Airtel ni wezi na hii nina ushahidi na mahali popote nipo tayari kutoa ushahidi

Same to me,yani ulivyoeleza hivyo hivyo.Nilijiunga bundle ya buku 1GB ndan ya dk10 wananiaambia bundle 90% limetumika.Nikawapigia wakanijibu bado sijatumiwa.Ndo nitoleee mpaka leo.

Wezi Sana hao
 
Nakubali

Nakubaliana na wewe,juzi tu voda nimetoka kutukana ,na nikawaambia wanirekodi siogopi chochote ,ushahidi Niko nao hata mahakamani nitawapeleka

Lakini Vodacom wanajitahidi sana. Kuwasaidia ni kuimarisha upande wa customer service tu ili watu wao wawe professionals badala ya kuwa na watu wanaosema "sio sisi ni system".
 
Same to me,yani ulivyoeleza hivyo hivyo.Nilijiunga bundle ya buku 1GB ndan ya dk10 wananiaambia bundle 90% limetumika.Nikawapigia wakanijibu bado sijatumiwa.Ndo nitoleee mpaka leo.

Wezi Sana hao
Airtel ni JANGA kwa watumiaji wa mitandao ya mawasiliano. It is the worst of all
 
Habari za leo wana forums!
Kwanza nianze kwa kusema sisi ambao kula yetu inategemea internet tumekuwa wahanga Sana wa unyonyaji unaofanywa na mitandao ya simu , binafsi nitajikita kwenye mtandao wa Airtel maana ndo nilikoshuhudia kwa macho yangu na ushahidi ninao

Mchezo ulikuwa hivi ;
Baada ya kuona kila siku natumia bando la 4000 kwenye upande wa Internet tu ikanibidi nianze kufanya uchunguzi mdogo ili nijue ni kwanini natumia bundle kiasi hicho?

Airtel Wana bundle lao la UNI OFA ambalo ukijiunga unapata gb 2 kwa 2000 utumie siku tatu hivyo Mimi kila siku natumia GB 4 kwa madai ya Airtel, maana kila siku naunga bundle mara mbili la sh 2000 kupitia Airtel money, Sasa Jana mchana mida ya saa sita baada ya kupokea sms yao ile ya bundle lako limefikia asilimia 90%
Nikajirushia hela kutoka tigo pesa kuja Airtel money Kama ilivyo kawaida yangu ili nijiunge gb 2 Tena ,kweli nikarusha na pesa ukaingia ikiwa inasoma balance ya sh.2020.96 nikajiunga bando la internet la Gb 2 nikatumiwa na sms kuwa umepokea gb 2 za kutumia kwa siku tatu ,aisee Cha kushangaza ndani ya dakika kumi na tano natumiwa sms umetumia bundle lako kwa asilimia 90% nikatulia Tena Kama dak.10 nikatumiwa sms nyingine umetumia bundle lako kwa asilimia 100% ikiwa na maana bando limeisha ndani ya nusu saa la gb2 ,na hapo sijafungua hata WhatsApp Wala browser yoyote, nilichofanya nikawapigia simu mara ya kwanza akadai hujanunua bando nikamuuliza mbona hela mmekata kwenye airtelmoney Sasa mmekata ya nini na kwa Nini mmenitumia sms kuwa nimepewa gb2 then ndani ya nusu saa mmetuma sms nimetumia kwa asilimia 100, akajibu kuwa inaonyesha ndio umenunua bundle kwa Airtel money Ila kwako hakijaingizwa! Hivyo subiri ndani ya masaa 24 tutatatua nikasema poa ,baada ya masaa 24 nikawapigia wakasema ndani ya masaa 3 itakuwa tayari kitu ikapita Sasa nikawa nikiwapigia simu nikiwaeleza Hilo swala wananikatia simu na nimepiga mara nyingi wanaendelea kukata ,Sasa kinachonishangaza Hilo jambo hata Leo limejirudia Tena na nikipiga simu wanakata bila kunipa majibu yoyote


