Aibu stendi ya Msamvu Morogoro

Aibu stendi ya Msamvu Morogoro

Umuhirindahu

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2014
Posts
349
Reaction score
170
Leo nimepita Morogoro,nipo njiani kuelekea Mwanza,sikuamini nilichokiona....choo cha stand(public toilet) kipo kimoja na ni kidogo,watu wamepanga foleni inahitaji usubiri karibu dakika 10 upate nafasi ya kuhisaidia...zaidi ya yote ni kichafu balaa..kuna mama yupo pale bize akikusanya mia mbili kwa kichwa...anyway maswali nnayo jiuliza(naomba mnisaidie) hivi haiwezekan akapatikana mwekezaji wa kutatua tatizo hili...?.utaratibu wa kupata tenda kama hii ukoje?Wahusika hii hali wanaiona?
 
Waluguru bado hawajaacha mila zao za kujisaidia vichakani ndio maana manispaa hawaoni sababu ya kujenga vyoo vingi wakati wanyaji hakuna bali wanaacha vichaka vingi kudumisha mila na desturi ya wenyeji........
 
sababu ni kwamba huyo anaekusanya hela hatumii choo hicho.
 
Mkuu kuna vyoo viwili ila tatito ni hilohilo. Uchafu uchafu. Afu wahudumu wachafu kuliko vyoo vyenyewe. Pia ukosefu wa maji ndo imekuwa hatari. Viongozi nao njaa kama wale jamaa zetu wa Escrow.
 
Ule mji haujapata viongozi makini kabisa na kama wapo basi wamekumbwa na posho disease, juzi 31.12.2014 mitaro imeziba kwa takataka kiasi cha maji ya mvua kujaa kwenye maduka ya watu,

Pale stand kuu Msamvu kuna kijibanda karibu na maefesho ya daladala kina ile milango ya kuzunguka hakieleweki kina kazi gani, naamini kimejengwa kwa fedha nyingi ikiwamo ununuzi wa hiyo milango ambayo ni gharama sana

Stand ya daladala kule mjini kati nako kumeshonana hakuna hata dalili ya kuwa na mawazo mapya ya kuhamishia au kuweka mfumo mbadala wa kuondoa msongamano wa magari

Ukienda soko kuu nako balaa mvua zikinyesha hakuingiliki maana tope zito lenye harufu mbaya ndilolinabakia kuwa burudani na kivutio kwa viongozi wa manispaa
 
Ni uzembe wa viongozi husika katika manispaa ya Morogoro...


Hata haieleweki kamati za kudumu za bunge huwa zinapita kufanya nini maana kila kukicha hali inakuwa hovyo, nadhani ifike wakati mambo ya posho za vikao zifutwe ili uwajibikaji urejee kwasasa bila posho people never work
 
sababu ni kwamba huyo anaekusanya hela hatumii choo hicho.

Ataendaje choo njaa kali she/he does not eat due to little pay, wateja hawaendi kwakuwa mazingira ni hovyo as result makusanyo yanakuwa madogo wakati huohuo wakubwa wamepenyeza mirija kwenye makusanyo kiduchu
 
Kuna kitu tunakisahau pia. wananchi wake wapo wanajali usafi au? hilo la kwanza lakini la pili nadhani think tank ya manispaa(baraza la madiwani) linajali posho zaidi badala ya kuangalia tatizo la asili la mji kuwa chini.Aidha maji yaani water table ya Morogoro ipo juu sana na ujenzi unaofanyika hauzingatii ukweli huo. kwani hata mto kikundi haufanyiwi ukarabati kuweza kuendana na utoaji wa majui katika mji huo.ni taabu sana ukiwa na think tank dhaifu katika maisha yanayokwenda kasi:flame:
 
siyo kweli kuwa choo ni kimoja ukiwa unaingia getini kushoto kipo choo na upande wa parking ya madereva taxi ipo kingine kimoja
 
Leo nimepita Morogoro,nipo njiani kuelekea Mwanza,sikuamini nilichokiona....choo cha stand(public toilet) kipo kimoja na ni kidogo,watu wamepanga foleni inahitaji usubiri karibu dakika 10 upate nafasi ya kuhisaidia...zaidi ya yote ni kichafu balaa..kuna mama yupo pale bize akikusanya mia mbili kwa kichwa...anyway maswali nnayo jiuliza(naomba mnisaidie) hivi haiwezekan akapatikana mwekezaji wa kutatua tatizo hili...?.utaratibu wa kupata tenda kama hii ukoje?Wahusika hii hali wanaiona?
Same to. Stand mpya pale SIMU2000 jengo kubwa vyoo vichache,nenda stand ya shamba mbagala rangi 3 unaweza usijisaidie na haja ikayeyuka
 
siyo kweli kuwa choo ni kimoja ukiwa unaingia getini kushoto kipo choo na upande wa parking ya madereva taxi ipo kingine kimoja


Je vina sifa za kuitwa vyoo?
 
siyo kweli kuwa choo ni kimoja ukiwa unaingia getini kushoto kipo choo na upande wa parking ya madereva taxi ipo kingine kimoja

Havitoshelezi, matundu mawili kila kimoja na idadi ya watu pale ni kubwa.

Tatizo lingine stendi kubwa kama ile haina sehemu ya kupumzika na kusubiri abiria. Ukiwa mchana kukiwa na jua kali au mvua utaiona kero yake.
 
Leo nimepita Morogoro,nipo njiani kuelekea Mwanza,sikuamini nilichokiona....choo cha stand(public toilet) kipo kimoja na ni kidogo,watu wamepanga foleni inahitaji usubiri karibu dakika 10 upate nafasi ya kuhisaidia...zaidi ya yote ni kichafu balaa..kuna mama yupo pale bize akikusanya mia mbili kwa kichwa...anyway maswali nnayo jiuliza(naomba mnisaidie) hivi haiwezekan akapatikana mwekezaji wa kutatua tatizo hili...?.utaratibu wa kupata tenda kama hii ukoje?Wahusika hii hali wanaiona?

kila kitu muwekezaji tu,nenda wew ukajiwekeze
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom