African Universities Score Poorly in World Rankings!

African Universities Score Poorly in World Rankings!

msimuoneee, ikiwa ni top african, kwani inawezekana chuo kikawa kizuri kwa africa halafu kibaya kwa dunia, si wanachukua ranking zilezile za duina...Nairobi university is the third in east africa. Makerere has overtaken University of Dar just these past two years, Dar was the best in East africa. Kenya hawawezi kuringana na yeyote hapa east africa, kwasababu elimu yao ni mfu. inakujaje kichwani mtu anaingia university baada ya kufika form four...thats rediculous....Uganda and tz wanasoma form one to form six ndio wanaenda chuo. ndio maana ni watu waliofeli tz tu ndo wanaenda kujiunga na vyuo vya Kenya, waliofaulu hawawezi kwenda kusoma kenya hata siku moja. wana elimu laini isiyo na thamani sana wanachofurahia ni kujaza wanafunzi ili waonekane kama wanao wasomi wengi, kumbe wasomi wao ni mabom.

Mfumo wa elimu ya Kenya ni kama Marekani meaning K-12(Kindergarten to grade 12). So hiyo siyo sababu ya elimu ya Kenya kuwa nzuri zaidi. Unless una taka kusema kwamba sisi Tanzania tunaoenda mpaka form six tuna elimu nzuri zaidi kuliko Wamarekani ambao wanaienda mpaka grade 12(form four kwa huku).
 
African varsities score poorly in world rankings

PIX2.jpg


A past graduation ceremony at Africa University, Nairobi. Kenyan universities again fared dismally in the seventh world universities ranking released on Thursday by the British Times Higher Education.​


By BENJAMIN MUINDI,
Posted Thursday, September 16 2010 at 21:09

Five elements of higher education were considered, including the volume of research undertaken and how the institutions were relevant to the job market.

Others were the number of students admitted against that of academic staff, diversity on campus — a sign of how global an institution is in its outlook, and the impact of the research conducted.

“The ability of a university to attract the very best staff from across the world is key to global success,” said lead researcher Ann Mroz.

“Institutions with a high density of research students are more knowledge-intensive, and the presence of an active post-graduate community is a marker of a research-led teaching environment

On research, the survey said the number of papers published in academic journals were considered as it gave an idea of an institution’s ability to get papers published in quality peer-reviewed journals.

“Institutions that published fewer than 50 papers a year have been excluded from the ranking,” the survey said, signifying the reason why Kenyan universities, and the region in general, may have scored so badly. “African universities face enormous challenges,” argued Prof Goolam Mohamedbhai, former secretary general of the Association of African Universities.

“Africa inherited an education system that was a carbon copy of its colonisers. It is now expected to compete on a completely non-level playing field. Not only is this unfair, it is also inappropriate.”

But Prof Mohamedbhai argues that African universities do not need to be ranked in the global setting.

“Their mission should be to produce the appropriate manpower required for Africa’s development, to undertake research that is of direct relevance to Africa.”

He adds: “This may not be acceptable for publication in the best scientific journals — and to reach out to assist the communities in the many challenges they are facing, especially poverty reduction.”

Daily Nation:*- News*|African varsities score poorly in world rankings

Jamani, maembe ni tofauti na machungwa... mbona wanafunzi watokeao Afrika huwa wanafaulu vizuri huku kiwanjani kuliko wenyeji wengi??? Nnahisi huku kiwanjani marerani, kutakuwa na wengi watakaobisha kuwa hii list si bora.

1. Pointi ya 'diversity' ilinichekesha... ni upuuzi wa wanaondika list bila kuielewa dunia wanayoichambua... yaani vyuo ka Harvard vimelalamikiwa kwa miaka mingi kubagua wasio weupe, na leo wao ni namba moja kwa sababu ya 'diversity' pia... hahaa - watakuambia ati weusi wengi hawafaulu ama hawana uwezo... sa mbona Joji bushi aliingia na kutokuwa mwanafunzi bora ???

2. Pointi ya 'research...' Vyuo vitano vya juu vipo ndani ya nchi tajiri - serikali inawapa fedha nyingi pamoja na vifaa vyovyote vinavohitajika. Pia kuna programs nyingi za kuleta fedha vyuoni, kuanzia na wa-alumni, kuishia na timu za mipira - ambazo pia zina-advert chuo... Kwa mfano, FIRSTCOLLINA kajadili vile Barrick hairuhusu wanafunzi... mtashangazwa ka wanaruhusu wanafunzi tokea nchini mwao hata ka si wabora kuliko wetu? ... hili ni kosa la sirikali - halitetei wala kuandaa wanafunzi kuwa wafanya kazi bora wa kesho

3. Pointi ya 'number of papers published'... vyuo vyetu vya ukulima vikiandika... vitachapwa ndani ya maJournal yao kule BBC? ... si wachapaji wanachagua vya kuandika, ama?