Sasa kwa mtu anayeweza kunushauri nifanyaje? Wajamaa wamekata hela nyingi mno Jana na Leo ndo nimewabaini huo mchezo kuwa kumbe wananikata pesa Airtelmoney na bando sipewi je huu sio wizi? Na Kuna voice record nyingine ninazo! So Nina uhakika na ninachoongea
Kwanza, ni apps gani zenye MB zaidi ya 200 halafu unaweka zaidi ya kumi kwenye simu yako? Tupe mfano hai usiongee kwa kuassume.
Pili, hizo Zuku, CatsNet na Raha hazipatikani kila sehemu. Coverage yake sio sawa na hii mitandao ya simu ambayo ipo almost nchi nzima.
Tatu, hata huko ni gharama pia kwa sisi watu wa chini. Mfano utakuta unapewa 10Mb/s na kwa mwezi ni 120,000/= sawa ni unlimited but mtu anayelalamika elf 2 yake kupotea unadhani ni rahisi kutoa laki kila mwezi kwa ajili ya internet? Bado gharama za kufunga hiyo internet(radio, access point, router, etc) japo wengine wanafanya ukilipia miezi mitatu wanafunga bure.

Halafu jifunze kuandika.
#garama -#gharama
#cat net -#Cats Net
#raha dot come -#raha.com (Liquid Telecom)
Inaonekana wewe ni mfanyakazi wa airtel,umekuja kutetea wezi wenzio.Nenda kawaambie wananchi tumeanza kuwastukia
 
AIRTEL kwa kwl ni wezi bila kupepesa macho
Mimi nilishanunuaga bundle kupitia airtel money, halaf cha kushangaza sikupew mb ila pesa wakakata, wakasema ndani ya masaa 24 nitapewa MB zangu..lakin mpaka leo ni zaid ya miez 2..
 
Kwanza, ni apps gani zenye MB zaidi ya 200 halafu unaweka zaidi ya kumi kwenye simu yako? Tupe mfano hai usiongee kwa kuassume.
Pili, hizo Zuku, CatsNet na Raha hazipatikani kila sehemu. Coverage yake sio sawa na hii mitandao ya simu ambayo ipo almost nchi nzima.
Tatu, hata huko ni gharama pia kwa sisi watu wa chini. Mfano utakuta unapewa 10Mb/s na kwa mwezi ni 120,000/= sawa ni unlimited but mtu anayelalamika elf 2 yake kupotea unadhani ni rahisi kutoa laki kila mwezi kwa ajili ya internet? Bado gharama za kufunga hiyo internet(radio, access point, router, etc) japo wengine wanafanya ukilipia miezi mitatu wanafunga bure.

Halafu jifunze kuandika.
#garama -#gharama
#cat net -#Cats Net
#raha dot come -#raha.com (Liquid Telecom)

IMG_0051.png

Jifunze kuwa muelewa sio taaluma yako unataka kujua
 
Hii iPhone ngapy mkuu

Kuna mambo mengine watu ucomment bila kujua.mifumo ya app kisa siku inaboreshwa na uwezo mkubwa mpaka utaka kiwango kikubwa cha speed ya internet,kama app zenye mfumo mkubwa ni ngumu kukaa bila kupakua data.ukiwa na app zaidi ya 20 na zote zipo active kwenye data unategemea nini.

Elimu ya teknolojia sio elimu ya siasa.
 
Airtel ni wezi kila upande juzijuzi nilihamisha pesa toka Airtel money kwenda Tpesa zote line zangu pesa ikakatwa ujumbe ukafika na salio likapunguzwa lakini pesa haikufika tpesa, nikatuma mara ya pili mchezo huohuo lakini nilipotuma mara yla tatu pesa iklfika lakini zile za mwanzoni pamoja na kuzikata hazikufika.
Niliwapigia customer care airtel money wakasema system yao inaonyesha pesa imekwenda, nikawapigia ttcl wakasema pesa haijaingia niongee na airtel money kama vipi warudishe kwenye simu yangulakini nilipowapigia airtel money walikataa na kuniambia pesa imekwenda.
Niliwapigia tcra wakanilambia nitume malalamiko kwa email.
Nilipotuma malalamiko ttcl walinipigia baadla yla kuongea nao wakaniambia airtel money watarudisha pesa zangu baadae ndio Airtel wakarudisha cha kujiuliza ina maana system zipo kwa ajili ya kudhulumu wateja na sio wao kupoteza pesa
 
HAWA AIRTEL WAMEOTA MAPEMBE DAWA NI SISI WATZ TUUGANE NA KUGOMA KUTUMIA AIRTEL
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom