Ajali mbaya kati ya gari ya magereza na lori

Ajali mbaya kati ya gari ya magereza na lori

shalua mpanda

Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
28
Reaction score
4
Ajali mbaya imetokea muda mfupi uliopita maeneo ya Mkenge wilaya ya Mkuranga kati ya gari ya magereza iliyobeba mfungwa ikitokea Kimanzichana kuja Mkuranga mjini,askari magereza watatu wamefariki dunia na mfungwa mmoja amefariki pia.Chanzo cha ajali ni dereva wa gari ya magereza kuhama eneo lake na kulifuata lori upande wake.Dereva wa gari ya magereza amepata majeraha kidogo.
 

Attachments

  • 1398164613975.jpg
    1398164613975.jpg
    37.3 KB · Views: 629
  • 1398164671078.jpg
    1398164671078.jpg
    36.5 KB · Views: 623
  • 1398164715549.jpg
    1398164715549.jpg
    41.1 KB · Views: 551
  • 1398164790259.jpg
    1398164790259.jpg
    52.9 KB · Views: 557
Familia nyingine zinaendelea kupoteza wapendwa wao hivi hivi kwa uzembe na ajali zinazozuilika. Wake mliopoteza waume na watoto mliopoteza wazazi poleni sana na Mungu wa Mbinguni awafariji na kuwatunza
 
Haikua na escort?

Hayo maroli ya magereza huwa yanaendeshwa kwa kasi yakitegemewa kupishwa wakati hayana vingora wala vimulimuli na mengi ni mabovu.
 
Udereva wa kujihami ndio utakaopunguza kwa kiasi kikubwa matukio ya ajali za barabarani.
 
ni vyema sasa, Tanzania tukaja na miradi mingi ya usalama barabarani, kwani ongozeko la ajali ni kubwa sana, elimu ya kutosha inahitajika kwa watumiaji wa barabara. poleni wafiwa na familia kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom