TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,870
- 5,755
Kelele zooote ni kwa sababu Magufuli amewabana kwelikweli. Zile blaablaa za oh,
rushwa imekidhiri, watumishi wa Umma wanajiona miungu watu, Serikali inaibiwa kwenye mikodini kutokana na kusafirisha mchanga, TRA hawakusanyi kodi, Bandarini kuna ubadhilifu na porojo kibao hazipo tena.
Huku mitaani heshima debe, tofauti ya wenye nacho na wasio nacho imekuwa ndogo sana, hakuna cha wa viti virefu wala vifupi.
Nawaza tu uchaguzi ukifanyika leo, hoja za Wapinzani ili wapewe kura zitakuwa Magufuli ni dikteta? Bashite? na upuuzi mwingine mwingi? Ubashite wa mtu Unatusaidia nini sisi watanzania? Hata kama angekuwa Dikteta kweli, kwa haya anayoyafanya Magufuli basi tulipaswa tuufurahie huo udikteta wake kama ungalikuwepo maana nchi imeanza kurudi kwenye misingi.
Au agenda yao itakuwa ni kulaani ukweli wa rais kuwaondoa watu kwenye mazoea ya kutofanyakazi? Nani hajui hivi sasa watanzania wameanza kubadilika na kuchapakazi badala ya kusubiri pesa za wala rushwa, mafisadi, za wauza unga. Pesa za hovyohovyo.
Au agenda yao itakuwa kulaani wauza unga kutangazwa hadharani? Katika hili wasipoangalia watanzania watawapopoa mawe maana adhari ya biashara hii haramu ilikuwa imefikia pabaya na tayari madhara haya yalishaanza kuonekana kwa serikali, familia na hata kwa mtu mmoja mmoja.
Au agenda yao ingekuwa kulaani Serikali kununua ndege, kujenga reli kwa kiwango cha standard gauge, kujenga barabara za juu, bomba la mafuta kutoka uganda hadi Tanzania n.k kwa propaganda kwamba mambo hayo hayana faida kwa mtu wa kawaida?
Ni mtanzania gani hajui ndege, reli , bomba la mafuta n,k vitakuza uchumi wetu na hivyo kusaidia upatikanaji wa huduma za jamii kama vile madawa, shule, maji, umeme n.k, huduma ambazo zinamgusa mwananchi wa kawaida moja kwa moja.
Au agenda yao ingekuwa kuwaambia wanancni jinsi gani Lissu, Gwajima na mavuvuzela mengjne yanavyojitanua kuinanga serikali?
Onyo: Kwa porojo,propaganda, udaku na hoja nyepesi nyepesi dhidi ya serikali ya Magufuli manpaswa kujitathmini sana.
rushwa imekidhiri, watumishi wa Umma wanajiona miungu watu, Serikali inaibiwa kwenye mikodini kutokana na kusafirisha mchanga, TRA hawakusanyi kodi, Bandarini kuna ubadhilifu na porojo kibao hazipo tena.
Huku mitaani heshima debe, tofauti ya wenye nacho na wasio nacho imekuwa ndogo sana, hakuna cha wa viti virefu wala vifupi.
Nawaza tu uchaguzi ukifanyika leo, hoja za Wapinzani ili wapewe kura zitakuwa Magufuli ni dikteta? Bashite? na upuuzi mwingine mwingi? Ubashite wa mtu Unatusaidia nini sisi watanzania? Hata kama angekuwa Dikteta kweli, kwa haya anayoyafanya Magufuli basi tulipaswa tuufurahie huo udikteta wake kama ungalikuwepo maana nchi imeanza kurudi kwenye misingi.
Au agenda yao itakuwa ni kulaani ukweli wa rais kuwaondoa watu kwenye mazoea ya kutofanyakazi? Nani hajui hivi sasa watanzania wameanza kubadilika na kuchapakazi badala ya kusubiri pesa za wala rushwa, mafisadi, za wauza unga. Pesa za hovyohovyo.
Au agenda yao itakuwa kulaani wauza unga kutangazwa hadharani? Katika hili wasipoangalia watanzania watawapopoa mawe maana adhari ya biashara hii haramu ilikuwa imefikia pabaya na tayari madhara haya yalishaanza kuonekana kwa serikali, familia na hata kwa mtu mmoja mmoja.
Au agenda yao ingekuwa kulaani Serikali kununua ndege, kujenga reli kwa kiwango cha standard gauge, kujenga barabara za juu, bomba la mafuta kutoka uganda hadi Tanzania n.k kwa propaganda kwamba mambo hayo hayana faida kwa mtu wa kawaida?
Ni mtanzania gani hajui ndege, reli , bomba la mafuta n,k vitakuza uchumi wetu na hivyo kusaidia upatikanaji wa huduma za jamii kama vile madawa, shule, maji, umeme n.k, huduma ambazo zinamgusa mwananchi wa kawaida moja kwa moja.
Au agenda yao ingekuwa kuwaambia wanancni jinsi gani Lissu, Gwajima na mavuvuzela mengjne yanavyojitanua kuinanga serikali?
Onyo: Kwa porojo,propaganda, udaku na hoja nyepesi nyepesi dhidi ya serikali ya Magufuli manpaswa kujitathmini sana.