Kijana leo
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 2,860
- 812
inasikitisha sana, huyo konda kafanya ukatili, huwezi msukuma mtu gari likiwa linatembea, pole kwa waliopoteza ndugu yao.
Innarillah wainarillah rajiun
Mimi nazani kama kuna abiria alikuwepo kwwnye hiyo daladala na anasoma Uzi huu na aliona hilo tukio muwakamate haraka sana hao wahusika kondakta na dereva wapelekwe polisi. Pia hata hilo Lori naamini kwa foleni ya Mandela road hata Ubungo halijafika kama kuna washuhuda wanalikumbuka Lori walifukuzie na bodaboda watalikamata.
Habari wapendwa katika Bwana
Kuna ajali imetokea Tazara karibia na mataa ya Tazara Bakhresa kuna binti amegongwa na Lori la mizigo. Kichwa chote kimesagika kwakuwa tairi zimepita kichwani hivyo kichwa kimetoka kabisa hivyo hajulikani. Polisi wamezuia kuchukua picha lakini alikuwa amevaa simpo nyeusi. Nguo hazitambuliki. Anaonekana kwa kukisia ni kama binti wa miaka 12-17 hivi.
Chanzo cha ajali alikuwa anajaribu kupanda daladala iliojaa kupita kiasi konda akamshusha kwalengo lakunguza abiria bahati mbaya akadondoka ndipo Lori likamkanyaga.
Hapo kwenye red ndo huwa nachoka kabisa na kupoteza hamu ya kushi Dar! Watu tumekosa ubinadam kabisa, tukio linaweza kufanyika hapa na watu wanaangalia tu wala hawatoi msaada! Inakuwaje mtu amekanyaga mtu halafu anakimbia tu bila kusimama au watu kumzuia asiondoke? Inakuwaje konda anasukuma mtoto bila watu wengine kutoa msaada?
Dar jifunzeni ubinadam aisee!! Matukio mengi tu hapo Dar yanatokea akina mama wanakwapuliwa mikoba na vibaka huku watu wanaangalia tu bila kutoa msaada wowote!!