4. Prof Goolam Mohamedbhai amegonga ikulu bab kubwa...

* Matatizo barani mwetu ni bado twaiga wakoloni... afu tunapimwa nao kwa standard zao ambazo mara nyingi hazihusiani na maisha yetu ama utamaduni wetu ama uwezo wetu... Swali la kujiuliza, hata rankings za AFrika - nani kaziandika? mkoloni ama mwananchi wa bara letu? ... nuff said
 
msimuoneee, ikiwa ni top african, kwani inawezekana chuo kikawa kizuri kwa africa halafu kibaya kwa dunia, si wanachukua ranking zilezile za duina...Nairobi university is the third in east africa. Makerere has overtaken University of Dar just these past two years, Dar was the best in East africa. Kenya hawawezi kuringana na yeyote hapa east africa, kwasababu elimu yao ni mfu. inakujaje kichwani mtu anaingia university baada ya kufika form four...thats rediculous....Uganda and tz wanasoma form one to form six ndio wanaenda chuo. ndio maana ni watu waliofeli tz tu ndo wanaenda kujiunga na vyuo vya Kenya, waliofaulu hawawezi kwenda kusoma kenya hata siku moja. wana elimu laini isiyo na thamani sana wanachofurahia ni kujaza wanafunzi ili waonekane kama wanao wasomi wengi, kumbe wasomi wao ni mabom.

Mpeni Sifa Yesu: Hapana masahihisho ni lazima nikupe. Sio kweli Kenya wanaingia University kwa kidato cha nne. Wao wana mfumo tofauti na sisi, ambao unakubalika kimataifa. Mwanafunzi ili aweze kustahili kwenda kusoma chuo kikuu inabidi amesoma Miaka 12 walau na akimaliza digrii ya kwanza iwe ni jumuisha ya walau miaka 15. Sasa angalia utaona kule Kenya wana mtindo wa 8-4-4, yaani miaka 8 pirmary (darasa la 1-8) halafu Sekondari miaka 4 na Chuo Kikuu ni miaka 4. Kwa hivyo mhitimu wa Kenya system atakuwa amekaa shuleni miaka 16. Tanzania tuna mfumo wa 7-6-3 yaani primary miaka 7, sekondari miaka 6 na CHuo kikuu 3, mhitimu wetu atakuwa amesoma miaka 16 kama wa kenya.

Lakini kuna kozi maalum ambazo mhitimu anakaa muda mwingi shuleni baada ya elimu ya sekondati, k.m daktari ni kozi ya miaka 5, architecture miaka 5, pharmasia 5 au 4, nurse 4, engineer 4, surveya kama wale wa Ardhi 4 nk.

Kigezo kinachotumia sio muda wa kufundisha ni kazi za walimu yaani publications, umaarufu wa walimu na tafiti. Kwetu huku tumelala sana, hata UDSM wanaonekana onekana sio kwa sababu ya wale mainjinia bali wanasheria, wale watu wa Arts hasa Saikolojia na ELimu ambao kwa kweli wamekuwa wakichapisha sana, ehhh nisisahu na Sayansi na vitengo vile mabli mbali vya tafiti na elimu mwendelezo
 
Mfumo wa elimu ya Kenya ni kama Marekani meaning K-12(Kindergarten to grade 12). So hiyo siyo sababu ya elimu ya Kenya kuwa nzuri zaidi. Unless una taka kusema kwamba sisi Tanzania tunaoenda mpaka form six tuna elimu nzuri zaidi kuliko Wamarekani ambao wanaienda mpaka grade 12(form four kwa huku).

1. Mtanzania alielimika bora na kumaliza form four ama form six kaelimika bora kuliko Mmarekani aliyemaliza G12. Wao wana-style za chuo, kwa hiyo - mwanafunzi anaweza kumaliza masomo ya Physics akiwa grade 10 halafu ka aenda chuoni kusomea Physics - keshasahau mengi... sisi bongo tunaendelea na Physics tokea mwanzo hadi mwisho wa form four ama six - kwa hiyo tukisoma physics chuoni, bado tupo fresh... I personally seen and experienced this when taking Calc I - yaani hata waliosoma preCalc walizubaishwa sana na ma-algebra, trig na mengineyo - building blocks to executing derivatives and integrations, etc

