Ajali mbaya basi la Green Star (Dar - Kahama)

Ajali mbaya basi la Green Star (Dar - Kahama)

vengu

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
740
Reaction score
536
basi hilo lilikua linatokea Dar kwenda Kahama, dereva alikuwa anaovertake roli akakutana uso kwa uso na lory lilokuwa limesheheni mbao.

Takriban watu wawili wamefariki papo hapo na majeruh wengi tu wamekatika viungo vyao.

Source: Mimi mwenyewe safarini Kagera

dreva na konda wamefia hospita ya mkoa singida na watu wengi 24 waliumia vibaya sana. dreva alilivaa roli lililokua limepaki barabarani. poleni wafiwa na majeruhi wote. mia
 
Basi la green star kutoka dar kwenda mwanza limepata ajari maeneo ya isuna limegonga roli kwa nyuma.inasemekana dereva wa basi kakatika miguu yote miwili na mtoto mmoja amefariki
 
basi hilo lilikua linatokea dar kwenda mwanza,dereva alikuwa anaovertake roli akakutana uso kwa uso na lory lilokuwa limesheheni mbao..takriban watu wawili wamefariki papo hapo na majeruh wengi tu wamekatika viungo vyao..source mimi mwenyewe safarin kagera

Wapi imetokea?! Poleni majeruhi, buriani mliotangulia kwenye haki.
 
huu wimbo wa ajari utakwisha lini jamani?matatizo tuliyo nayo wa tz ni ajari tosha!poleni wafiwa.
 
Poleni sana jamani. Madereva wanachoka kwa kuwa hawapumziki. Ni mpaka serikali itakapoamka na kuwabana wamiliki wa mabasi waajiri madereva wawili kwa basi moja. Na wanapaswa kufanya kama nchi za wenzetu ambapo kupumzika ni lazima kwa madereva wa longtrip. Ujiulize mtu aendeshe toka Dar hadi mwanza siku nzima na kesho huyo huyo hadi dar tena. Ni lazima achoke na akishakuwa na fatigue anakuwa na maamuzi yasiyo sahihi always. Serikali iweke points. Kila dereva akifika hapo ateremke apande mwingine na huyu abaki hapo hadi kesho yake bus likirudi na kuwe na kitu kama ticket atakayopewa huyo anayepanda. Kinachofanyika sasa ni usanii kwa kuwa bus likitoka stand ya kwanza hukaguliwa na wanachofanya wenye mabasi ni kutafuta mtu mwenye leseni anakuwa kama dereva wa pili na wakitoka stand hushuka na kurudi kufanya mambo yake. Na hii inachangiwa na kutowalipa mishahara hawa madereva. Hupewa posho tu . Ukimwambia dereva umpe mtu wa pili ina maana wagawane posho na mara nyingi atasema anaweza kwenda peke yake. Hatari.
 
Nasikia hiyo kampuni ya mabasi inamilikiwa na mheshimiwa kiongozi mkuu wa bunge la JMT.
RIP waliopoteza maisha, na Mungu awajalie majeruhi wote wapone haraka.
Poleni sana jamani. Madereva wanachoka kwa kuwa hawapumziki. Ni mpaka serikali itakapoamka na kuwabana wamiliki wa mabasi waajiri madereva wawili kwa basi moja. Na wanapaswa kufanya kama nchi za wenzetu ambapo kupumzika ni lazima kwa madereva wa longtrip. Ujiulize mtu aendeshe toka Dar hadi mwanza siku nzima na kesho huyo huyo hadi dar tena. Ni lazima achoke na akishakuwa na fatigue anakuwa na maamuzi yasiyo sahihi always. Serikali iweke points. Kila dereva akifika hapo ateremke apande mwingine na huyu abaki hapo hadi kesho yake bus likirudi na kuwe na kitu kama ticket atakayopewa huyo anayepanda. Kinachofanyika sasa ni usanii kwa kuwa bus likitoka stand ya kwanza hukaguliwa na wanachofanya wenye mabasi ni kutafuta mtu mwenye leseni anakuwa kama dereva wa pili na wakitoka stand hushuka na kurudi kufanya mambo yake. Na hii inachangiwa na kutowalipa mishahara hawa madereva. Hupewa posho tu . Ukimwambia dereva umpe mtu wa pili ina maana wagawane posho na mara nyingi atasema anaweza kwenda peke yake. Hatari.
 
Tatizo wala si kutokuwa na madreva 2,mabasi mengi cku hizi kuna madreva 2,tatizo kubwa ni wana leseni zinazotakiwa na je wamezipata kwa kuingia darasani?mi cku moja nilikuwa nasafiri,tumefika chalinze dreva akaombwa leseni akawa anayo ila haimuruhusu kuendesha basi,yake ni Class E!trafic alimuhoji kisha akamwambia haya endesha tuone naye trafiki akiwa ndani ya gari,jamaa akaendesha umbali wa kama mita 200,trafiki akamwambia nishushe, muendelee na safari!
 
Very sad indeed, kiukweli madereva hawapumziki. Na mwendo wa bus za Dar-Mwanza ni hatari mno, hususan jioni wakitoka Igunga ambapo hawana tena kuzuizi njiani mpaka wanaingia Mwanza mwendo wao huwa ni hatari. Wanakimbizana hovyo na traffics huwapungia mikono tu hasa pale Bahi na Misigiri.
 
Nawapa pole wote waliokuwemo kwenye basi. Eeh Mungu utusaidie na utusamehe maana sikuhizi kila kukicha ni ajali
 
duh sad news again,haya mabus madereva wake wako rough sana,wanakimbia speed sana
 
Tangu Kampuni hii ianze safari zake ndo Leo nasikia limepata ajari mbaya na kubwa kama hii, inawezekana kuna udhaifu umezalishwa kwa sasa kwani ni Mabasi ambayo ulikuwa ukisafiri nayo unakuwa na amani na kuisi usalama wa kutosha. Poleni mliopata Majeraha na mungu awape uvumilivu wote mliopoteza ndugu na jamaa na R.I.P wote mliotangulia mbele ya Haki nyinyi mmetangulia nasi tunafuata.
 
basi hilo lilikua linatokea Dar kwenda Kahama, dereva alikuwa anaovertake roli akakutana uso kwa uso na lory lilokuwa limesheheni mbao.

Takriban watu wawili wamefariki papo hapo na majeruh wengi tu wamekatika viungo vyao.

Source: Mimi mwenyewe safarini Kagera

Hapo kwenye red ndo pametambulisha wewe unani, coz mtu wa kabila lingine asingesema anakoelekea angeishia tu source ni yeye mwenyewe yupo safarini
 
Poleni sana wafiwa na Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Madereva jamani punguzeni mwendo na kuwa waangalifu.
 
madereva wawili ni muhim,nasafiri mara kwa mara dar to mbeya almost basi zote ninazo panda zina dereva mmoja.Kuna siku nili muuliza dereva hivi ana fight vipi usingizi?akasema ni kudra za mwenyezi mungu tu mie nika choka.serikali isipo chukua hatua madhubuti haya mabasi yata tumaliza.Pole kwa majeruhi na wafiwa
 
omba yasikukute maana yakikukuta ni kilema au kifo au kuimizwa kisaikolojia . hizi ajali ni tishio kama ukimwi
 
Back
Top Bottom