Ahadi hewa kuhusu ongezeko la mishahara

Ahadi hewa kuhusu ongezeko la mishahara

Mimi sio mtumishi ila kuna watumishi kama wawili nimeona wana Complain watu wa Karibu yangu

Sasa wacha walalamike wao, wewe unaingia unapapatika kama kuku aliyekatwa ghafla kichwa kufanya nini? Wao hawana smart phone za kutokea duku duku zao humu? Unaelewa taratibu za annual increment? Au wewe unaponea hapo kwenye kipato chao? Nenda kafanye kazi zako, achana na mishahara ya watu!
 
Mimi kwangu imeongezeka 197,000

I guess kwa mwezi nina nyongeza ya 96500 maana walisema wataweka nyongeza ya two month pamoja.

So, yes nyongeza ya mshahara imetufikia
 
Mkuu! Ukiamua kuajiriwa, lizika na unachopangiwa na bosi wako. Bosi hawezi kukulipa kiwango cha kukidhi mahitaji yako vinginevyo utaacha kumtumikia. Mwajiri na waajiri wote ulipa kiwango cha kumfanya mwajiriwa awe tegemezi ili kila siku uwaze bila yeye huwezi kuishi! Wanaojitambua wakipata mtaji husepa! Kalaghabao!
Andika basi kwa kiswahili

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
mimi ni mtumishi, nilikuwa nalipwa takehome ya Tsh. 1,550,000/=, ila mshahara wa mwezi huu nimeongezewa laki 3 na elfu 40, kwaiyo mshahara wa mwezi huu nimepokea Tsh. 1,890,000/= kama takehome.

Wewe ni muongo mkubwa kwani hiyo tsh 340,000/- ilikuwa ni posho hadi isiwe na makato ya kodi baada ya kuongezwa kwenye mshara wa awali? Maana umeongeza hiyo figure toka mshahara wa awali bila kodi ndani as if ni allowance fulani? Kwanza kwa huo mshahara uliokuwa unapata kabla huwezi kuongezewa annual increment ya kiasi hicho, au nikurudhie circular hapa uone! Acha kupiga watu kamba hapa!
 
Wee muongo! Yaani uongezewe 340,000 alafu nzimanzima iongezeke kwenye take home bila kukatwa kodi? Acha fix mbele ya watu wenye akili

Yeye anadhani anadanganya kuku hapa! Kwanza kwa mshahara wake huo hawezi kuongezewa ths 340,000/- Hii ni kwa wenye mishahara inayoanzia tsh 4,000,000/- na kwenda juu.
 
mimi ni mtumishi, nilikuwa nalipwa takehome ya Tsh. 1,550,000/=, ila mshahara wa mwezi huu nimeongezewa laki 3 na elfu 40, kwaiyo mshahara wa mwezi huu nimepokea Tsh. 1,890,000/= kama takehome.
Ss mleta uzi huu unatoa wapi maneno ya uongo zidi ya serikali? Mama piga kazi wenyewe watumishi wamesema kwa maneno na vitendo.
 
Unatakiwa kwanza kuelewa kuwa annual salary increment ni ongezeko la mwaka la mshahara kulingana na kiwango chako cha mshahara kwa mwezi. Kama katika circular umeandikiwa annual increment yako ni tsh 40, 000 ina maana ikiisha miezi 12 juu ya msumari utaongezewa sh 40,000 kwenye mshahara wako.
Pili kama hujaongezewa ina maana tangu ajira yako au tangu kupanda daraja au tangu kupewa cheo kipya chenye mshahara mpya, hujatimiza miezi 12, kwa hiyo annual increment yako itakuwa effected mwezi July 2024. Nadhani wengi mnaolalamika humu ni vijana msiojua annual increments zinalipwaje! Haya nenda chapu kafanye kazi! Subiri hiyo mpaka 2024 kwa sababu kwanza umeandika kitu usichokijua kufikiria waliolipwa annual increment ni flat rate! Hata mimi ni mfanyakazi lakini najua annual increment inalipwaje! Kama ulimalizia vijihela vya wiki iliyopita kwenye kiti moto ukijua wiki hii kuna mshahara mpya wenye increment mlima basi utakuwa umekutana na moto mkali! Nenda kajipinde ofisini kama samaki wa kwenye senti tano!
Case closed kwa hii comment tu
 
sijakulazimisha uamini mkuu, nimeelezea uhalisia
Wewe kabisa uliyekuwa ukimlalamikia baba yako kuuza nyumba yake, na kutumbua hela yote peke yake! Na pasipo kukupa hata 100 kama urithi! Au nimekufananisha?
 
Back
Top Bottom