2. Mkuu Mwanafalsafa - mie naamini kuwa waKenya wananufaika na kuelimika kiBBC tokea shule za msingi - wanaelewa lugha za chuo bora kuliko sisi wengi waTanzania ... yaani nilishuhudia vile sisi tunavoanza shule za sekondari, wengi ni ka wanaanza darasa la kwanza... hawaelewi so subsequently, wengi wana-memorise kupasi mitihani... Jah know swali likibadilishwa lugha, wanazubaishwa... Ni maoni yangu kuwa sisi waTanzania, masters of swahili, tuna uwezo wa kukua waswahili... siku hizi hata wapolipoli wanakuwa wakielewa kiswahili hata kabla ya kuingia mashuleni... labda zamani mwalimu Nyerere alihisi wanavijiji wengi hawakujua kiswahili bora, ila siku hizi - sidhani hii ni kesi... maoni yako mkuu?
 
Kwa nchi kama Tz, kila kitu kinaendeshewa kisiasa,bodi ya mikopo, lecturers na maamuzi mengi ya bodi za vyuo yanafanywa kisiasa zaidi.Mfano mzuri ni mwaka huu vyuo havifunguliwi mpaka uchaguzi upite,gap la miezi miwili hilo,haliwezi kufidiwa.
Mpaka ifikie wakati tuweze kutenganisha siasa na mambo mengine yenye maslahi kwa taifa kama elimu,hapo ndipo tutaweza kupiga hatua mbele.

hii ni pointi... kwa nini vyuo vyafungwa kwa sababu ya uchaguzi ???? ...afu, likely, watachaji wanafunzi ka vile hawajapitwa na miezi miwili... mara nyingine mie hufikiriaga kwamba hawa viongozi wetu wanaopenda kunenepea na kuzeeka "kazini" hawataki elimu zitakazindua wapinzani... ama?
 
Tatizo la university za kiafrika ni kuwa wanafanya tafiti nyingi mno, utashangaa lakini hizi zinawekwa makabatini au ofisi za serikali, hawaziweki mahali ambapo zitaonekana, na kusomwa na wenzao. Ukiangalia na Max aliwahi kutoa ushuhuda hapa websites za universities zetu ni HOVYO kabisa, hata unashangaa kama wana wataalamu wa IT. Lakini ukienda huko utakuta wana kitengo kabisa na wanafundisha IT tena kali kali kweli, lakini waheshimiwa wale hawaweki chochote kwenye website yao.

Mara nyingi mimi nimefikiri ni uwezo wa fedha wa kumaintain hizo websites. Lakini kumbe si hivyo. Ni UCHOYO! Nina marafiki zangu kwenye hivyo Vyuo, nawatumia soft copy ya mada niliona zinawafaa, unamtumia mtu moja ukitegemea atawaonyesha wenzake, wapi Bwana akishaisoma anakaa kimya. Ukikutana naye ataisifia ilivyokuwa nzuri, ukimuuliza kama aliisambaza anajibu, hapana ile si ilikuwa nakala yangu. NI NANI ANAMTEGEMEA ATAWAPASHA WENZIE, MIYE NILIYE MBALI!

Sitaji Chuo lakini kuna Chuo Kikuu kipya kule Bongo, wana publications kibao, wana tafiti nzuri zenye mengi mno, wana walimu wabobeaji katika fani zao, fani zao ni za pekee Africa hakuna mithil yake. Kwa kuwa viongozi wao wamekaa kisiasa inapokuja kwenda Sabasaba maonyesho ni lazima waende ingawaje wanapurukushwa dakika za mwisho - hata pesa maskini wanapata kwa shida kwa ajili ya kununua vifaa vya kuandaa maonyesho. Lakini wao ni vinara katika maonyesho tangu yameanza. Sasa tembelea tovuti yao,,,,UTAPATWA NA MACHOZI! UKIWASEARCH HUMU KWENYE MITANDAO KUPITIA UNIVERSITIES ZINGINE HASA ZA ULAYA NA MAREKANI WAMEJAZANA KIBAO

Sasa hawa wanaweza wakawa wa kwanza Africa lakini kwa kuwa wameweka vichwa vyao chini wakiangalia magoti yao yanafanana ni nani atawaona. Tena wana links na establishments nyingi mno duniani lakini wanajitangaza kwa Chama tu!!!!! Habari ndiyo hio WALA MSIOGOPE UNIVERSITIES ZETU SIKO MBALI ILA TU UONGOZI NA UJUHA WA KUTO-MARKET KAZI ZAO
 
Back
Top Bottom