Ajali Daraja la Kinyerezi, Daraja halipitiki

Ajali Daraja la Kinyerezi, Daraja halipitiki

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,163
Reaction score
11,230
Gari kubwa la kuchanganyia Zege (concrete mixing truck) limezidi uzito daraja na kusababisha daraja kuharibika.

Ni lile daraja la Muda lililojengwa baada ya lile la kwanza kuharibika baada ya kupita gari lililozidi uzito.

Kwa sasa magari yanayotumia daraja hilo yamelazika kutumia njia mbadala.
 

Attachments

  • 1425749784382.jpg
    1425749784382.jpg
    45.7 KB · Views: 3,070
leo hiyo foleni ya barabara ya segerea itakuwa balaa na hv ni weekend duh. madereva wengine hamna kitu hawaoni hata uzito unaoruhusiwa kupita?
 
Haaa jamani si daraja jipya hili! kajenga nani kabla ya kulaumu dereva
 
Huu ni uzembe na kutokujali

Hilo daraja halijawekwa kibao kuonyesha uzito unaoruhusiwa kupita???

Dereva mwenyewe hajui amebeba uzito gani???
 
Kwa mambo vile yalivyo hapa TZ sidhani kama hapo tatizo ni uzito wa hilo gari. Tatizo letu sugu hapa TZ ni kudharau wataalam na kuendekeza wanasiasa kwasababu wanajua kubinuabinua midomo yao. Structure zote ambazo tunazo zinatakiwa kuishi kama mwanadamu anavyoishi, ziwe zinafanyiwa uchunguzi mara kwa mara kwa vipindi fulani na ripoti kuandaliwa na hivyo maintenance zitakuwa zinafanyika kwa wakati. Mfano tangu zile mvua kubwa ziliponyesha ni kipi kimefanyika kuangalia ubora wa hayo madaraja na maintenance zipi zimefanyika!, Jibu ni hakuna ni siasa tu. Mtakuja kumuonea bure mwenye hilo lori.
 
Huyo Dereva pmbavu kabisa. Haoni alama zote zilizopo pale! Alipe haraka na afungwe kwa malicious destruction of public infrastructure.
 
Huyo Dereva pmbavu kabisa. Haoni alama zote zilizopo pale! Alipe haraka na afungwe kwa malicious destruction of public infrastructure.

Najiuliza, hawa madereva wa magari makubwa wanazo kichwani au? Kuna signs pale za uzito unaoruhusiwa, na pia hilo daraja lilivunjwa juzi juzi na lori lingine tena lililozidisha mzigo, wanashindwa hata kujifunza kutokana na uzembe wa madereva wenzao? Pia alishindwa pita kule chini wanakopita wenzake wenye uzito uliozidi?? Huyu achinjwe! Yule mwingine sijui alifanywa nini!
 
Huyo Dereva pmbavu kabisa. Haoni alama zote zilizopo pale! Alipe haraka na afungwe kwa malicious destruction of public infrastructure.

Inashangaza. Alama zipo za max. tonnage kwa kipindi hiki wakati daraja la kudumu lipo kwenye ujenzi. Akili ya kawaida ilipasa tu huyo dereva kuona gari analoendesha ni kubwa kuliko uwezo wa daraja temporary!
 
Huu ni uzembe na kutokujali

Hilo daraja halijawekwa kibao kuonyesha uzito unaoruhusiwa kupita???

Dereva mwenyewe hajui amebeba uzito gani???


Nimepita sana kwenye hilo daraja kwa siku za karibuni. Kuna vibao vya kuonesha uzito unaoruhusiwa. Na mara zote magari yenye uzito kama hilo lililovunja daraja yamekuwa yakipita bondeni mwa daraja.
 
Kwa mambo vile yalivyo hapa TZ sidhani kama hapo tatizo ni uzito wa hilo gari. Tatizo letu sugu hapa TZ ni kudharau wataalam na kuendekeza wanasiasa kwasababu wanajua kubinuabinua midomo yao. Structure zote ambazo tunazo zinatakiwa kuishi kama mwanadamu anavyoishi, ziwe zinafanyiwa uchunguzi mara kwa mara kwa vipindi fulani na ripoti kuandaliwa na hivyo maintenance zitakuwa zinafanyika kwa wakati. Mfano tangu zile mvua kubwa ziliponyesha ni kipi kimefanyika kuangalia ubora wa hayo madaraja na maintenance zipi zimefanyika!, Jibu ni hakuna ni siasa tu. Mtakuja kumuonea bure mwenye hilo lori.

Hilo daraja la muda.
 
Kwa mambo vile yalivyo hapa TZ sidhani kama hapo tatizo ni uzito wa hilo gari. Tatizo letu sugu hapa TZ ni kudharau wataalam na kuendekeza wanasiasa kwasababu wanajua kubinuabinua midomo yao. Structure zote ambazo tunazo zinatakiwa kuishi kama mwanadamu anavyoishi, ziwe zinafanyiwa uchunguzi mara kwa mara kwa vipindi fulani na ripoti kuandaliwa na hivyo maintenance zitakuwa zinafanyika kwa wakati. Mfano tangu zile mvua kubwa ziliponyesha ni kipi kimefanyika kuangalia ubora wa hayo madaraja na maintenance zipi zimefanyika!, Jibu ni hakuna ni siasa tu. Mtakuja kumuonea bure mwenye hilo lori.

Tuongelee daraja la kinyerezi:
Wee unakaa wapi nchi hii? Unalijua hilo daraja? Unajua pembeni yake kuna nini kinaendelea?? Unajua historia yake japo ni fupi ya hili daraja ambalo mleta mada anasema halipitiki? Umezoom hiyo picha inayoonekana?
Yawezekana uko sahihi kidogo, ila asilimia kubwa ya hawa madereva wa malori naona ni madereva tu sababu wanajua kufanya chombo cha moto kitoke point moja kwenda nyingine, ila kichwani wengi nina mashaka nao!
 
Back
Top Bottom