AFYA: Je, Unafahamu kwikwi ni nini na chanzo chake?

AFYA: Je, Unafahamu kwikwi ni nini na chanzo chake?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
693
Reaction score
1,164
20210114_144408_0000.png


Kwikwi hutokana na kushtuka na kusinyaa kwa ghafla kwa misuli mikuu ya upumuaji (diaphragm) ambako hujirudia rudia na kusababisha hewa kuingia kwa kasi kwenye mapafu.

Kwikwi sio ugonjwa; kwikwi ya muda mfupi ni kero ndogo tu ambayo inapita, lakini kwikwi isiyokatika inaweza kuwa dalili ya tatizo lingine ambalo huenda likahitaji uchunguzi wa kitaalamu.

Sababu zinazopelekea kupata kwikwi;

Kula haraka haraka au kula sana (kuvimbiwa)
Kula vyakula vyenye viungo sana
Kunywa vinywaji vyenye gesi(carbonated beverages) au vya baridi sana
Ulevi au kunywa pombe nyingi kwa mpigo
Upungufu wa maji na madini mwilini (dehydration)
Tumbo kujaa gesi, asidi (hyperacidity) au vidonda vya tumbo

Sababu hizi mara nyingi husababisha kwikwi ya muda mfupi ambayo huisha bila kuhitaji matibabu wala uchunguzi wa kitaalamu.

Kuzuia kwikwi ni muhimu tu kwa wale wanaopata mara kwa mara.
Matibabu ya kienyeji: (Usifanye kwa mtoto)

Kumshitua mhusika, au kumzubaisha ili kuondoa mawazo yake kwenye kwikwi

Kunywa glasi ya maji iliyojaa bila kukata pumzi

Kubana pumzi na kuhesabu mpaka kumi

Kuweka sukari chini ya ulimi
Kulala. Usingizi ni dawa moja nzuri sana ya kwikwi

Kwa mtoto anayenyonya waweza kumnyonyesha, au kumuweka begani ili acheue

Muone daktari kwa matibabu kama

Kwikwi haikatiki kwa muda mrefu (siku au zaidi), Kwikwi inakusababisha kuchoka sana, Kama mapigo ya moyo yanabadilika, Kama unashindwa kulala kutokana na kwikwi,Kama inasababisha msongo mawazo kutokana na kujirudia mara kwa mara.
 
VIPI kuhus kwikwi iliyodumu kwa zaidi ya mwezi, na njia zote ulizotaja zikawa zmeshindwa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom