Afrika Kusini wanayo hoja?


nchi zote ulizozitaja zinazopinga uhamiaji hawaui wala kuwachoma moto wao hawana haki ya kuwachoma moto. je wewe umependa hii ya kuwachoma? kwani hawana njia nyingine za kuwatoa wahamiaji south africa
 

Issue sio kuwaondoa bali wanawaondoaje? Kwa kuwasha moto biashara zao? Ama kwa kuwauwa kwa kuwachoma moto
 
SA na Tanzania ni tofauti SA raia wao wamepewa kipaumbele sana kwa kila utakachokihitaji kufanya kama umedhamilia tofauti na Tanzania vikwazo vingi...ukitaka kuanzisha kiwanda chochote hata kama huna eneo wapo watu wanasimamia na vyote unapata wapo Wasouth tuliowaambia wanafanya na wengine walishafanikiwa kitambo kupitia hizo fursa...wewe ukiwa na Identity isiyochafuka unaomba mkopo mpaka wa 200,000,000 kwenye simu watakuja kuhakikisha address yako baadae wiki tuu ushapata hela na kama una kazi unasambaza mzigo maisha yanaenda...Wazimbabwe ndio wamekua wakopaji wakuu na tenda nyingi za serikali wanachukua wao wengi wana address na id sasa wewe usiitwe mjinga kwa nini wakati fursa zipo kwako nje nje...
 
Kila Rais abaki na vijana wake, aangalie sera zake kuhusu vijana na ajira kwa vijana wake, atafute njia sahihi za kuwavutia vijana wake wabaki na waipende nchi yao. Hakuna mtu wala kikundi cha watu kinachopaswa kuilazimisha SA iwapokee wahamiaji eti kwa kuogoga kulaumiwa au Boko haram. Boko haram ni matunda ya siasa chafu, na sera mbovu za uchumi kwa vijana.
 
Issue sio kuwaondoa bali wanawaondoaje? Kwa kuwasha moto biashara zao? Ama kwa kuwauwa kwa kuwachoma moto
kuna wale waliowaondoa wafugaji wahamiaji haramu kwenye mashamba yao kwa kuwakatakata mapanga ng'ombe wao, tena watanzania wenzao. Pia kuna wale wahamiaji haramu kule Kagera ambao walifurushwa na mifugo yao bila kujitetea.

Jambo la msingi SA iwaondoshe wahamiaji haramu wooooooooooooooooote warudi kwao, na wale waliofungua biashara ya vinyozi, kuuza ukwaju, viberiti na dawa za kulevya waondoke mara moja ili wabakie wale wageni wanaostahili kubaki kwenye kazi za hospitalini na kwingineko ambao utaalamu wao unahitajika. Tuache visingizio vya kijinga vya eti ni wavivu, ni walevi, hawajitambui, hawazioni fursa, nk. it is nonsense.
 
Mleta mada anadanda danda tu na utetezi wake,hakuna nchi ambayo haina wahamiaji lakini pia kila nchi inapambana kuzuia uhamiaji haramu ila serikali ya SA haifanyi nliiona kipindi kimoja cha Tv kilikuwa kinawahoji wabongo wanaishi SA,yani kuna mbongo teja huko SA na hana kibali cha kuishi huko ila anakwambia ameshakamatwa sana na polisi huko ila anaachiwa na polisi wameshamzoe. Sasa hata Tz serikali isingewajibika katika kuzuia wahamiaji haramu basi pia nako wangejaa hivyo huwezi kulaumu nchi wanazotoka hao wahamiaji haramu inachotakiwa ni serikali kuwadhibiti.

Sasa serikali ya SA imeshindwa kutimiza majukumu yake na matokeo yake wananchi hufanya uhalifu na serikali inawaangalia na wewe mkuu unaona wa sawa tu hujari kuwa kuna hawamiaji halali nao hushambuliwa.
 
Dawa ya hilo sio vijana kukimbilia SA bali ni kuishinikisha na kuishawishi serikali yao inawarahisishia maisha yao. Na wataweza kufanya hivyo kwa kubaki nchini mwao na kuhakikisha kuwa kwa gharama yoyote ile wanawachagua viongozi ambao watayafanya maisha yao yawe bora hukohuko kwenye inchi zao. Wahakikishe kuwa wanapiga kura, kila kura inahesabiwa na matokeo ya kura yanatangazwa kama yalivyo.
 
Na mimi ninakubaliana na wewe mkuu kwamba serikali haikufanya kazi yake ya kuwafurusha wahamiaji na wala kuweka utaratibu kwa wahamiaji waliotaka kufanya kazi na biashara ndogondogo. Lakini ni lazima ukumbuke kuwa kuwazuia wahamiaji ni kazi ngumu sana inayohitaji bajeti kubwa sana. Marekani inawalazimu kujenga ukuta ngali sana kusaidia mikakati mingine iliyopo ya kuwazuia wahamiaji. Lakini pia, hata hapa Tanzania ni Dr. JPM aliyeanza kuipa sura mpya CCM. CCM ya zamani na vyama vingine vyilivyoleta uhuru kwenye mataifa yao vilikumbatia "Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja". Vyama hivi havikujali hali ya uchumi kwa wananchi wao bali amani na utulivu kwa mataifa yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…