Ahadi ya Meli mpya kwa wana Kagera

Ahadi ya Meli mpya kwa wana Kagera

marcusgarvey

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2015
Posts
891
Reaction score
235
Katika kampeini iliyomwingizaJK madarakani, moja ya ahadi zake tamu ilikuwa ni kuwapatia wakazi wa mkoa wa Kagera meli mpya kama mbadala wa meli iliyopinduka ya MV Bukoba, ahadi hii kama kawaida ya chama tawala, CCM ni ile ile, sera ni zile zile.

Ahadi hii imeyeyuka na juzi jumatatu almanusura taifa liingie tena kwenye majonzi baada ya meli iliyochakaa na mbovu Mv Serengeti iliyokuwa haina hata boya moja kutaka kupinduka na kuleta maafa mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa manispaa ya bukoba waliokuwa pembezoni mwa ziwa wakishuhudia live sinema ya kutisha kwa zaidi ya masaa matano,kweli CCM ni ile ile na sera ni zile zile na ahadi ni zile zile.
 
Katika kampeini iloyomwingiza jk madarakani,moja ya ahadi zake tamu ilikuwa ni kuwapatia wakazi wa mkoa wa kagera meli mpya kama mbadala wa meli iliyopinduka ya mv bukoba,ahadi hii kama kawaida ya chama tawala,ccm ni ile ile,sera ni zile zile,ahadi hii imeyeyuka na juzi jumatatu almanusura taifa liingie tena kwenye majonzi baada ya meli nzee na mbovu mv serengeti iliyokuwa haina hata boya moja kutaka kupinduka na kuleta maafa mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa manispaa ya bukoba waliokuwa pembezoni mwa ziwa wakishuhudia live sinema ya kutisha kwa zaidi ya masaa matano,kweli ccm ni ile ile na sera ni zile zile na ahadi ni zile zilevcx
Na huku Songea grid ya taifa
 
Bingwa wa mambo Yohana Magu.Inaimarishwa reli ya kati pamoja na kuletwa meli kubwa za mizigo.Abıria tumia brbr nı ya haraka zaidı.
 
Katika kampeini iloyomwingiza jk madarakani,moja ya ahadi zake tamu ilikuwa ni kuwapatia wakazi wa mkoa wa kagera meli mpya kama mbadala wa meli iliyopinduka ya mv bukoba,ahadi hii kama kawaida ya chama tawala,ccm ni ile ile,sera ni zile zile,ahadi hii imeyeyuka na juzi jumatatu almanusura taifa liingie tena kwenye majonzi baada ya meli nzee na mbovu mv serengeti iliyokuwa haina hata boya moja kutaka kupinduka na kuleta maafa mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa manispaa ya bukoba waliokuwa pembezoni mwa ziwa wakishuhudia live sinema ya kutisha kwa zaidi ya masaa matano,kweli ccm ni ile ile na sera ni zile zile na ahadi ni zile zilevcx

Ndg kwa uongo huu! Daa! Umezidi. Una uhakika na unachokisema juu ya hili? "mv serengeti iliyokuwa haina hata boya moja" Nahodha wa meli hiyo na timu yake aliwashauri abiria watulie kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya sana. Zaidi ya hapo hata abiria walipohojiwa walijibu kuwa hata mtu angetumia mavazi maalumu ya kujihami isingesaidia kwa kuwa hali ya hewa ilikuwa mbaya sana. Hayo ya kwako ya kizushi wayatoa wapi yakhe? Hiii sasa sifa, ya kwako ni zaidi ya sinema.
 
Ta kamugisha,endelea kusubilia meli wakati hata mv victoria iko kwenye mawe,mv butiama nayo haiwezi kuimili mikikimikiki ya ziwa victoria,sanasana tusubili msiba mwingine mkubwa
 
Kumbuka kikwete aliahidi meli mpya yenye uwezo wa kuimili kashkash za lake victoria,meli inayozidi uwezo mv victoria,lkn mpaka leo imekuwa aibu kwa jk,nadhani mwenzangu umekulia lumumba na wewe ni wale wale wenye ahadi zile zile
 
A! Aaa! Kwa bahati mbaya JK hakuweza kutimiza ahadi hiyo kama ambavyo pia aliahidi meli mpya kule Kigoma, lakini msitie shaka wana Kagera na Wanakigoma, Pombe Magufuli atatimiliza yote kama mtamchagua. Upembuzi yakinifu na mchanganuo mahususi vilichelewa na hivyo kumcheleweshas JK kutimiza, lakini mpango mkakati umeshakuwa tayari na inshallah, Magufuli atatimiza. Tumpe kula zetu!!
 
