Ni zaidi ya nusu karne tokea mwaka 1960 uitwe mwaka wa Afrika.
Katika kipindi hiki Afrika imeshuhudia ustawi wa kujivunia lakini pia imelia na kusaga meno kwa udhalimu na maangazi makubwa dhidi ya watu wake.
Afrika imeongozwa na viongozi wema na waadilifu kama Mwalimu Nyerere, Kwame Nkrumah wa Ghana na Kenneth Kahunda wa Zambia.
Afrika imeteswa katika mikono ya wauwaji na mafisadi kama Mobutu wa Zaire, Sani Abacha wa Nigeria, na sasa wapo kina Al Bashir wa Sudan na wengine wengi.
Miaka zaidi ya hamsini baada ya uhuru kutoka ukoloni mkongwe, Afrika inayashuhudia mambo yote yaliyowasukuma wanamapinduzi kudai uhuru ambayo ni: ukoloni wa mfumo wa uliberali mamboleo, dhuluma, unyonyaji, udini, ukabila na ubaguzi wa rangi na kila aina ya uovu.
Baya zaidi ni kwamba serikali nyingi zilizochaguliwa kidemokrasia zina sura ya kidikteta. Zinanuka rushwa na ufisadi. Zinatumia mabavu na sheria kuikiuka na kuidhibiti haki. Zinawaonea na kuwanyonya raia.
Ni jambo la kawaida kumkuta mama lishe analipa kodi zaidi ya "mwekezaji" anayemiliki hoteli ya kimataifa au mgodi wa dhahabu.
Matokeo yake ni kuongezeka kwa umaskini, ujinga na magonjwa ingawa takwimu zao zinaonyesha uchumi kukua na kupongezwa na Benki ya Dunia na IMF. Kwa waafrika wengi tumaini la kuiona Afrika yenye neema ya asali na maziwa limetoweka.
Katika kipindi hiki Afrika imeshuhudia ustawi wa kujivunia lakini pia imelia na kusaga meno kwa udhalimu na maangazi makubwa dhidi ya watu wake.
Afrika imeongozwa na viongozi wema na waadilifu kama Mwalimu Nyerere, Kwame Nkrumah wa Ghana na Kenneth Kahunda wa Zambia.
Afrika imeteswa katika mikono ya wauwaji na mafisadi kama Mobutu wa Zaire, Sani Abacha wa Nigeria, na sasa wapo kina Al Bashir wa Sudan na wengine wengi.
Miaka zaidi ya hamsini baada ya uhuru kutoka ukoloni mkongwe, Afrika inayashuhudia mambo yote yaliyowasukuma wanamapinduzi kudai uhuru ambayo ni: ukoloni wa mfumo wa uliberali mamboleo, dhuluma, unyonyaji, udini, ukabila na ubaguzi wa rangi na kila aina ya uovu.
Baya zaidi ni kwamba serikali nyingi zilizochaguliwa kidemokrasia zina sura ya kidikteta. Zinanuka rushwa na ufisadi. Zinatumia mabavu na sheria kuikiuka na kuidhibiti haki. Zinawaonea na kuwanyonya raia.
Ni jambo la kawaida kumkuta mama lishe analipa kodi zaidi ya "mwekezaji" anayemiliki hoteli ya kimataifa au mgodi wa dhahabu.
Matokeo yake ni kuongezeka kwa umaskini, ujinga na magonjwa ingawa takwimu zao zinaonyesha uchumi kukua na kupongezwa na Benki ya Dunia na IMF. Kwa waafrika wengi tumaini la kuiona Afrika yenye neema ya asali na maziwa limetoweka.