Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Afisa Tarafa ya Chag'ombe Al Hajj Saadat Mtware amewahamiza wananchi kujitahidi katika kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ikiwa leo ni siku ya mwisho wa uandikishaji huo.
Al Hajj Mtware akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Temeke Mhe Sextus Mapunda katika Iftra maalum iliyoandaliwa na Diwani wa Kata ya Sandali Mhe Christopher Kabalika amewataka wananchi ambao bado hawajajiandikisha kutumia fursa ya siku ya leo March 23,2025 kufika katika vituo vya uandikishaji kujiandikisha ili mwezi Oktoba katika Uchaguzi Mkuu wananchi wawe na sifa za kuchagua viongozi.
Al Hajj Mtware akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Temeke Mhe Sextus Mapunda katika Iftra maalum iliyoandaliwa na Diwani wa Kata ya Sandali Mhe Christopher Kabalika amewataka wananchi ambao bado hawajajiandikisha kutumia fursa ya siku ya leo March 23,2025 kufika katika vituo vya uandikishaji kujiandikisha ili mwezi Oktoba katika Uchaguzi Mkuu wananchi wawe na sifa za kuchagua viongozi.