kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,931
- 7,828
Kuna watu wanaona dunia na wamarekani hawakumuelewa Trump. Tabia ya kibabe na kujitwisha upolisi wa dunia ni sera iliyoiletea mzigo mkubwa kifedha marekani na kusababisha uchumi wake kuzorota. Kisaikolojia Marekani imeiweka dunia kuelewa wao ni tajiri kupindukia na ni kama baba wa dunia.
Hali hii inahatarisha nafasi ya marekani kiuchumi duniani kwani nchi zingine kama China zinasonga mbele haraka na bila kutapanya mali zake duniani. Marekani sera yake ya kujimwambafy ni unafiki kwani inaacha umaskini kwa watu wake wa kawaida ukitapakaa huku ikijifanya kusaidia dunia kwa manufaa ya matajiri wake ambao ni matajiri duniani.
Hicho nilichoeleza ndio Trump alikua anajaribu kurekebisha. Marekani kuachana kujitwisha majukumu kifedha duniani na kutaka wengine kutoa mchango sawa.
Kwa mfano alitaka kujitoa kijeshi ulaya na maeneo mengi kupunguza matumizi ili kuimarisha uchumi wao. Pia kushawishi wawekezaji wa Marekani kurudisha mitaji yao Marekani ili kurejesha ajira kwa Wamarekani.
Kwa sera za Marekani Afrika ilipata nafuu ya kuingiliwa mambo yake.
Tukumbuke uingiliaji wa nje wa sera za mademocrats kama kule libya na suala la Rwanda kuvamia Congo mambo yaliyoleta maafa makubwa Afrika. Tusisahau sera za mademocrats za kina Obama kulazimisha mtazamo wao kuhusu ushoga na ndoa za jinsia moja. Tusisahau tamaa ya kuweka vituo vya kijeshi Afrika.
Kwa ufupi Trump alitoa likizo kuhusu sera za ubeberu mkali wa Marekani. Kwa wenye kuona kwa macho matatu wanaona bora trump angeendelea urais Marekani.
Mnasemaje wandugu
Hali hii inahatarisha nafasi ya marekani kiuchumi duniani kwani nchi zingine kama China zinasonga mbele haraka na bila kutapanya mali zake duniani. Marekani sera yake ya kujimwambafy ni unafiki kwani inaacha umaskini kwa watu wake wa kawaida ukitapakaa huku ikijifanya kusaidia dunia kwa manufaa ya matajiri wake ambao ni matajiri duniani.
Hicho nilichoeleza ndio Trump alikua anajaribu kurekebisha. Marekani kuachana kujitwisha majukumu kifedha duniani na kutaka wengine kutoa mchango sawa.
Kwa mfano alitaka kujitoa kijeshi ulaya na maeneo mengi kupunguza matumizi ili kuimarisha uchumi wao. Pia kushawishi wawekezaji wa Marekani kurudisha mitaji yao Marekani ili kurejesha ajira kwa Wamarekani.
Kwa sera za Marekani Afrika ilipata nafuu ya kuingiliwa mambo yake.
Tukumbuke uingiliaji wa nje wa sera za mademocrats kama kule libya na suala la Rwanda kuvamia Congo mambo yaliyoleta maafa makubwa Afrika. Tusisahau sera za mademocrats za kina Obama kulazimisha mtazamo wao kuhusu ushoga na ndoa za jinsia moja. Tusisahau tamaa ya kuweka vituo vya kijeshi Afrika.
Kwa ufupi Trump alitoa likizo kuhusu sera za ubeberu mkali wa Marekani. Kwa wenye kuona kwa macho matatu wanaona bora trump angeendelea urais Marekani.
Mnasemaje wandugu
kama marekani itakuwa kama ulaya maneno matupu bila vitendo haki ya MUNGU mtachinjana mpaka basi na ubabe wenu wa kilofa mfano Saudia, congo, afagh,Libya nk marekani inajitahidi kuzima ubabe wa wawababe