Airtel na Vodacom acheni wizi wa Megabytes (MB)

Airtel na Vodacom acheni wizi wa Megabytes (MB)

Jaji matundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2014
Posts
251
Reaction score
92
Kwa mfano airtel yatosha kuna kifurushi kimoja nimejiunga nacho jana usiku cha airtel kwenda airtel nikapewa mb 100 pamoja na dakika na sms lakini nikashangaa nilipo download kitu kimoja cha mb saba nikashangaa mb zote 100 zikawa ziimekwisha hali hiyo imekua ikijirudia rudia mara kadhaa hasa upande wa mb ndipo usiku huohuo nikaamua kuwa tolea uvivu kuwauliza kwanini kifurushi kinawahi kuisha ukilinganisha na matumizi wakanijibu nizime simu na kuwasha dhen nitarudishiwa MB zangu cha kushangaza nilipo zima simu nikawasha nikaangalia mb walizoniambia sikuona kitu nikamuua niwapigie tena wale castomer care wakaacha wakapokea lakini hawaongei nikawa namsikia dada mmoja akichati na kwa kuangalia walikua wanatongozana kutokana na nakauli za mahaba nilizo kuwa nazisikia yule dada alipogundua nawasikia akanikatia simu nikajarikupiga tena mara mbili lakini mara zote nikaambiwa ili kuongea na mtoa huduma nikubali kutozwa sh 60 kutoka kwenye akaunt yangu

kwa upande wa voda wameshusha mb za vodacom-vodacom kutoka mb 100 mpaka 50 mb bila taarifa ya mabadiliko hayo kwa wateja wao

pia wanamapungufu mengine ukiacha hayo ya kushusha mb wana mtindo wa kunyonya mb nyingi ukilinganisha na mtumizi mfano juzi nilijiunga na kifurushi cha voda-voda nilidownload camera 360 pekeyake lakin mb zote 50 zikawa zimekwisha this is not fare

nimeandika hapa ili kuwalaani AIRTEL na VODA na kama wewe umekua on the same road kama mimi tuungane ili kutokomeza wizi huu.

TCRA kama bado hajahongwa mtuokoe na majangili hawa tunajua ni kweli wanatafuta faida lakini kwanini wanatuongezea umasikini?
 
mkuu hali ni mbaya sana nchi hii, hakuna utawala wa sheria? ndiyo maana watu wanachukua pesa kwa lumbesa bila kuhojiwa, sembuse kuiba mb ni janga
 
Inawezekana kama unatumia computer kuna automatic updates ambazo huwa zinadownload bejind the scenes so before u conclude jaribu kucheck hilo na issue ya antivirus updates pia.
 
Vodacom wanafanya wizi sana. Yaani kuna wakati unakifurushi kinataka kwisha na una pesa kwenye simu. Kwa kujihami unataka kuongeza kifurushi, wanakwambia usubiri mpaka cha kwanza kiishe. Unapiga simu au kuangalia video mitandaoni, hawakwambii kama kimeisha wanaanza kukwangua ile hela yako kwenye simu. Huu ni ujambazi...
 
mkuu Nico mimi situmii computer natumia cm naona tatizo ni wizi sio kifaa
 
Nilifikiri wananionea peke yangu kumbe ndio kamtindo kao,sitasahau siku walipo niambia kuwa kifurushi chako kimekwisha huku nikiwa bado nina dakika kama 34,mb 165 na sms nyingi tu na muda wa kuisha ulikuwa bado,iliniuma sana
 
Back
Top Bottom