Ndugu wasomaji na wanajukwaa naomba mfumo ufiche majina yangu niliyosajilia humu na hili jambo liende public tupate majibu ya serikali.
Tarehe 5 Juni 2025 serikali kupitia sekretarieti ya ajira ilitangaza nafasi za ajira nyingi katika kada mbalimbali, miongoni mwake zilikuwa nafasi 850 za walimu wa economics. Agost 13 waliitwa kwenye usaili wa mahojiano na maelekezo ikawa ni baada ya wiki mbili tangu tarehe hiyo wataanza kupangiwa vituo vya kazi.
Tangu pale kulikuwa na kimya kingi sana, mwezi Oktoba walipangiwa walimu 12 tu kati ya 850 na 838 kubaki bila kujua hatima yao.
Siku chache baada ya hapo katibu wa sekretarieti Mick Kiliba alitoa taarifa ya kuelekeza watendaji wake kupanga vituo kwa ajira ya mwaka wa fedha uliopita kabla ya November kuisha lakini halikutokea.
Baadaye waziri Ridhiwani Kikwete akatoa press kuelekeza kuanza kwa mchakato wa ajira 12000 na hizo ndio sauti ya kila kiongozi.
Ningependa tusaidieni mwenye kumfikia Kiliba atujulishe je, hizi 838 zilizobaki zitatoka lini? Au mpango wake umepitwa na wakati kwa hiyo tuondoe matumaini? Maana wale wa physics na biashara wameitwa interview tena kabla ya majibu ya Agosti.
Nimeuliza kuhusu Economics kwa sababu miaka mingi sasa sio somo la kipaumbele kwenye ajira za serikali. Sasa Katibu Mick Kiliba au Waziri Ridhiwani watupe mwelekeo wa hizo nafasi ili tujue mbivu na mbichi.
Bahati mbaya sana kupitia email ya sekretarieti, kupitia serikali mtandao nimelihoji mara nyingi na hawakuwahi kutoa response yoyote hata ya kuvunja moyo. Ahsante
Tarehe 5 Juni 2025 serikali kupitia sekretarieti ya ajira ilitangaza nafasi za ajira nyingi katika kada mbalimbali, miongoni mwake zilikuwa nafasi 850 za walimu wa economics. Agost 13 waliitwa kwenye usaili wa mahojiano na maelekezo ikawa ni baada ya wiki mbili tangu tarehe hiyo wataanza kupangiwa vituo vya kazi.
Tangu pale kulikuwa na kimya kingi sana, mwezi Oktoba walipangiwa walimu 12 tu kati ya 850 na 838 kubaki bila kujua hatima yao.
Siku chache baada ya hapo katibu wa sekretarieti Mick Kiliba alitoa taarifa ya kuelekeza watendaji wake kupanga vituo kwa ajira ya mwaka wa fedha uliopita kabla ya November kuisha lakini halikutokea.
Baadaye waziri Ridhiwani Kikwete akatoa press kuelekeza kuanza kwa mchakato wa ajira 12000 na hizo ndio sauti ya kila kiongozi.
Ningependa tusaidieni mwenye kumfikia Kiliba atujulishe je, hizi 838 zilizobaki zitatoka lini? Au mpango wake umepitwa na wakati kwa hiyo tuondoe matumaini? Maana wale wa physics na biashara wameitwa interview tena kabla ya majibu ya Agosti.
Nimeuliza kuhusu Economics kwa sababu miaka mingi sasa sio somo la kipaumbele kwenye ajira za serikali. Sasa Katibu Mick Kiliba au Waziri Ridhiwani watupe mwelekeo wa hizo nafasi ili tujue mbivu na mbichi.
Bahati mbaya sana kupitia email ya sekretarieti, kupitia serikali mtandao nimelihoji mara nyingi na hawakuwahi kutoa response yoyote hata ya kuvunja moyo. Ahsante