Ajali mbaya ya BASI, LORI, NOAH, HIACE na PIKIPIKI.

Ajali mbaya ya BASI, LORI, NOAH, HIACE na PIKIPIKI.

mende 2014

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2014
Posts
763
Reaction score
131
Ajali iliyotokea jana na leo hapa Bunda ni katika maeneo yafuatayo. Bulamba hiace na pikipiki jana wanne wamefariki, Lori na nyumbu eneo la Serengeti jana wanne wamefariki na majeruhi 40, Noah na pikipiki eneo la Balili jana afariki mmoja ambaye ni mtendaji, Hiace na pikipiki eneo la daraja mbili karibu na Vilian Ukerewe road leo afariki mmoja, Zakaria express eneo la Serengeti ikitokea Tarime kwenda Mwanza nayo yaua ila uhakika wa waliofariki haijajulikana. Yote haya yametokea wilaya ya Bunda. Hospitali ya BDDH imejaa majeruhi wa ajali hizo.
 
poleni wabunda na wafiwa na majeruh mungu awape neema ya faraja mapema .ameen
 
Ndugu zangu wengi wa Mkoa wa Mara ni wababe mno. Hata sheria za barabarani wanataka kuoneshana ubabe! Ajali hizi zina gharama kubwa sana kwenye familia za marehemu/majeruhi na taifa kwa jumla.
 
Ninasikitishwa sana na UZEMBE wa hawa madereva

Ni bora wawe wazembe kwenye ngono lakini sio kwenye vyombo vya usafiri vyenye watu wengi

Poleni majeruhi na mpone mapema

RIP marehemu wote

Mungu naomba uwafariji wote
 
Ndugu zangu wengi wa Mkoa wa Mara ni wababe mno. Hata sheria za barabarani wanataka kuoneshana ubabe! Ajali hizi zina gharama kubwa sana kwenye familia za marehemu/majeruhi na taifa kwa jumla.

Mkuu hivi ubabe huu hadi kwenye hatari ya kifo?
 
Poleni wafiwa na majeruhi.

Mleta mada hata picha moja tu umeshindwa kuchukuwa?
 
Polen wafiwa na Mungu afanye wepesi wa majeruhi kupina haraka
 
Inatisha pia napata wasiwasi na hao wanaohusika na utoaji wa hizo leseni. Pole kwa wafiwa.
 
Poleni ndg zangu wana bunda! Tunawaombea maheruhi wapone haraka! Madereva kuweni makini muwapo barabarani, ajali hizi zinagharimu maisha ya watu!
 
Zakaria wanayaita ndege ya ardhini... Yanakimbizwa ni balaa....

Poleni majeruhi, r.i.p marehemu wote....
 
Poleni sana wafiwa na majeruhi wote wa ajali hizo maana ni sikitisho sana. Yaani Zakaria ndo hukimbizwa kama vile inafukuzwa na kifo. May the soul RIP.
 
Jamaa Hawa ni wababe sana mabasi ya tarime zakaria batco yanakimbia mno hata matuta hayajali ila ukithibutu kumkemea dereva abiria wanakurudi poleni waathirika kemeeni mwendo wa madereva mwendo wa kawaida unafaa sana
 
Poleni wafiwa na majeruhi.

Mleta mada hata picha moja tu umeshindwa kuchukuwa?

Ndugu yangu natumia simu ndo maana kuja attach picha inakuwa ngumu niliishajaribu nikashindwa labda kama unafahamu nielekeze.
 
Duh! Poleni sana ndugu zangu. Mungu awafanyie wepesi majeruhi na awalaze pema peponi waliotangulia mbele ya haki.
 
Back
Top Bottom