Ajenda za maandamano zimeongezeka?

Ajenda za maandamano zimeongezeka?

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
104,319
Reaction score
183,599
Nauliza tu maana Naona wengine wanazungumzia bei za bidhaa ilhali tuliambiwa ajenda ya Maandamano ni miswada ya sheria za uchaguzi

Ufafanuzi tafadhali
 
Nauliza tu maana Naona wengine wanazungumzia bei za bidhaa ilhali tuliambiwa ajenda ya Maandamano ni miswada ya sheria za uchaguzi

Ufafanuzi tafadhali
Kama wewe hujanywa Chai au umelelala na njaa unakaribishwa kwenye Maandamano.

Kama wewe umechoshwa na Tozo za kuhamia Burundi unakaribishwa kwenye Maandamano.

Kama wewe umechoka kuzulumiwa Ardhi kama walivyo Masai wa Ngorongoro na Loliondo unakaribishwa kwenye maandamano.

Kama wewe unahasira na Bandari zote kukodishwa unakaribishwa kwenye Maandamano.

Kama wewe umechoshwa na Mgao wa Umeme basi unakaribishwa kwenye Maandamano.
 
Nauliza tu maana Naona wengine wanazungumzia bei za bidhaa ilhali tuliambiwa ajenda ya Maandamano ni miswada ya sheria za uchaguzi

Ufafanuzi tafadhali
1. Umeme hata niliko hakuna umeme
2. Sukari
3. Ajira Kwa vijana
4. Misuada yasheria za uchaguzi
5. Tume ya uchaguzi
 

Attachments

  • 20240123_184254.jpg
    20240123_184254.jpg
    415.9 KB · Views: 3
wanasema nyumba moja ila milango inakua ni mingi.Arab spring kama inahakisi flani hivi kwa wabantu ikianzia tz,Ug,Ken waasisi wakiwa makamanda wa CDM.

nimewaza mbaali kule kwa arab afican countries.
 
Kama wewe hujanywa Chai au umelelala na njaa unakaribishwa kwenye Maandamano.
Mmmm!
Hiyo ina maana nikaandamane kama sijakula kwa siku mbili mfululizo.

Hivi makasiriko ya mtu ambaye amelala na njaa na hajakula mnayajua? 😂😅😌
....lakini kama CHADEMA watatoa Maji, Juisi, Mihogo, Chipsi Mayai....watakuwa wameokoa Jahazi.

Wazingatie hili la watu kuwa na Njaa. Kadi ya CDM=Juisi ya Machungwa.

Tionane barabarani.
 
Mmmm!
Hiyo ina maana nikaandamane kama sijakula kwa siku mbili mfululizo.

Hivi makasiriko ya mtu ambaye amelala na njaa na hajakula mnayajua? 😂😅😌
....lakini kama CHADEMA watatoa Maji, Juisi, Mihogo, Chipsi Mayai....watakuwa wameokoa Jahazi.

Wazingatie hili la watu kuwa na Njaa. Kadi ya CDM=Juisi ya Machungwa.

Tionane barabarani.
Karibu Mkuu Ugali, mimi nitakununulia.
 
1. Umeme hata niliko hakuna umeme
2. Sukari
3. Ajira Kwa vijana
4. Misuada yasheria za uchaguzi
5. Tume ya uchaguzi
6. US$ 200 bilioni za dhahabu/makinikia zimeishia wapi?
7. Noah za kila mtanzania zinawasili lini bandarin?
 
Karibu Mkuu Ugali, mimi nitakununulia.
Mbingu itafunguka!

...mpaka sashivi sijalala, na sijakula chakula cha jioni/usiku

...kieleweke kweli hiyo kesho, manake hutaki ukutane na mimi nikiwa na makasiriko ya Njaa-Mbowe anaweza kuitisha Uchaguzi wa Mwenyekiti papohapo kwa vurumai zangu.

...Ahsante
 
Yani hata kama hujui chochote kinachoendelea ww andamana tuu utapewa muongozo huko huko juu kwa juu
 
Maandamano yanaenda kukusemea hata wewe johnthebaptist . Karibu kwenye maandamano.

Tutaangazia yafuatayo:-
*Hali ngumu ya maisha ya mtanzania.
*Bei za bidhaa kupanda kiholela.
*Waathirika wa mafuriko DSM kupuuzwa na kifanyiwa dhihaka na RC Chalamila.
*Miswada ya sheria za uchaguzi.
 
Back
Top Bottom