Aili Mali Tripp mwandishi wa kitabu cha Joan Wicken

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,265
Nimefika Chuo Kikuu Cha Iowa, Iowa City nyakati za mchana nikitokea Detroit ambako ndiko nilikoingia Marekani nikitokea Amsterdam.

Kutoka Detroit nimepanda ndege ndogo hadi Iowa City na hapo nikachukua taxi hadi University of Iowa.

Nimepewa mwaliko na Prof. James Giblin.

Chuo kina hoteli yake ya kufikia wageni.

Muda si muda simu ya chumbani kwangu inalia.
Prof. Giblin huyo.

Anasema Kiswahili utadhani kazaliwa Kariakoo.

"Mzee wa Tanga nasikia umewasili nitakuja kukuchukua jioni uje nyumbani tule."

Prof. Giblin mkewe Mtanzania.

Dada yangu kafurahi kuniona kwake na yeye pia anasomesha.

Stori zikawa za Dar es Salaam Kariakoo yake na Bi. Kidude na taarab ya Zanzibar.

Wamarekani wanapojifunza somo mfano lugha ya Kiswahili hawaingii nusu nusu utashangaa.

Wanaingia kusoma kila kitu hadi muziki na utamaduni.

Nimepigwa na butwaa nilipokuwa hapo chuoni wale wenye kusema Kiswahili hawazungumzi na mimi ila kwa Kiswahili na kuniuliza mengi ya sehemu wanazozijua Tanzania.

Chuo Kikuu Cha Iowa Idara ya African History imeandaa kongamano kuhusu historia ya Afrika na wataalamu wengi wamealikwa.

Baadhi ya waalikwa tunafahamiana tumeonana Tanzania miaka ya nyuma kama Jonathon Glassman na James Brennan.

Hawa ni mtu na mwanafunzi wake.

James Brennan kapiga goti kwa Jonathon Glassman kusoma shahada ya uzamivu na ndiye aliyemwagiza aje kuzungumza na mimi Tanga wakati wa utafiti wake.

Ilikuwa hapo University of Iowa ndipo nilipokutana na Aili Tripp.

Alinikabili na kunieleza kuwa alikuwa na hamu kubwa ya kuzungumza na mimi kwani yeye baba yake alikuwa akisomesha Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam na akijuana na Ally Sykes akienda kumtembelea kwake Mbezi Beach.

Akaniambia yeye kasoma Bunge Primary School darasa moja na Mariam Abdul Sykes.

"How's she doing?"
Hili sikulitegemea.

"Mariam passed away many years back."

Leo nilitoka nyumbani.

Niliporudi nikakuta juu ya laptop yangu kitabu hicho hapo chini alichoandika Aili Mali Tripp.

Kitabu hiki kaniletea Zitto Kabwe.
Hakika dunia ni ndogo sana.

Nikiwa University of Iowa nikakutana na Prof. Michael Lofchie mwandishi wa kitabu: "Backgroud to Revolution," (1965).

Prof. Lofchie akaniambia kuwa yeye na Ally Sykes walikuwa marafiki wakubwa sana wakati alipokuwa Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Akaniambia kuwa alikuwa na hamu ya kukutana na mimi aliposikia kuwa nakuja kwenye kongamano na nitazungumza.

Ndugu yangu chukua tahadhari ukisikia msomi wa Kimarekani ana hamu na wewe jitayarishe kwani hakutafuti mpige soga.

Huyo kakusoma yako anayotaka kuyajua kutoka kwako kwa ushahidi.
Nililijua hili baadae.

Nilimfikishia Ally Sykes salamu zake kutoka kwa rafiki zake Marekani ambao miaka mingi hawajaonana.
Kitabu cha Aili Mari Tripp kimenikumbusha mengi.

Picha hiyo ya watu wengi Aili Tripp kasimama nyuma kushotoni kwangu na picha ya tatu ni Prof. Michael Lofchie.

Picha ya tatu ni James Brennan na ya nne ni James Giblin akiwa ofisini kwake akionyesha kitabu cha Abdul Sykes.

NB:
"Unakumbuka mambo vizuri.

Niliishi karibu na Mariamu Sykes pale Mbezi tukiwa watoto na tulikuwa marafiki.
Nasikitika kusikia kwamba alikufa.

Nitavutiwa kujua maoni yako kuhusu kitabu kuhusu Joan Wicken na Mwalimu Nyerere."
Aili Trip.

1694806505132.png

1694806334997.png

1694806440148.png

1694806466931.png
 
Atakuwa nduguye Linda Tripp aliyeibua kashfa ya Bill Clinton na Monica Lewinsky
 
Babu shikamoo
I declare this "nakubali Sana MCHANGO wako apa JF uko very deep in detail ukitoa udini ww ni hazina apa JF Nina mengi ya kujifunza kwako Babu"
Ninja,
Wewe kwa umri wako na mimi kwa umri wangu wa miaka 71 wewe ni mwanangu si mjukuu.

