Ajali za bodaboda zaua 400

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,293
33,078
JESHI la Polisi kupitia kikosi cha Usalama barabarani nchini kimesema jumla ya ajali za pikipiki (bodaboda) 2601 zilizotokea kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu zilisababisha vifo vya madereva 487 wa pikipiki hizo.

Akizungumza na gazeti hili jana ofisini kwake, Kamishna Msaidi wa Polisi, kikosi cha usalama barabarani Johansen Kahatano alisema ajali hizo zinazidi kuongezeka kila mwaka kutokana na sababu mbalimbali.

“Kwa mwaka 2009 kulitokea ajali 3406 na waliokufa ni 502,mwaka uliofuata ajali 4363 na vifo 683 na ilipofikia mwaka 2011 zilitpkea ajali zingine 5384 na waliokufa ni 945, taarifa hii inaonyesha kuwa kila mwaka vifo vinaongezeka”alisema Kahatano.

Alisema kuongezeka kwa bodaboda na uelewa mdogo wa sheria za usalama barabarani kwa madereva hao ndiyo sababu kubwa ya ongezeko la ajali hizo.

Alisema pikipiki zilizo sajiliwa mwaka 2009 kwa ajili ya biashara hiyo ni 87,826 na hadi kufikia mwaka 2011 kulikuwa na pikipiki 1,34,831 na kwamba wamiliki wake wamekuwa hawana elimu ya kutosha kwa ajili ya kuwasaidia madereva wao.

Aliongeza kuwa kutokana na changamoto hiyo wamepata msaada kutoka kwa Taasisi zisizo za kiserikali kwa mikoa mbalimbali hapa nchini zinazotoa elimu ya mafunzo ya udereva kwa pikipiki ili kupunguza ongezeko la ajali

“Mafunzo hayo yalianza Juni mwaka huu,Kwa mkoa wa Tanga kuna taasisi inayoitwa APEC inatoa mafunzo kwa Bodaboda 2000 hadi sasa na Mkoa wa Mtwara inaitwa British Gas inatoa mafunzo kwa Bodaboda 600,lengo ni kupunguza ajali hizi kote nchini”alisema Kahatano.

Hata hivyo alikiri kuelemewa na utekelezaji wa jukumu la kukamata waendesha pikipiki wanaovunja sheria barabarani kutokana na wingi wao ukilinganisha na uchache wa Askari wa usalama barabarani.
Kwa sasa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Sumatra limeingia makubaliano na halmashauri zote nchini kuanzia Julai mwaka huu kutoa leseni ya biashara kwa kila dereva wa bodaboda ili kuwatambua rasmi na kupunguza matukio ya ukabaji dhidi yao.

Aidha aliwataka madereva wote na wamiliki wao kutambua sheria za barabarani na kujali uhai wao pindi wanapokuwa barabarani na kwamba endapo kila mmoja atafanya hivyo itakuwa ni njia sahihi ya kupunguza au kumalizika ajali hizo.Ajali za bodaboda zaua 400
 
Back
Top Bottom