Aina ya samaki bahari ya hindi

Aina ya samaki bahari ya hindi

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,837
Wakuu,

Nahitaji kufahamu aina ya samaki wanaopatikana bahari ya hindi, ambao nikienda Ferry nina uhakika nitapawapata kwa wingi.

Msaada wakuu
 
Wasiliana na Magu anajua idadi ya samaki walioko baharini na ziwani na hata kwa majina pia atakutajia.
 
Wakuu,

Nahitaji kufahamu aina ya samaki wanaopatikana bahari ya hindi, ambao nikienda Ferry nina uhakika nitapawapata kwa wingi.

Msaada wakuu
Daaah nimesahau kidogo, kulikuwa na jamaa mmoja amewahi kuwa mkuu wa uvuvi TZ kitambo, yaani alikuwa anawajua samaki wote wa vidimbwi, mabwawa, mito, maziwa na bahari za TZ kwa majina, idadi, umri na idadi ya mayai yao.
 
Muulize mjomba magu hata ukitaka ujue koo zao utapata details
 
Samaki waliopo kwenye soko ni Changu,Kibua,Numbi,Bangara,Jodari,
 
Kama mfuko mzuri
piga1. kole kole .(jipange)
2.changu na changu doa(jipange)
3.Tasi na tasi mwamba.
4.Nguru(jipange)
5.Panje
6.Taa aina zote japo wengi sio watamu.
7.Mkundaji
8.Kikande.
9.Kuku bahari.
10.Vibua.
11.Saladin
12.Jodari(jipange)
13Pweza(jipange)
14Ngisi hasa ngisi gome(jipange)
15.Baracuda -Nzia
16.Sehewa -kwa pilau hawa!
17.Chuchunge
18.Vipepeo.
19.Nyenga(jamii ya taa wadogo wenye mikia ya sumu)
20.Bunju mtamu but be careful so poisonous ukimkosea imekula kwako
21.Bunju miba-bolingo huyu hana noma unamlampaka matako yake
22.Saleh -samaki mmoja mtamu sana
23.Mboo ya mvuvi au wahindi wanamwita bumla mtamu sana ila sura yake unaweza kutishia watoto
Ukitaka zaidi nisuv8ri nikimaliza kula daku saa 10 alfajr
 
Kama mfuko mzuri
piga1. kole kole .(jipange)
2.changu na changu doa(jipange)
3.Tasi na tasi mwamba.
4.Nguru(jipange)
5.Panje
6.Taa aina zote japo wengi sio watamu.
7.Mkundaji
8.Kikande.
9.Kuku bahari.
10.Vibua.
11.Saladin
12.Jodari(jipange)
13Pweza(jipange)
14Ngisi hasa ngisi gome(jipange)
15.Baracuda -Nzia
16.Sehewa -kwa pilau hawa!
17.Chuchunge
18.Vipepeo.
19.Nyenga(jamii ya taa wadogo wenye mikia ya sumu)
20.Bunju mtamu but be careful so poisonous ukimkosea imekula kwako
21.Bunju miba-bolingo huyu hana noma unamlampaka matako yake
22.Saleh -samaki mmoja mtamu sana
23.Mboo ya mvuvi au wahindi wanamwita bumla mtamu sana ila sura yake unaweza kutishia watoto
Ukitaka zaidi nisuv8ri nikimaliza kula daku saa 10 alfajr

mkuu vibua wanauzaje hapo ferry.. kwa kg au idadi ya samaki? na ni pesa ngapi?
 
Siko ferry mkuu ila mtu wa pwani najua samaki asilimia 90
Huyu samaki anaitwaje?
20220421_201728.jpg
 
Back
Top Bottom