comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 8,222
- 5,946
Wanabodi, mimi hapa sijaongeza neno hata moja naileta ramli hii kama ilivyo; ukiikubali sema twawile; ukiikataa nenda kwa mganga mwingine; au bali hivyo ulivyokuwa unaamini.
Wakati tukianza ngwe ya pili ya miaka 20 ya karne hii ni vema muyasikie haya ya Wapiga Ramli kuhusu Afrika na wana wa Afrika katika miaka 20 ijayo.
Wapiga ramli wa masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii wanatabiri yafuatayo kuhusu Afrika;
1. ELIMU
(i) Uwekezaji katika elimu/rasilimali watu utendelea kusuasua na kutokuwa kipaumbele kwa nchi nyingi.
(ii) Wachache wenye elimu bora hawatakuwa na msaada mkubwa sana kwa jamii bali watatumia elimu yao kuwatawala wasio na elimu kubwa na pia kujilimbikizia mali.
(iii) Uandishi na usomaji wa vitabu kama chanzo cha maarifa utazikwa kaburini
.(iv) Vyanzo vingine vya elimu kama "simu janja", teknohama, vitaendelea kutumika kimzaha mzaha tu, hasa kufukua na kushabikia miziki na udaku.
2. SIASA NA UONGOZI BORA.
(i) Kizazi kilicholeta uhuru kitakuwa kinatoweka na kitatoweka na maadili na taratibu zake za uongozi.
(ii) Uongozi wa kizazi kipya chenye mlengo na haiba ya popo kitashamiri. Kizazi hicho kitataka kupata mafanikio yanayohitaji mipango thabiti na muda wa kutosha katika muda mfupi sana.
Kitatamani Afrika iwe kama Ulaya Magharibi au China katika muda mfupi wa miaka 10-15. Hakitakuwa na vipaumbele vinavyolenga maendeleo ya watu, bali miradi ya kujifananisha na Ulaya.
Kitatamani uafrika kwa maneno lakini kitauenzi uzungu kwa vitendo.
(iii) Demokrasia itazidi kudorola. Shughuli za kisiasa zitatekwa nyara na vikundi vya watawala ili watawale "milele", wao, wake zao, watoto wao au wajukuu zao.
(iv) Katiba za nchi nyingi zitakuwa kama vitabu vya hadithi za Abnuas. Watawala watazisigina watakavyo.
(v) Uhuru wa kujieleza, kukosoa watawala utaota mbawa. Watawala wa kizazi hicho watatamani kuwa na hati milki ya mawazo ya wananchi wanao watawala.
(vi) Haki ya wananchi kuchagua viongozi wao na kupanga mstakabari wa maisha yao na dira ya nchi zao itanyakuliwa na watawala na makuadi wa kisiasa.
Harakati za kudai "Haki na Uhuru" katika nchi ambazo ni "huru", zitatamalaki Afrika, na kujirudia kama ilivyokuwa miaka ya 1950-60.
(vii) Wasomi wengi wa Afrika wataikimbia siasa na kusubiri fadhila ya kuzawadiwa vyeo vya kiutawala. Midomo ya itafungwa kulinda mikate yao.
3. UCHUMI
(i) Utegemezi kiuchumi utaongezeka. China itazipiku nchi za Magharibi katika kuitawala Afrika kiuchumi, hasa kwa nchi za Bustani ya Eden (Afrika chini ya Sahara).
(ii) kwa mshawasho wa maendeleo ya chapuchapu, viongozi wa Afrika watavamia "misaada" na mikopo "ndoana" kutoka China na hivyo kuifanya Eden kuwa "mali" ya China kiuchumi.
(iii) Uzalishaji mali na hasa kilimo utaendelea kwa kasi hii hii ya konokono, na kutoa fursa ya nchi nyingine za mashariki ya mbali nazo kuimiliki kiasi Afrika kupitia chakula.
(iv) Wana wa Afrika walio wengi waishio mijini na vijijini hali zao kiuchumi zitakuwa za kubahatisha.
(v) Mataifa ya Magharibi hayatakubali kuachia milki ya uchumi wa Afrika na rasilimali zake. Vita kati ya China, Urusi, Marekani na Ulaya kuhusu rasilimali za Afrika itakuwa kubwa sana.
Wachumi na watawala wa Afrika kwa pamoja wataendelea kukusanywa na kuwekwa kwenye
vyumba vya majadilianao ya "ushirikiano wa kiuchumi" pale Beijing, Moscow, Brussels na Washington. Kama kawaida,mwataambulia majigambo ya kuhudhuria mikutano hiyo.
