Ajali Ubungo Riverside

Hii sasa ni freemason ila ngoja wale wakombozi walioko mtwara watatua hapo Dar na hata huku kanda ya kaskazini na patachimbika. Poleni wote waliofikwa na mauti na marehemu wote walale kwa Amani ya bwana!
 
ngoja niwasiliane na ndugu zangu kwanza huko dar....huwezi jua!!!
 
Ukisafiri hata kwa miguu siku hizi, ukifika salama ni jambo la kumshukuru Mungu. Mungu awalaze mahali pema peponi, waliofariki. Na awape nguvu wafiwa!
 
Ninasikitika kuawaarifu kua kuna ajali mbaya imetokea Ubongo Riverside ambapo gari aina ya lori limeacha njia na kugonga watu.

Kwa uchache inasemekana maiti 20 zimeokotwa eneo la ajali.

Habari zaidi zitawajia hivi punde
Nimepita hapo mahali hivi punde. idadi ya marehemu haiwezi kufikia hiyo idadi ulitoitaja Mkuu
 
free maseee @ work
Inawezekana sadaka za damu zinatakiwa kuzimu!!!!!!!! Ehee Mungu tuepushe na roho ya ajali na laana ya kuzimu!!! Watanzania kutubu na kumpokea Yesu na kuacha madhambi ni muhimu na Maombi pia!!!!!!!!!

 
kuna ajali imetokea river-side pale ambapo lori limepoteza mwelekeo na kugonga magari mengine manne na kisha kudondokea daladala lilojaa abiria..watu wamefariki huku wengine wakikatika vichwa...harakati za kuwanasua zinaendelea
 
Duh!
Wapumzike kwa amani....inauma sana.
 
kuna ajali imetokea river-side pale ambapo lori limepoteza mwelekeo na kugonga magari mengine manne na kisha kudondokea daladala lilojaa abiria..watu wamefariki huku wengine wakikatika vichwa...harakati za kuwanasua zinaendelea

Mbaya!
 
Hii sasa ni freemason ila ngoja wale wakombozi walioko mtwara watatua hapo Dar na hata huku kanda ya kaskazini na patachimbika. Poleni wote waliofikwa na mauti na marehemu wote walale kwa Amani ya bwana!
Mkuu Livapool hao wakombozi ni kina nani??????? Kazi yao ni ipi????????
 
mh!
Poleni watanzania.
Mungu awarehem watu wake.
Awapokee watu wake katika enz yake.
Atupe kufa kwema nasi tulioachwa hai.
 
Hizi ajali za barabarani sasa jamani! Magari mabovu yanaruhusiwaje kutembea barabarani? Na madereva wasiokuwa na leseni wamejaa tele mitaani!

Ni uzembe wa Mambo ya ndani ambayo imeshindwa kabisa kuwadhibiti polisi ili wahakikishe sheria za barabarani zinafuatwa kila siku. Barabara zetu kusema kweli zinatisha sana. Ukitoka asubuhi na kurudi nyumbani jioni unashukuru Mungu, ukiwa safarini roho mkononi ukifika salama unabaki na wasiwasi kama safari ya kurudi itaisha salama. Nchi yetu imeoza hili siyo siri kila mahali pamejaa madudu tu.

Poleni sana wafiwa Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi~AMEN
 
Mkuu, ya kweli haya?
mbona taarifa mnaleta zinakinzana?
kuna ajali imetokea river-side pale ambapo lori limepoteza mwelekeo na kugonga magari mengine manne na kisha kudondokea daladala lilojaa abiria..watu wamefariki huku wengine wakikatika vichwa...harakati za kuwanasua zinaendelea
 
Ujinga,umaskini,Maradhi,ufisadi sasa ajali MUNGU tunusuru.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…