Aina nyingine ya kusherehekea siku yako ya kuzaliwa

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Wakuu,

Leo katika pitapita yangu mitaa fulani nimewakuta jamaa kama wanne hivi wakimmwagia maji machafu mdada huku kicheko kikiendelea. Nilisistuka na kuhoji kulikoni maana nilidhani mdada kawatendea jambo baya hao jamaa hivo wakaamua kumwadhibu kwa kummwagia maji machafu toka barabarani, jibu nililipewa ninilifanya niishiwe mbavu kwa kucheka.

Eti leo ni siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa huyo mdada hivo walikuwa wakimrejesha enzi ya utoto kwa kuchafuka kama watoto wanavochafuka kwa michezo yao. Nikatafakari mtindo huu na kuanza kujiuliza labda ni utakata wa kuandaa mambo ya keki na vinywaji ndo kumewafanya kuonesha aina hii ya sherehe (birthday) barabarani.

Dunia ina wabunifu wengi.
 
Wakuu, leo katika pitapita yangu mitaa fulani nimewakuta jamaa kama wanne hivi wakimmwagia maji machafu mdada huku kicheko kikiendelea. Nilisikuka na kuhoji kulikoni maana ninidhani mdada kawatendea jambo baya hao jamaa hivo wakaamua kumwadhibu kwa kummwagia maji machafu toka barabarani, jibu nililipewa ninilifanya niishiwe mbavu kwa kucheka.
Eti leo ni siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa huyo mdada hivo walikuwa wakimrejesha enzi ya utoto kwa kuchafuka kama watoto wanavochafuka kwa michezo yao. Nikatafakari mtindo huu na kuanza kujiuliza labda ni utakata wa kuandaa mambo ya keki na vinywaji ndo kumewafanya kuonesha aina hii ya sherehe (birthday) barabarani.
Dunia ina wabunifu wengi.
Mkuu nomeshuhudia hata kwenye sherehe ya harusi bwana harusi anachafuliwa kwa dizel chafu na rafikizake ambao hawajaoa ati adgabu ya kutoroka chama cha ukapera
 
Mkuu nomeshuhudia hata kwenye sherehe ya harusi bwana harusi anachafuliwa kwa dizel chafu na rafikizake ambao hawajaoa ati adgabu ya kutoroka chama cha ukapera
Diesel!!!!!!!!!? Hiyo hatari mbona?
 
Wakuu,

Leo katika pitapita yangu mitaa fulani nimewakuta jamaa kama wanne hivi wakimmwagia maji machafu mdada huku kicheko kikiendelea. Nilisistuka na kuhoji kulikoni maana nilidhani mdada kawatendea jambo baya hao jamaa hivo wakaamua kumwadhibu kwa kummwagia maji machafu toka barabarani, jibu nililipewa ninilifanya niishiwe mbavu kwa kucheka.

Eti leo ni siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa huyo mdada hivo walikuwa wakimrejesha enzi ya utoto kwa kuchafuka kama watoto wanavochafuka kwa michezo yao. Nikatafakari mtindo huu na kuanza kujiuliza labda ni utakata wa kuandaa mambo ya keki na vinywaji ndo kumewafanya kuonesha aina hii ya sherehe (birthday) barabarani.

Dunia ina wabunifu wengi.


Uswahilini kuna mbinu nyingi sana mkuu. Mimi mwaka jana siku ya birthday yangu walikuja wadada (2) kunipikia na kuniogesha pia na kunilaza huku wakinibembeleza kama vile mtoto. Nikaomba kitumbua wakaniambia wewe ndiyo kwanza umezaliwa leo hata kubalehe bado, unataka kujiumiza ili iweje? Sie tumekuja kukusaidia tu leo hii, kesho ukisha balehe utakuwa huru kufanya uyatakayo. Mpaka leo nikiyakumbuka haya maneno nacheka sana na kuwashangaa wadada wa mjini.
 
Uswahilini kuna mbinu nyingi sana mkuu. Mimi mwaka jana siku ya birthday yangu walikuja wadada (2) kunipikia na kuniogesha pia na kunilaza huku wakinibembeleza kama vile mtoto. Nikaomba kitumbua wakaniambia wewe ndiyo kwanza umezaliwa leo hata kubalehe bado, unataka kujiumiza ili iweje? Sie tumekuja kukusaidia tu leo hii, kesho ukisha balehe utakuwa huru kufanya uyatakayo. Mpaka leo nikiyakumbuka haya maneno nacheka sana na kuwashangaa wadada wa mjini.
Oh mkuu, kesho yake ikawaje? Nimenogewa mkuu.
 
Kesho yake wala sikuwa na hamu ya ku-do demu wowote....ila ninawajibika kufurahisha mwili na kuondoa stress.
Dah, ningekuwa mie ningefuatilia kutimiza ahadi waliyoitoa. Bahati kama hizi wengine hatuzipati!!!!
 
Kuna zile clips za vichekesho,yule dada anayeongea kwa rafudhi ya kihaya"Njoo unimwagie" au "njoo uniroge"....Uswazi bhana
 
Back
Top Bottom