(vi)"Utumwa" wa kichumi utakuwa changamoto kubwa kwa wana wa Afrika.
4. MAISHA YA KIJAMII
(i) Matamanio ya kutajirika bila kufanya kazi yataongezeka. Michezo ya kamari itashamiri hadi vijijini.
(ii) "Utumwa" wa fikra utaimarika. Milana desturi za kiafrika zitayeyuka kwa kasi kubwa.
(iii) Ulaghai wa kidini utaongezeka. Viongozi wa kidini wanaoishi kwa kuwafukarisha waumini wataongezeka.
(iv) "Biashara" ya waafrika kwenda kuabudu ughaibuni, wakiaminishwa kuwa huko ni mataifa teule na watapata thawabu za Mwenyezi Mungu itaongezeka sana.
(v) "Uhuru" wa mabinti kuhusu kutumia miili na talanta zao utaongezeka.
(vi) Janga la ushoga litainyemelea Afrika kwa kasi kubwa.
(vii) matarajio ya kuwaunganisha wana wa Afrika kibiashara na kiuchumi (EAC, SADC, TFTA, AfCFTA) yatakumbwa na changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni ubinafsi tu wa wana wa Afrika wenyewe.
(viii) Wanamichezo waafrika/wenye asili ya Afrika popote walipo wataendelea kuiteka Dunia.
(ix) Tabia ya"omba omba" itazagaa kuanzia kitaifa hadi ngazi ya mtu mmoja mmoja, bila kujali nafasi ya mtu katika uongozi wa nchi, dini au familia.
(x) Wengi wa wana wa Afrika wataaminishwa na manabii wa uongo kuwa changamoto za maisha yao zitaondoka kupitia Nyumba za Ibada. Wengi watanasa katika mtego huu.
(xi) Pamoja na misukosuko hiyo wana wa Afrika wataendelea kuthamini UTU kuliko watu wa mataifa nje ya Afrika.
(xii) Wana wa Afrika wataendelea kulinda uhuru wa bendera kwa mbwembwe zote na mshikamano.
Waungwana, je itakuwa vema kuyapuuza hayo ya wapiga ramli kuhusu Afrika kwa kuwa ramli hizo zimejikita kwenye mengi mabaya au ni vema tuzitafakari mapema na kuchukua hatua stahiki, ili mabaya tajwa yasitokee?
Karibu 2020.
Wakati tukianza ngwe ya pili ya miaka 20 ya karne hii ni vema muyasikie haya ya Wapiga Ramli kuhusu Afrika na wana wa Afrika katika miaka 20 ijayo.
Wapiga ramli wa masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii wanatabiri yafuatayo kuhusu Afrika;
1. ELIMU
(i) Uwekezaji katika elimu/rasilimali watu utendelea kusuasua na kutokuwa kipaumbele kwa nchi nyingi.
(ii) Wachache wenye elimu bora hawatakuwa na msaada mkubwa sana kwa jamii bali watatumia elimu yao kuwatawala wasio na elimu kubwa na pia kujilimbikizia mali.
(iii) Uandishi na usomaji wa vitabu kama chanzo cha maarifa utazikwa kaburini
.(iv) Vyanzo vingine vya elimu kama "simu janja", teknohama, vitaendelea kutumika kimzaha mzaha tu, hasa kufukua na kushabikia miziki na udaku.
2. SIASA NA UONGOZI BORA.
(i) Kizazi kilicholeta uhuru kitakuwa kinatoweka na kitatoweka na maadili na taratibu zake za uongozi.
(ii) Uongozi wa kizazi kipya chenye mlengo na haiba ya popo kitashamiri. Kizazi hicho kitataka kupata mafanikio yanayohitaji mipango thabiti na muda wa kutosha katika muda mfupi sana.
Kitatamani Afrika iwe kama Ulaya Magharibi au China katika muda mfupi wa miaka 10-15. Hakitakuwa na vipaumbele vinavyolenga maendeleo ya watu, bali miradi ya kujifananisha na Ulaya.
Kitatamani uafrika kwa maneno lakini kitauenzi uzungu kwa vitendo.
(iii) Demokrasia itazidi kudorola. Shughuli za kisiasa zitatekwa nyara na vikundi vya watawala ili watawale "milele", wao, wake zao, watoto wao au wajukuu zao.
(iv) Katiba za nchi nyingi zitakuwa kama vitabu vya hadithi za Abnuas. Watawala watazisigina watakavyo.
