BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,118
๐๐ฟ Neno "AJALI" limetumika sana tangu Lowassa afariki.
๐๐ฟ Neno hilo limetumika kuelezea majanga ya kutengenezwa yaliyomkuta Lowassa.
๐๐ฟ Kwa mujibu wa Raphael Chegeni, ajali hizo ndizo zilizoharakisha kifo cha Lowassa.
๐๐ฟ Kilichomsononesha zaidi Lowassa ni kuwa ajali hizo zilitengenezwa na waliovaa ngozi ya Urafiki.
๐๐ฟ Ajali kubwa zaidi ni ile ya Mwaka 2008 iliyogharimu nafasi yake ya Uwaziri Mkuu.
๐๐ฟ Mtengenezaji wa ajali hiyo hatimaye amejulikana wakati wa msiba wa Lowassa
๐๐ฟ Licha ya kujinasibu kuwa "Rafiki Mkubwa" wa Lowassa, siyo ndugu au rafiki yeyote wa Lowassa aliyetamka kuwa Mheshimiwa huyo alishiriki kwenye kumuuguza au kuifariji familia.
๐๐ฟ Hakuna hotuba yeyote iliyoonesha ukaribu wa Mheshimiwa huyo na Hayati Lowassa.
๐๐ฟ Hata yeye mwenyewe wakati wa kuaga mwili wa Lowassa hakupeana mkono wala kuzungumza na mwanafamilia yeyote wa Lowassa.
๐๐ฟ Pale Masaki hakuingia ndani kuwapa pole wafiwa baada ya kusaini kitabu cha maombolezo.
๐๐ฟ Pale Monduli, wengine walienda kuiaga familia kwa ukaribu, yeye akapotea kama mvuke.
๐๐ฟ Neno letu kwa watengeneza ajali wote: Acheni tabia hiyo chafu.
๐๐ฟMnatupora viongozi wetu na mnasononesha mioyo ya watu na kuacha mama zetu Wajane.
๐๐ฟ Msipoacha mtakufa KIBUDU
LALA SALAMA SHUJAA. TUTAONANA BAADAE