuna misemo imepitwa na wakati, naweza nkakubali lakini hebu tuvae miwani zenye lens tofauti.

Namjua mtu ambae amesoma na hali ya kwao ilikuwa hohehahe, hakuna ajira, vibarua vya kubeba zege vilimfanya apate TB na kadhalika na kadhalika. Akapata mtu mmoja aliemuonea huruma, akamwambia tunakuingiza jeshini lakini mishahara miwili ya mwanzo sio yako. Akakubali na Leo ni mwanajeshi. Anaisaidia familia yake na yeye mwenyewe yake yanamuendea.

Nakubaliana na wewe kwamba isifikie tukawa watumwa, lakini amini amini nakwambieni hali ni mbaya zaidi ya tunavyoiona. Humuhumu jukwaani wapo ambao wamepata ajira zao kwa njia ambazo wanazijua wenyewe na nyengine ni as rushwa mbaya kabisa ya ngono. Na ajira hizo hizo ndio zikawa ukombozi wao na familia zao.

Sawa,hilo silibishi na ninaweza kusema hivyo kwa huyo mjeda ni kama bahati,vipi angeambiwa atoe mishahara kwa miezi 6?

Sawa nayo ingepita angekuwa huru(japo mm naww hatujui kama kweli yuko huru au bado ni mtumwa,inawezekana jamaa bado anamtumia akiwa na shida zake binafsi mpaka mtu unakosa raha ya kazi)haya vipi wale ambao wanautumwa endelevu,yeap;wako kazini wana hali nzuri kimaisha watoto wanasoma lakini kuna boss ambaye nyege zikimshika tuu ni unaambiwa akukute chumba namba flan,je huyu kama ni mke/mume wa mtu ndoa yao haiwezi ingia mashakani?

Familia itakuwa na furaha ya kweli?kuna magonjwa,kunyanyasikia nakuumia kisaikolojia n.k..jee kipi bora??maana bado huo ni utumwa pia,.
 
Si unaona ndo nlikuwa namwita dadaako joanah ili aje apate material ikiwezekana ajitose kwenye korosho? Mi ni jiniaz sema tu K Vant zimeharibu mfumo wangu wa kumbukumbu mpaka nashindwa kukumbuka kikokotoo kinahusika na Korosho au bunge lisilo na nguvu
Naona uvivu kusoma asee
 
Hakika haupo kwenye kundi la wanawake wazuri waliokosa akili na kupelekea ukosefu wao wa kukosa akili kusababisha kuja kuumia kwa sehemu Za siri ..

Aise abarikiwe mama mumu " kwa kuzaa binti mzuri mwenye Akili na hakuacha kukunyima/kukupunja malezi mema ...

Hongera ... uko vizuri -natamani kujifunza mengi zaidi kupitia wewe ...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika haupo kwenye kundi la wanawake wazuri waliokosa akili na kupelekea ukosefu wao wa kukosa akili kusababisha kuja kuumia kwa sehemu Za siri ..

Aise abarikiwe mama mumu " kwa kuzaa binti mzuri mwenye Akili na hakuacha kukunyima/kukupunja malezi mema ...

Hongera ... uko vizuri -natamani kujifunza mengi zaidi kupitia wewe ...

Sent using Jamii Forums mobile app
"mumu" hahaha

Hii inaitwa name calling. Unaweza chezea BAN nikiamka vibaya
 
ukitoa rushwa kupata kazi, ni dhahiri umefail integrity test. Naogopa sana na siwezi kutoa rushwa, najua itaniletea shida kwenye utendaji wangu wa kazi na pia nakua nimemkosea Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukosefu wa ajira ni changamoto ya dunia nzima.Kinachotofautisha kati ya nchi moja hadi nyingine ni ukubwa wa tatizo.Kila binadamu hubanwa na mahitaji ambayo kuyatimiza bila pesa haiwezekani.Pia,kupata fedha bila vyanzo ni ngumu.Chanzo kikuu cha mapato kwa wengi ni kuajiriwa,ama serikalini au taasisi binafsi.