(v) Uhuru wa kujieleza, kukosoa watawala utaota mbawa. Watawala wa kizazi hicho watatamani kuwa na hati milki ya mawazo ya wananchi wanao watawala.
(vi) Haki ya wananchi kuchagua viongozi wao na kupanga mstakabari wa maisha yao na dira ya nchi zao itanyakuliwa na watawala na makuadi wa kisiasa.
Harakati za kudai "Haki na Uhuru" katika nchi ambazo ni "huru", zitatamalaki Afrika, na kujirudia kama ilivyokuwa miaka ya 1950-60.
(vii) Wasomi wengi wa Afrika wataikimbia siasa na kusubiri fadhila ya kuzawadiwa vyeo vya kiutawala. Midomo ya itafungwa kulinda mikate yao.
3. UCHUMI
(i) Utegemezi kiuchumi utaongezeka. China itazipiku nchi za Magharibi katika kuitawala Afrika kiuchumi, hasa kwa nchi za Bustani ya Eden (Afrika chini ya Sahara).
(ii) kwa mshawasho wa maendeleo ya chapuchapu, viongozi wa Afrika watavamia "misaada" na mikopo "ndoana" kutoka China na hivyo kuifanya Eden kuwa "mali" ya China kiuchumi.
(iii) Uzalishaji mali na hasa kilimo utaendelea kwa kasi hii hii ya konokono, na kutoa fursa ya nchi nyingine za mashariki ya mbali nazo kuimiliki kiasi Afrika kupitia chakula.
(iv) Wana wa Afrika walio wengi waishio mijini na vijijini hali zao kiuchumi zitakuwa za kubahatisha.
(v) Mataifa ya Magharibi hayatakubali kuachia milki ya uchumi wa Afrika na rasilimali zake. Vita kati ya China, Urusi, Marekani na Ulaya kuhusu rasilimali za Afrika itakuwa kubwa sana.
Wachumi na watawala wa Afrika kwa pamoja wataendelea kukusanywa na kuwekwa kwenye
vyumba vya majadilianao ya "ushirikiano wa kiuchumi" pale Beijing, Moscow, Brussels na Washington. Kama kawaida,mwataambulia majigambo ya kuhudhuria mikutano hiyo.
(vi)"Utumwa" wa kichumi utakuwa changamoto kubwa kwa wana wa Afrika.
4. MAISHA YA KIJAMII
(i) Matamanio ya kutajirika bila kufanya kazi yataongezeka. Michezo ya kamari itashamiri hadi vijijini.
(ii) "Utumwa" wa fikra utaimarika. Milana desturi za kiafrika zitayeyuka kwa kasi kubwa.
(iii) Ulaghai wa kidini utaongezeka. Viongozi wa kidini wanaoishi kwa kuwafukarisha waumini wataongezeka.
(iv) "Biashara" ya waafrika kwenda kuabudu ughaibuni, wakiaminishwa kuwa huko ni mataifa teule na watapata thawabu za Mwenyezi Mungu itaongezeka sana.
(v) "Uhuru" wa mabinti kuhusu kutumia miili na talanta zao utaongezeka.
(vi) Janga la ushoga litainyemelea Afrika kwa kasi kubwa.
(vii) matarajio ya kuwaunganisha wana wa Afrika kibiashara na kiuchumi (EAC, SADC, TFTA, AfCFTA) yatakumbwa na changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni ubinafsi tu wa wana wa Afrika wenyewe.
(viii) Wanamichezo waafrika/wenye asili ya Afrika popote walipo wataendelea kuiteka Dunia.
(ix) Tabia ya"omba omba" itazagaa kuanzia kitaifa hadi ngazi ya mtu mmoja mmoja, bila kujali nafasi ya mtu katika uongozi wa nchi, dini au familia.
(x) Wengi wa wana wa Afrika wataaminishwa na manabii wa uongo kuwa changamoto za maisha yao zitaondoka kupitia Nyumba za Ibada. Wengi watanasa katika mtego huu.
(xi) Pamoja na misukosuko hiyo wana wa Afrika wataendelea kuthamini UTU kuliko watu wa mataifa nje ya Afrika.
(xii) Wana wa Afrika wataendelea kulinda uhuru wa bendera kwa mbwembwe zote na mshikamano.
Waungwana, je itakuwa vema kuyapuuza hayo ya wapiga ramli kuhusu Afrika kwa kuwa ramli hizo zimejikita kwenye mengi mabaya au ni vema tuzitafakari mapema na kuchukua hatua stahiki, ili mabaya tajwa yasitokee?
Karibu 2020.