Abraham Lincolnn
JF-Expert Member
- Apr 12, 2018
- 2,510
- 4,217
Wakuu nisipende kuwachosha
Ila inasikitisha sana kuona ikulu ambapo Nyerere aliwahi kusema kuwa ni mahala patakatifu imebadilika na kuwa pango la walanguzi.
Leo ikulu hapafanyiki tena mikutano ya kujadili mikataba ya madini,utiaji saini miradi ya maendeleo n.k Bali imekuwa sehemu ya kufanya karamu kuonana na viongozi wastaafu kupongezana n.k
Kiongozi mkuu wa nchi amekuwa mwepesi kuhudhuri shughuli nyepesi nyepesi zisizokuwa na tija kubwa kwa taifa huku akiacha hoja za msingi na miradi ya msingi ya kimaendeleo hususan kwa nchi yetu masikini ambayo bado hali ya uchumi si nzuri na changamoto ni nyingi mno kwa wananchi ambao wamepigwa na maisha hata hawakumbuki siku zao za kuzaliwa.
Kiongozi mkuu wa nchi amebaki kufanya makongamano,teuzi,birthday party n.k huku akisahau kuna miradi ya kimkakati kama JNHP, SGR pia anapaswa kubrainnstorm kuja na miradi mingi ili uchumi ukue watanzania waondokane na umasikini unaowatesa miaka nenda rudi.Sijakataa mtu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku moja kati ya 365 lakini vipi masikini wanaoteseka siku zote 365 huku yule waliyemtuma wakitegemea atawaondolea umasikini akiponda raha (kiujumla maisha ya Rais kwa mshahara wake ni bonus tosha kwa siku zote 365 ukilinganisha na watanzania wengi ) lakini bado pia kabla hajatimiza azma za waliomtuma tayari anafanya karamu tena hali ya kuwa wale waliomtuma hawakumbuki hata siku zao za kuzaliwa kwa tabu na masumbuko ya umasikini wanaoupitia!
Wakuu nina mengi moyoni ila hasira zimenikaba kwenye koo mpaka nashindwa kuendelea. Naomba niishie hapa kwa Leo .
Ila inasikitisha sana kuona ikulu ambapo Nyerere aliwahi kusema kuwa ni mahala patakatifu imebadilika na kuwa pango la walanguzi.
Leo ikulu hapafanyiki tena mikutano ya kujadili mikataba ya madini,utiaji saini miradi ya maendeleo n.k Bali imekuwa sehemu ya kufanya karamu kuonana na viongozi wastaafu kupongezana n.k
Kiongozi mkuu wa nchi amekuwa mwepesi kuhudhuri shughuli nyepesi nyepesi zisizokuwa na tija kubwa kwa taifa huku akiacha hoja za msingi na miradi ya msingi ya kimaendeleo hususan kwa nchi yetu masikini ambayo bado hali ya uchumi si nzuri na changamoto ni nyingi mno kwa wananchi ambao wamepigwa na maisha hata hawakumbuki siku zao za kuzaliwa.
Kiongozi mkuu wa nchi amebaki kufanya makongamano,teuzi,birthday party n.k huku akisahau kuna miradi ya kimkakati kama JNHP, SGR pia anapaswa kubrainnstorm kuja na miradi mingi ili uchumi ukue watanzania waondokane na umasikini unaowatesa miaka nenda rudi.Sijakataa mtu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku moja kati ya 365 lakini vipi masikini wanaoteseka siku zote 365 huku yule waliyemtuma wakitegemea atawaondolea umasikini akiponda raha (kiujumla maisha ya Rais kwa mshahara wake ni bonus tosha kwa siku zote 365 ukilinganisha na watanzania wengi ) lakini bado pia kabla hajatimiza azma za waliomtuma tayari anafanya karamu tena hali ya kuwa wale waliomtuma hawakumbuki hata siku zao za kuzaliwa kwa tabu na masumbuko ya umasikini wanaoupitia!
Wakuu nina mengi moyoni ila hasira zimenikaba kwenye koo mpaka nashindwa kuendelea. Naomba niishie hapa kwa Leo .