Hali hiyo ndio husababisha watu wengine wawe tayari kufanya chochote ili wapate ajira.Wakiombwa rushwa ya fedha hutoa,wapo ambao hulazimika kutumia miili yao kama zawadi kwa mtoa ajira.

Wasio na fedha wanaahidi mishahara ya miezi kadhaa kulingana na makubaliano.Unakuta mtu kaanza kazi,badala ya hali yake kuwa bora kwa sababu ana kipato cha uhakika,maisha ndio yanazidi kuwa magumu.Kumbe anamfanyia kazi mtu.Na wapo wanaogeuzwa watumwa wa mapenzi pia.

Kila mtoa ajira anapohitaji kutimiza matakwa ya mwili wake,anaagiza tuu.Ndani ya ofisi moja unakuta wapo watu hata watano wenye kuchangia penzi la mtoa ajira kwa sababu wamepewa kazi kwa mtindo wa aina moja.

Kutoa rushwa ili kupata kazi ni matokeo ya juu ya kutojitambua.Unapaswa kuelewa kuwa unapoajiriwa maana yake umefuzu vigezo vya ajira,yaani unaonekana unaweza kutekeleza kazi ambayo umeomba na kutengeneza matokeo,sasa rushwa ya nini?

Zipo hasara ambazo utaandamana nazo ikiwa utaingia kazini kwa kutoa rushwa.Ukizielewa zitakuongoza kukataa rushwa ama kuwa mtumwa.

Unapoajiriwa kwa kutoa rushwa maana yake hiyo kazi umepewa na siyo kwamba umefuzu kutokana na vigezo vyako vya kwenye wasifu wa kitaaluma na uzoefu pamoja na jinsi ulivyojibu maswali ya wasaili.

Uliyempa rushwa anakuweka kwenye daraja la watu ambao amewapa kazi kwa kusaidiwa/kubebwa,kwa hiyo atakushurutisha kikazi kwa namna anavyotaka kwa sababu ya kiburi kuwa bila yeye usingepata kazi.

Unaweza kudhani rushwa uliyompa ni kigezo cha yeye kukuheshimu na kujua thamani yako,Hapo unajidanganya,kwani mlipokuwa mnapeana rushwa kuna mahali popote mliandikishiana au kutiliana saini???

Maoni yangu:pamoja na changamoto hii ya ajira tuliyonayo kwa Taifa,hasa kwetu vijana tusikubali kunyanyasika na kuwa watumwa kwa namna yoyote Ile,.pamoja na ugumu wa maisha na dhiki tunazopitia ni bora kuwa huru masikini kuliko tajiri mtumwa..uhuru wetu ni wathamani mnoo kupitia huo unaweza kufanya jambo lako na ukalisimamia kuliko kunyanyasika na kusimangwa.

Mungu ibariki Tanzania
Mungu tubariki vijana wa Tanzania..
Haahahah huu upupu wa akili, uliusahau wapi....mbona sijawai kuona unatema madini hivi!!!!

Anyway, sorry nimefukua kuburi....

Cc:
Miss you fundi...
 
Sawa,hilo silibishi,.na ninaweza kusema hivyo kwa huyo mjeda ni kama bahati,vipi angeambiwa atoe mishahara kwa miezi 6??sawa nayo ingepita angekuwa huru(japo mm naww hatujui kama kweli yuko huru au bado ni mtumwa,inawezekana jamaa bado anamtumia akiwa na shida zake binafsi mpaka mtu unakosa raha ya kazi)haya vipi wale ambao wanautumwa endelevu,yeap;wako kazini wana hali nzuri kimaisha watoto wanasoma lakini kuna boss ambaye nyege zikimshika tuu ni unaambiwa akukute chumba namba flan,je huyu kama ni mke/mume wa mtu ndoa yao haiwezi ingia mashakani?familia itakuwa na furaha ya kweli?kuna magonjwa,kunyanyasikia nakuumia kisaikolojia n.k..jee kipi bora??maana bado huo ni utumwa pia,.
Una madini sana best
 
Back
Top Bottom