barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,739
- 32,874
Kuna ajali imetokea Rombo jioninya tarehe 05/02/2017.
Viongoz wa CCM waliokuja kushiriki miaka 40 ya ccm Kimkoa iliofanyika wilayani Rombo akiwapo MNEC wa Same wamepata ajali maeneo ya Mwika wakirejea makwao toka Rombo.
Kwa taalifa za awali watu watano wamefariki ktk ajali hiyo.
Gari hiyo ilikuwa ni ya MNEC wa SAME na alikuwa amebeba Wanavyuo pia
========
UPDATE:
Timu ya waandishi waliotoka Moshi kwenye sherehe za miaka 40 ya CCM Moshi yapata ajali.
Inasemekana watu kadhaa wamefariki papo hapo.
Ajali imehusisha fuso, bodaboda na gari nyingine waliokuwemo waandishi pia.
Kwa mujibu wa Mwandishi wa Habari wa Majira, Flora Temba kwenye gari walikuwemo watu watano na wanne wamefariki amepona Kimambo Jackson aliyekuwa anaendesha gari.
Chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni Fuso lililokuwa nyuma kufeli breki kisha kuwagonga na kuwasukuma kwenda mtaroni kisha kugonga pia Bodaboda na Fuso kwenda kupinduka.
Waliofariki inadaiwa ni zaidi ya wanne kwakuwa kuna waliokuwa kwenye Fuso pamoja na mwendesha bodaboda.
Taarifa za awali zinaonyesha waliofariki ni mwandishi Arnold Swai kafariki. Mwandishi mwingine wa gazeti la Habari leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Hai.
Taarifa zaidi zinasema walikuwa kwenye shughuli za chama (CCM) wilayani Rombo.
Hawa hapa viongozi wa UVCCM na CCM waliofariki kwenye ajali ya gari jana Rombo:
Anold Swai (M/kiti UVCCM Hai)
Ally Mmbaga(MNEC Same)
Edwin Msele (K/Hamasa Shrk Kilimanjaro)
Anna Malamsha.
Ajali imetokea maeneo ya Mwika Mawanjeni maarufu kama Bar Mpya Moshi mkoani Kilimanjaro. Inaelezwa kuwa ndani ya gari walikuwemo watu sita wakiwemo viongozi wa CCM wakitoka kushiriki sherehe za miaka 40 ya CCM kimkoa yaliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Msingi Shauri Tanga wilayani Rombo. Chanzo cha ajali inaelezwa kuwa ni fuso kufeli breki na kuligonga gari dogo.
“Waliofariki ni mwenyekiti wa Uvccm wilayani hai na mwandishi wa habari Leo Arnold Swai, mjumbe wa NEC ya CCM na Katibu wa CWT mkoa wa Kilimanjaro ally Mmbaga na wanafunzi makada wa CCM kutoka vyuo vikuu vya ushirika na KCM. Majeruhi wa ajali hiyo ni Jackson Kimambo amekimbizwa Hospitali na wote walikuwa wakitoka kwenye maadhimisho ya kilele cha miaka 40 ya kuzaliwa CCM wilayani Rombo” -Ujumbe wa mwandishi wa habari Lucy Ulomi ambaye sasa yupo hospitali ya KCMC akifuatilia habari hiyo.
Viongoz wa CCM waliokuja kushiriki miaka 40 ya ccm Kimkoa iliofanyika wilayani Rombo akiwapo MNEC wa Same wamepata ajali maeneo ya Mwika wakirejea makwao toka Rombo.
Kwa taalifa za awali watu watano wamefariki ktk ajali hiyo.
Gari hiyo ilikuwa ni ya MNEC wa SAME na alikuwa amebeba Wanavyuo pia
========
UPDATE:
Timu ya waandishi waliotoka Moshi kwenye sherehe za miaka 40 ya CCM Moshi yapata ajali.
Inasemekana watu kadhaa wamefariki papo hapo.
Ajali imehusisha fuso, bodaboda na gari nyingine waliokuwemo waandishi pia.
Kwa mujibu wa Mwandishi wa Habari wa Majira, Flora Temba kwenye gari walikuwemo watu watano na wanne wamefariki amepona Kimambo Jackson aliyekuwa anaendesha gari.
Chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni Fuso lililokuwa nyuma kufeli breki kisha kuwagonga na kuwasukuma kwenda mtaroni kisha kugonga pia Bodaboda na Fuso kwenda kupinduka.
Waliofariki inadaiwa ni zaidi ya wanne kwakuwa kuna waliokuwa kwenye Fuso pamoja na mwendesha bodaboda.
Taarifa za awali zinaonyesha waliofariki ni mwandishi Arnold Swai kafariki. Mwandishi mwingine wa gazeti la Habari leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Hai.
Taarifa zaidi zinasema walikuwa kwenye shughuli za chama (CCM) wilayani Rombo.
Hawa hapa viongozi wa UVCCM na CCM waliofariki kwenye ajali ya gari jana Rombo:

Anold Swai (M/kiti UVCCM Hai)

Ally Mmbaga(MNEC Same)

Edwin Msele (K/Hamasa Shrk Kilimanjaro)

Anna Malamsha.
Ajali imetokea maeneo ya Mwika Mawanjeni maarufu kama Bar Mpya Moshi mkoani Kilimanjaro. Inaelezwa kuwa ndani ya gari walikuwemo watu sita wakiwemo viongozi wa CCM wakitoka kushiriki sherehe za miaka 40 ya CCM kimkoa yaliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Msingi Shauri Tanga wilayani Rombo. Chanzo cha ajali inaelezwa kuwa ni fuso kufeli breki na kuligonga gari dogo.
“Waliofariki ni mwenyekiti wa Uvccm wilayani hai na mwandishi wa habari Leo Arnold Swai, mjumbe wa NEC ya CCM na Katibu wa CWT mkoa wa Kilimanjaro ally Mmbaga na wanafunzi makada wa CCM kutoka vyuo vikuu vya ushirika na KCM. Majeruhi wa ajali hiyo ni Jackson Kimambo amekimbizwa Hospitali na wote walikuwa wakitoka kwenye maadhimisho ya kilele cha miaka 40 ya kuzaliwa CCM wilayani Rombo” -Ujumbe wa mwandishi wa habari Lucy Ulomi ambaye sasa yupo hospitali ya KCMC akifuatilia habari hiyo.