Ajali tena MASEYU-MOROGORO

Ajali tena MASEYU-MOROGORO

Wadau ni kweli wasafiri wa leo kati ya DSM na MORO ni mateso makubwa kwani mpaka sasa saa tano asubuhi hii hakuna gari yoyote ya kutoka DSM iliyopita hapa stendi MORO.
 
Poleni sana hususan wafiwa. Morogoro road inatakiwa kupanuliwa at least mpaka Chalinze.
 
Wadau ni kweli wasafiri wa leo kati ya DSM na MORO ni mateso makubwa kwani mpaka sasa saa tano asubuhi hii hakuna gari yoyote ya kutoka DSM iliyopita hapa stendi MORO.

tatizo linakuja pale BREAK DOWN INAPOTAKIWA KUJA KUYATOA,ITAPITA WAPI???,MAANA HIYO SAA 8 USIKU TUMEPITA NJIA ZA PANYA MAPORINI HADI TUMEFANIKIWA KUIMALIZA HIYO FOLEN,LAKIN PIA INAONEKANA HAPA MORO HAKUNA MAGARI YA KUWEZESHA HUO MCHAKATO,IFIKE WAKAT SERIKALI IWEKEZE KWENYE TRENI ZA kwenda kasi
 
Hapo mahala 'MISEYU'sijui kuna shetani gani.Maana wiki tatu zilizopita kuna ghari ya Azam ilikula mzinga hapo kwenye kona ya kutelemka kuelekea morogoro!

safari za usiku ni majanga ingawa nzuri sana
 
What is the status now? It is 13:08 now....barabara imeshafunguliwa? Magari yanatembea? The government can't afford a highway to be closed for such a long time!
 
Duuh poleni wafiwa na majeruhi... ila mkuu ni magari 300 au 3000??
 
nchi hiii bwana, yaani kila kitu bora liende, nashangaa yakianza majigambo ya vyuo, eti udsm wanatoka kifua mbele kuwa wanaongoza kutoa watu wenye madaraka mmakubwa serikalini, mmadaraka makubwa with no meaning ......mchumi gani huyu hawezi even kuona oppotunity costs?, mambo ya kipumbavu yanaendelea yeye yupo japan, hapo kijitonyama mtu ametumbukia kisimani, inawezekanaa asipate taarifa au anajuaa kilichofanyika lkn atkaa kinya kama babu na wajukuul azi ipo hiki kipindi kilichobaki, tunalo watz!

mchumi grade ONE=mwigulu michembe!!
 
Tz inadeal na urban area likitokea jambo faster..cku zlzpta kuna dogo alipata ajal mliman city alivyotoka 2 getin gar ikaruka mferejin faster trafic wa kutosha dk 10 gar ya kuvuta ikafka ukipata ajal out na reception utaisoma ndo Tz ye2 2fanyaje...wafiwa na mliokaa kwenye folen polen
 
kwakweli watu wanaotia huruma pale ni abiria na wale wafanyabiashara wa NYANYA WANAOWAH KARIAKOO

Nimepita hapo nimeona hii ajali, na polisi alikuwa keshafika Ila dereva wa fuso alishaondolewa, kuna damu tu pale alipokuwa amekaa na pamehaibika kabisa.

Madereva tukiwa barabarani huwa tuna haraka sana na fujo nyingi sisizo na msingi. Tukishafika tulikokuwa tunakwenda na kujiuliza tulichokuwa tunakimbilia hata kuhatarisha maisha jibu ni hakuna. Utakuta mtu anakupita kwa kazi sana na baadaye unamkuta kasimama mahali na anapiga story tu. Kimsingi huwa hakuna cha maana tunachokimbilia kila wakati. Tuache mambo haya jamani, tukumbuke watoto wetu wanatuhitaji.
 
WATU WATANO WAFARIKI DUNIA BAADA YA MALORI MATATU KUPATA AJALI MASEYU MOROGORO.


Source: http://jumamtanda.blogspot.com/2013/06/watu-watano-wafariki-dunia-baada-ya.html

Mkoroshokigoli


DSC07322.JPG

WATU watano wamefariki dunia baada ya kutokea kwa ajali ilihusisha magari matatu katika eneo la Maseyu tarafa ya Mikese katika barabara kuu ya Dar es Salaam-Morogoro katika tukio lililotokea majira ya saa 1:45 usiku wa Juni Mosi mkoani hapa. PICHA JUMAMTANDA.BLOGSPOT.COM

Mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Morogoro, Boniface Mbao akizungumza katika eneo la tukio alisema kuwa ajali hiyo imehusisha magari matatu aina ya Mistubishi Fuso lenye namba ya usajili T 855 BZW kugongana na Scania zenye namba ya usajili T 657 AFJ yaliyogongana uso kwa uso na wakati yakitaka kulipita scania nyingine yenye namba ya usajili na T 827 AJJ ambayo ilishindwa kupanda mlima na kuziba robotatu ya barabara na kupelekea watu watano kufariki dunia na majeruhi wawili.
 
Back
Top Bottom