Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally, amezungumzia sakata la mshambuliaji wa klabu hiyo, Jonathan Sowah, na kuthibitisha kuwa walimuondoa kambini Dodoma na kumrejesha Dar es Salaam mara baada ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons.
Ahmed amesema Sowah kwa sasa yupo nje ya kikosi cha Simba, huku akieleza kuwa klabu bado haijawa tayari kutoa taarifa ya kina kuhusu sababu za uamuzi huo.
“Sowah tulimuondoa kambini na kumrejesha Dar es Salaam. Siwezi kueleza ni kwa nini aliondolewa wala nini kitafuata hadi klabu itakapokuwa tayari kutoa taarifa rasmi kuhusu kilichotokea na hatua zitakazochukuliwa,” amesema Ahmed.
Kutokana na hali hiyo, huenda mshambuliaji huyo akaukosa mchezo wa Dabi ya Kariakoo dhidi ya Yanga utakaopigwa Machi 1, 2026 katika dimba la Amaan, Zanzibar.
“Sowah tulimuondoa kambini na kumrejesha Dar es Salaam. Siwezi kueleza ni kwa nini aliondolewa wala nini kitafuata hadi klabu itakapokuwa tayari kutoa taarifa rasmi kuhusu kilichotokea na hatua zitakazochukuliwa,” amesema Ahmed.
Kutokana na hali hiyo, huenda mshambuliaji huyo akaukosa mchezo wa Dabi ya Kariakoo dhidi ya Yanga utakaopigwa Machi 1, 2026 katika dimba la Amaan, Zanzibar.