A! Aaa! Kwa bahati mbaya JK hakuweza kutimiza ahadi hiyo kama ambavyo pia aliahidi meli mpya kule Kigoma, lakini msitie shaka wana Kagera na Wanakigoma, Pombe Magufuli atatimiliza yote kama mtamchagua. Upembuzi yakinifu na mchanganuo mahususi vilichelewa na hivyo kumcheleweshas JK kutimiza, lakini mpango mkakati umeshakuwa tayari na inshallah, Magufuli atatimiza. Tumpe kula zetu!!
 
kwetu alisema patakuwa Dubai ya Africa,kule kwake bwagamoyo alisema uwanja wa ndege ulaya utajengwa na bandari ya kisasa. Sasa kama kwao bwagamioyo hajajenga kitu itakuwa huko porini kwenu? kumbuka hata ifm ilikuwa wawe wamehamia msata bwagamioyo, holaaa.
 
Laiti ingezama na hatuombei ungesikia kamati imeundwa na kupewa miezi kibao kuchunguza kwakutumia kodi zetu wenyewe.
 
Wananchi wa Mikoa ya KAGERA, MWANZA, GEITA na MARA msiipigie CCM kura katika uchaguzi ujao wametudanganya kuwa watatuletea meli kubwa na yenye hadhi na mpaka leo hatujaona kitu. Jana mliona ile taharuki ya MV Serengeti karibu tuwapoteze ndugu zetu kama tuliwapoteza ndugu zetu katika ajali ya MV Bukoba. KATAENI CCM ni walaghai sana.
 
A! Aaa! Kwa bahati mbaya JK hakuweza kutimiza ahadi hiyo kama ambavyo pia aliahidi meli mpya kule Kigoma, lakini msitie shaka wana Kagera na Wanakigoma, Pombe Magufuli atatimiliza yote kama mtamchagua. Upembuzi yakinifu na mchanganuo mahususi vilichelewa na hivyo kumcheleweshas JK kutimiza, lakini mpango mkakati umeshakuwa tayari na inshallah, Magufuli atatimiza. Tumpe kula zetu!!

Hivi unaelewa nini maana ya ahadi??
 
Katika kampeini iloyomwingiza jk madarakani,moja ya ahadi zake tamu ilikuwa ni kuwapatia wakazi wa mkoa wa kagera meli mpya kama mbadala wa meli iliyopinduka ya mv bukoba,ahadi hii kama kawaida ya chama tawala,ccm ni ile ile,sera ni zile zile,ahadi hii imeyeyuka na juzi jumatatu almanusura taifa liingie tena kwenye majonzi baada ya meli nzee na mbovu mv serengeti iliyokuwa haina hata boya moja kutaka kupinduka na kuleta maafa mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa manispaa ya bukoba waliokuwa pembezoni mwa ziwa wakishuhudia live sinema ya kutisha kwa zaidi ya masaa matano,kweli ccm ni ile ile na sera ni zile zile na ahadi ni zile zilevcx

Wananchi wa kanda ya ziwa maisha ni zaidi ya meli.
 
Kuna siku nilikuwa nasikiliza bunge, nilisikia kama waziri alisema hizo meli ziko hatua za mwisho. Lakini leo ni miaka kama miwil imepita. CCM ni zaidi ya jang.
 
Kwa watu wa mkoa wa kagera meli ndo kiunganishi rahisi kwa mikoa mingine ya ukanda wa ziwa,meli ndo yenye gharama nafuu za usafiri wa abiria na mizigo,na ndo maana jk aliona akitoa ahadi hii ndipo ataweza kuwateka wakazi wa kanda ya ziwa,point ni kwamba alihaidi kwa miaka kumi kwa confidence kubwa kuwa atatekeleza,hata hivyo imebaki kuwa hadithi,bidhaa zinazid kupanda bei kwasababu ya gharama za kusafirisha mizigo kuwa kubwa,ndizi pale mwanza ni bei kali tofauti na kipindi ilipokuwa inafanya kazi mv victoria
 
"HOJA KUU NI AHADI YA MELI MPYA KWA WAKAZI WA KANDA YA ZIWA." Twendelee....

Ndg kwa uongo huu! Daa! Umezidi. Una uhakika na unachokisema juu ya hili? “mv serengeti iliyokuwa haina hata boya moja” Nahodha wa meli hiyo na timu yake aliwashauri abiria watulie kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya sana. Zaidi ya hapo hata abiria walipohojiwa walijibu kuwa hata mtu angetumia mavazi maalumu ya kujihami isingesaidia kwa kuwa hali ya hewa ilikuwa mbaya sana. Hayo ya kwako ya kizushi wayatoa wapi yakhe? Hiii sasa sifa, ya kwako ni zaidi ya sinema.
 
Back
Top Bottom