Habari za leo wana forums!
Kwanza nianze kwa kusema sisi ambao kula yetu inategemea internet tumekuwa wahanga Sana wa unyonyaji unaofanywa na mitandao ya simu , binafsi nitajikita kwenye mtandao wa Airtel maana ndo nilikoshuhudia kwa macho yangu na ushahidi ninao
Mchezo ulikuwa hivi ;
Baada ya kuona kila siku natumia bando la 4000 kwenye upande wa Internet tu ikanibidi nianze kufanya uchunguzi mdogo ili nijue ni kwanini natumia bundle kiasi hicho?
Airtel Wana bundle lao la UNI OFA ambalo ukijiunga unapata gb 2 kwa 2000 utumie siku tatu hivyo Mimi kila siku natumia GB 4 kwa madai ya Airtel, maana kila siku naunga bundle mara mbili la sh 2000 kupitia Airtel money, Sasa Jana mchana mida ya saa sita baada ya kupokea sms yao ile ya bundle lako limefikia asilimia 90%
Nikajirushia hela kutoka tigo pesa kuja Airtel money Kama ilivyo kawaida yangu ili nijiunge gb 2 Tena ,kweli nikarusha na pesa ukaingia ikiwa inasoma balance ya sh.2020.96 nikajiunga bando la internet la Gb 2 nikatumiwa na sms kuwa umepokea gb 2 za kutumia kwa siku tatu ,aisee Cha kushangaza ndani ya dakika kumi na tano natumiwa sms umetumia bundle lako kwa asilimia 90% nikatulia Tena Kama dak.10 nikatumiwa sms nyingine umetumia bundle lako kwa asilimia 100% ikiwa na maana bando limeisha ndani ya nusu saa la gb2 ,na hapo sijafungua hata WhatsApp Wala browser yoyote, nilichofanya nikawapigia simu mara ya kwanza akadai hujanunua bando nikamuuliza mbona hela mmekata kwenye airtelmoney Sasa mmekata ya nini na kwa Nini mmenitumia sms kuwa nimepewa gb2 then ndani ya nusu saa mmetuma sms nimetumia kwa asilimia 100, akajibu kuwa inaonyesha ndio umenunua bundle kwa Airtel money Ila kwako hakijaingizwa! Hivyo subiri ndani ya masaa 24 tutatatua nikasema poa ,baada ya masaa 24 nikawapigia wakasema ndani ya masaa 3 itakuwa tayari kitu ikapita Sasa nikawa nikiwapigia simu nikiwaeleza Hilo swala wananikatia simu na nimepiga mara nyingi wanaendelea kukata ,Sasa kinachonishangaza Hilo jambo hata Leo limejirudia Tena na nikipiga simu wanakata bila kunipa majibu yoyote
Sasa kwa mtu anayeweza kunushauri nifanyaje? Wajamaa wamekata hela nyingi mno Jana na Leo ndo nimewabaini huo mchezo kuwa kumbe wananikata pesa Airtelmoney na bando sipewi je huu sio wizi? Na Kuna voice record nyingine ninazo! So Nina uhakika na ninachoongea