Mjukuu wangu mkubwa ana umri wa miaka 10.

Mimi ni baba kwako.

Mimi sijapata kuandika dini kwani sina elimu hiyo.

Mimi nimezamia katika somo linalojulikana kama "Corrective History," yaani kurekebisha historia zilizokosewa.

Historia ya uhuru wa Tanganyika ilikuwa mhanga wa historia yake ya uhuru kuandikwa na watu ambao hawakuwa wanaijua na wengine kuipotosha kwa makusudi kwa kujaribu kukwepa mchango wa Waislam katika historia hiyo.
 
Ninja,
Wewe kwa umri wako na mimi kwa umri wangu wa miaka 71 wewe ni mwanangu si mjukuu.

Mjukuu wangu mkubwa ana umri wa miaka 10.

Mimi ni baba kwako.

Mimi sijapata kuandika dini kwani sina elimu hiyo.

Mimi nimezamia katika somo linalojulikana kama "Corrective History," yaani kurekebisha historia zilizokosewa.

Historia ya uhuru wa Tanganyika ilikuwa mhanga wa historia yake ya uhuru kuandikwa na watu ambao hawakuwa wanaijua na wengine kuipotosha kwa makusudi kwa kujaribu kukwepa mchango wa Waislam katika historia hiyo.
Usipanic Maalim neno babu siku hizi vijana wanalitumia pia kumaanisha mshikaji au rafiki. Hapo kwenye corrective history umenipa kitu kipya nilikuwa sikijui
 
Ninja,
Wewe kwa umri wako na mimi kwa umri wangu wa miaka 71 wewe ni mwanangu si mjukuu.

Mjukuu wangu mkubwa ana umri wa miaka 10.

Mimi ni baba kwako.

Mimi sijapata kuandika dini kwani sina elimu hiyo.

Mimi nimezamia katika somo linalojulikana kama "Corrective History," yaani kurekebisha historia zilizokosewa.

Historia ya uhuru wa Tanganyika ilikuwa mhanga wa historia yake ya uhuru kuandikwa na watu ambao hawakuwa wanaijua na wengine kuipotosha kwa makusudi kwa kujaribu kukwepa mchango wa Waislam katika historia hiyo.
Kaka yangu Mohamed, nikiri kuwa kwa siku za karibuni nimekuwa mhanga wa kufuatilia maandiko yako. Una hazina kubwa ya taarifa za kihistoria hasa kabla na wakati wa Uhuru bila kujali ni sahihi au lah. Kosa lako ni moja tu, kutanguliza Udini ktk maandiko yako. Vitabu vyote vya historia ya Uhuru wa Tanganyika nilivyowai kuvisoma,hakuna mwandishi aliyekwepa kutambua mchango wa unaowaita Waislam. Hiyo historia unayojaribu kuiweka sawa kama ingekuwa inaongelea Uislamu kama taasisi ningekuelewa, lakini unapo ongea Muislam kama mtu ni ubaguzi wa kidini unaoupalilia. Unataka kutuonyesha kuwa Waislam walibaguliwa tangu day one baada ya kupata uhuru?

Uniwiye radhi kwasababu nimepata muda wa kusoma threads zako nyingi, na sijasita kutia neno.
 
Mzee wetu,Ilimu yako iko vizuri,Nafikiri Sasa ni wakti wa kuanza kutoa speeches kwenye local colleges na ikiwezekana waanza kukutambua kwa kukupa Honorary PHD.Vipi uko interested au wako interested?Au wao wanagawa PHD kwa Wanasiasa TU?
 
Mzee wetu,Ilimu yako iko vizuri,Nafikiri Sasa ni wakti wa kuanza kutoa speeches kwenye local colleges na ikiwezekana waanza kukutambua kwa kukupa Honorary PHD.Vipi uko interested au wako interested?Au wao wanagawa PHD kwa Wanasiasa TU?
Tzhosts, ni kweli kama kuna watu wanaostahili honorary PhD basi huyu kaka yangu Mohamed Said anastahili kwasababu ya mchango wake mkubwa na machapisho yake.
 
Mzee wetu,Ilimu yako iko vizuri,Nafikiri Sasa ni wakti wa kuanza kutoa speeches kwenye local colleges na ikiwezekana waanza kukutambua kwa kukupa Honorary PHD.Vipi uko interested au wako interested?Au wao wanagawa PHD kwa Wanasiasa TU?
Naunga mkono Hoja, mzee wetu huyu si tu apewe PhD, bali apewe nafasi asomeshe watu historia hii katika vyuo na shule zetu hapa nchini.
 
Back
Top Bottom