Ajali basi la majinja

Ajali basi la majinja

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
1,683
Reaction score
2,157
Kumetokea ajali ya basi la majinja lililokuwa linatoka Mbeya kwenda Dar. Sababu ya ajali ni mwendo kasi wa basi la majinja ambalo lilitaka kulipita gari lingine ambapo walikutana na lori upande wa pili na kumlazimisha dereva kulipeleka gari porini kuepusha kugongana uso kwa uso na hivyo, basi kupinduka vibaya sana. Hakuna vifo mpaka sasa ila majeruhi zaidi ya 28 wamepelekwa hospitali ya Morogoro. Majeruhi zaid wanaendelea kupokelewa. Dereva wa basi amekimbia. Ajali imetokea morogoro mjini eneo la nane nane.

Chanzo. Radio one stereo breaking news.

Ajali imetokea maeneo ya FRANSALIAN barabara kuu ya dsm, ajali imetokea baada ya basi hilo kugongana na lori lililokuwa likitokea dsm. Kwa mujibu wa majeruhi wa ajali hiyo, ajali imetokea pale dereva wa basi alipotaka kulipita gari la mbele huku akiwa mwendo kasi. Kwa mujibu wa majeruhi na mashuhuda wengine hakuna aliyepoteza maisha na dereva wa basi hilo amekimbia.
 
Kumetokea ajali ya basi la majinja lililokuwa linatoka Mbeya kwenda Dar. Sababu ya ajali ni mwendo kasi wa basi la majinja ambalo lilitaka kulipita gari lingine ambapo walikutana na lori upande wa pili na kumlazimisha dereva kulipeleka gari porini kuepusha kugongana uso kwa uso na hivyo, basi kupinduka vibaya sana. Hakuna vifo mpaka sasa ila majeruhi zaidi ya 28 wamepelekwa hospitali ya Morogoro. Majeruhi zaid wanaendelea kupokelewa. Dereva wa basi amekimbia. Ajali imetokea morogoro mjini eneo la nane nane. Chanzo. Radio one stereo breakingnews.
 
gari linaitwa majinjah...linafanya safari za dar -mbeya!lilikua linatoka mbeya kwenda dar!hakuna mtu aliyepoteza maisha
 
Poleni majeruhi. Ila mm nawachukia madreva zetu wao ndio chanzo cha ajali

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Poleni majeruhi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Bora kama dereva wa basi kavunjika miguu na kiuno.
 
Nalifahamu sana hilo bus nisha wahi kupanda kutoka Mby hadi Dar tulitoka saa 12 tukaingia Dar saa 10:45. Wakati mengine yanaingiaga Dar Saa 1. Lina mwendo mpela mpela sana.
Pole Majeruhi.
 
poleni sana Mwenyenzi Mungu awape nguvu na mpone harakara. dereve kuweni mkini mnapokuwa barabarani tafadhali sana.
 
Nalifahamu sana hilo bus nisha wahi kupanda kutoka Mby hadi Dar tulitoka saa 12 tukaingia Dar saa 10:45. Wakati mengine yanaingiaga Dar Saa 1. Lina mwendo mpela mpela sana.
Pole Majeruhi.

Kwa safari za Mby hawa jamaa Majinja hawafai hata kidogo, siharibu biashara za watu, lakini tusiposema kabla ya ajali,haina maana kusema tukiwa majeruhi.
 
Back
Top Bottom