Fitinamwiko
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 4,803
- 1,419
Good, next time Mwema akampige vibao Chande. Policcm wapo juu ya sharia na mahakimu wakome kujipendekeza kwa serikali ya CCM
![]()
Chande fanya ziada kulinda usalama wa mahakimu
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Lushoto Wilson Yona (35), amekiona cha moto kwa kile kilichodaiwa kushambuliwa kwa kupigwa vibao, mateke na ngumi na Mkuu wa Upelelezi wa wilaya hiyo, wakati akitekeleza wajibu wake kazini. Tukio hilo la aina yake lilitokea saa 2:16 asubuhi ofisini kwa hakimu huyo, katika Mahakama ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga wakati akiwa anaandika hukumu za washtakiwa wengine.
- Ni Mkuu wa Upelelezi aliyemnasa vibao, mateke na ngumi akiwa ofisini
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Afisa Upelelezi mkoa wa Tanga, Azizi Kimatta, alisema hakimu huyo baada ya kupata maumivu alipewa fomu ya PF3 kwa ajili ya matibabu iliyotolewa na polisi Na. 5224 PC Hamis. Akiongea na NIPASHE Jumapili, kuhusu mkasa huo, hakimu huyo alisema akiwa ofisini kwake Machi 22, mwaka huu, mkuu huyo wa upelelezi alimfuata na kuanza kumshambulia akimtuhumu kuwa hajui kufanya kazi yake vizuri.
Hakimu alidai kuwa pamoja na polisi kukataa kufungua jalada la kesi kwa madai ya kumlinda bosi wao, anakusudia kutumia njia nyingine ya kufungua kesi hiyo. "Amenishambulia sana kwa ngumi, vibao na mateke utadhani mhalifu eti anadai kuna watuhumiwa nimewapatanisha na walalamikaji wakati suala la kupatanisha ni la jeshi la polisi. "Nikamwambia sikutambui namfahamu mwendesha mashtaka wako mwambie aje nimfahamishe, na ndipo alipoanza kuniporomoshea kipigo kama mhalifu", alidai hakimu huyo.
NIPASHE Jumapili ilimtafuta mtuhumiwa anayejulikana kwa jina la Jumanne Juke na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constantino Massawe bila mafanikio. Hata hivyo, Afisa Upelelezi, Kimatta aliimbia NIPASHE kuwa suala hilo linaendelea kufanyiwa uchunguzi na polisi.
walichapwa viboko walimu, watoto wamepata sifuri, sasa wanapigwa mahakimu, ngoja tufungwe...
Hapo Hakimu kama kweli alipigwa basi alijitakia kwa sababu huwezi kumwambia mkuu wa upelelezi ambaye ndiye huandikia majalada kuja mahakamani kuwa hamtambui ila mwendesha mashtaka aliyechini ya Mkuu wa upelelezi, hapo kuna ukweli kuwa mrungura ulitembea na huenda alikula na mwendesha mashtaka, hata hayo majibu aliyotoa yanatosha kuonyesha jeuri, kipigo alistahili kwa sababu mahakimu wengi wanaharibu kesi baada ya kupokea rushwa
Unafanywa uchunguzi gani tena?
Tanga kuna laana gani.Mara mkuu wa wilaya Korogwe kamtukana Mwanasheria,Mkuu wa wilaya Tanga kapigana,kataka kumuweka ndani Padre, Mkuu wa upelelezi Lushoto kampiga Hakimu.Mkoa wa Tanga unatakiwa kufanyiwa maombi.heri wapigane wenyewe kwa wenyewe
Lilianza kwa walimu sasa limehamia mahakamani,siku hizi mtu akipata mafunzo na kuwa na uhakika wa kulindwa basi anaweza fanya lolote,eti wanafanya upelelezi..jamani upi tene kama kufungua jalada tu nongwa?TUTAPIGANA SISI ZAIDI YA RWANDA SIKU NAINGOJA KWA HAMU.